Modiri Marumo

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Modiri Marumo (alizaliwa Gaborone, 6 Julai 1976) ni mchezaji wa soka wa zamani wa Botswana ambaye alikuwa anacheza kama kipa.

Kazi ya klabu[hariri | hariri chanzo]

Marumo alianza kazi yake na timu ya Jeshi la Ulinzi la Botswana.

Alisaini katika klabu ya Misri iitwayo Haras El Hodood mwezi Februari 2008, akiwa mchezaji wa kwanza wa Botswana kucheza katika ligi ya Misri.

Alihamia Afrika Kusini mwezi Agosti 2010, akisaini katika klabu ya Bay United.

Alimaliza kazi yake na Polokwane City, hukohuko Afrika Kusini.

Makala hii kuhusu mchezaji mpira fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Modiri Marumo kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.