The Africa Project

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

The Africa Project (kwa Kiswahili: Mradi wa Afrika) ni shirika la kujitolea lisilolenga faida lililoanzishwa na watu wanaojitolea mnamo 2005 ambalo linasaidia mipango na huduma za ufikiaji katika mkoa wa KwaZulu-Natal nchini Afrika Kusini.[1]

Shirika hilo linajitahidi kushughulikia umaskini uliokithiri, VVU, kifua kikuu, utapiamlo, na masuala mengine ambayo yanaathiri watoto na familia katika maeneo ya vijijini katika nchi ya Afrika Kusini. The African Project linafanya kazi na asasi zisizo za kiserikali za mitaa ambao hutoa huduma katika jamii zao ikiwa ni pamoja na Mpango wa Kufikia wa Sizanani,[2] huko Nkandla Afrika Kusini,pia ni Kituo cha Huduma cha Duduza,[3] huko Westbank, Afrika Kusini. Shirika la The African Project linakaribisha wale ambao wanataka kuleta mabadiliko katika maisha ya watoto na familia barani Afrika. "Pamoja, kuna maisha mengi sana tunaweza kubadilisha!"

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. "The Africa Project | Together, there are so many lives we can change!" (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2021-08-08. 
  2. "Sizanani Outreach Programme". www.sizananioutreach.com. Iliwekwa mnamo 2021-08-08. 
  3. "Nakala iliyohifadhiwa". Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2019-07-31. Iliwekwa mnamo 2021-08-08.