Marumaru

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Uchoraji asilia waonekana kwenye uso wa marumaru iliyokatwa na kusuguliwa.
Sanamu ya marumaru yamwonesha mungu wa Kiroma Venus

Marumaru (pia: marmar - kutoka kar. مرمر) ni mwamba wa gange uliobadilika kutokana na joto na shindikizo ndani ya ganda la dunia katika kipindi cha miaka mamilioni. Kikemia ni hasa CaCO3.

Ni jiwe gumu sana inayopatikana katika rangi mbalimbali.

Hupendwa sana kama jiwe la ujenzi hasa kama ni nyeupe. Kama ni haba katika eneo fulani hutumiwa kama mapambo tu yaani kuta zafunikwa kwa marumaru. Jiwe lenye rangi mbalimbali hutumiwa kwa sakafu katika majengo muhimu au kama mapambo ya kuta za ndani.

Tangu kale marumaru ilitumiwa pia kwa sanamu.


[hariri] Tovuti za Nje

WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:


WikiLettreMini.svg Makala hiyo kuhusu "Marumaru" bado ni mbegu. Unaweza kusaidia kuikuza kwa kubofya kitufe kilichoandikwa "hariri".

Ikiwepo makala kuhusu Marumaru kwa lugha nyingine, unaweza kuitafsiri kwa Kiswahili.