Marumaru
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Marumaru (pia: marmar - kutoka kar. مرمر) ni mwamba wa gange uliobadilika kutokana na joto na shindikizo ndani ya ganda la dunia katika kipindi cha miaka mamilioni. Kikemia ni hasa CaCO3.
Ni jiwe gumu sana inayopatikana katika rangi mbalimbali.
Hupendwa sana kama jiwe la ujenzi hasa kama ni nyeupe. Kama ni haba katika eneo fulani hutumiwa kama mapambo tu yaani kuta zafunikwa kwa marumaru. Jiwe lenye rangi mbalimbali hutumiwa kwa sakafu katika majengo muhimu au kama mapambo ya kuta za ndani.
Tangu kale marumaru ilitumiwa pia kwa sanamu.
Tovuti za Nje [hariri]
- Inlaid marble
- Tips for cleaning marble
- Learning to carve by Marc Levoy.
- Marmo Qarry in the Massa-Carrara region, Italy
| Makala hii kuhusu mambo ya kemia bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Marumaru kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |