Millard Ayo

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Millard Ayo.

Millard Afrael Ayo (alizaliwa Arusha, 26 Januari, 1986) ni mtangazaji, mwandishi wa habari na mwanablogu kutoka nchini Tanzania.

Millard anafahamika sana kwa kipindi chake cha Amplifier katika redio ya Clouds FM Archived 14 Aprili 2019 at the Wayback Machine.. Alianza kutambulika baada ya kujiunga na ITV/Radio One mwaka 2008 kabla ya mwaka 2010 kujiunga Clouds FM.

Millard Ayo, vilevile anamiliki tovuti ya habari mbalimbali za ndani na nje ya Tanzania inayoitwa millardayo.com ambayo ni moja ya tovuti bora nchini Tanzania. Mbali na hayo, Millard anayo idhaa katika YouTube inaitwa Ayo TV. Idhaa hiyo inatoa habari mbalimbali na inatenda kama televisheni (TV) Mtandaoni.[1]

Ayo amekuwa maarufu Afrika Mashariki kwa wepesi wa kutoa habari kwa muda, matukio kama: siasa, michezo na burudani amekuwa akiyafikisha kwa watu mbalimbali kwa wakati husika.

Tanbihi

  1. Wasifu wa Millard Ayo katika wavuti yake
Makala hii kuhusu mwandishi fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Millard Ayo kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.