Algae
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Mwani)
Algae (umoja ni alga, uwingi algae; pia: mwani) ni jina la kundi kubwa la viumbehai vidogo kati ya protista sana vinavyofanana na mimea. Zina uwezo wa kujilisha kwa njia ya usanisinuru yaani hutengeneza chakula chao kwa msaada wa mwanga wa jua.
Kuna aina nyingi sana za algae nyingine zina seli moja tu na nyingine zina seli nyingi. Aina kubwa zinajulikana kama mwani za baharini. Katika uwezo wa usaninisinuru zinalingana na mimea lakini hukosa viungo vingi vilivyo kawaida kati ya mimea hivyo katika taksonomia au mpangilio wa spishi hazihesabiwi kati ya mimea.
Algae hazina majani, mizizi na viungo vyingine vya mimea.