Nazareti
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Nazareti (الناصرة kwa Kiarabu, נצרת kwa Kiebrania) ni mji wenye watu 65.000 upande wa kaskazini wa nchi ya Israeli, ambao kihistoria unajulikana kama Galilaya.
Wakazi wengi ni raia wa Israeli wanaoongea Kiarabu na kufuata dini za Uislamu (68,7%) na Ukristo (31,3%).
Nazareti unajulikana kama mji walipokulia Bikira Maria na mwanae Yesu Kristo, ambaye kadiri ya Injili, ingawa alizaliwa Bethlehemu, alikuwa anatajwa kama Mnazareti.
Viungo vya nje[hariri]
- The New Official site of Nazareth City
- Nazareth City Website
- Nazareth in the Jewish Encyclopedia
- W.R.F. Browning, Oxford Dictionary of the Bible: Nazareth