Mahabharata

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Nakala ya picha ya vita vya Kurukshetra

Mahabharata (kwa Kisanskrit महाभारत) ni utendi mkuu mmojawapo wa Kisanskriti wa Uhindi ya zamani, mwingine ukiwa ni Rāmāyaṇa. Utendi huu ni sehemu ya itihāsa (au "historia") ya Kihindu na inaunda sehemu muhimu ya hadithi za kale za Kihindu.

Ina umuhimu mkubwa kwa utamaduni wa Bara dogo la Uhindi, na ni nakala muhimu ya Uhindu. Majadiliano yake kuhusu malengo ya kibinadamu (dharma au wajibu, artha au lengo, kāma, radhi au hamu na moksha au ukombozi) unachukua nafasi katika utamaduni wa kijadi, ukijaribu kuelezea uhusiano kati ya mtu binafsi na jamii na ulimwengu (asili ya 'nafsi') na utendaji kazi wa karma.

Mada yenyewe inaweza kutafsiriwa kama "hadithi kuu ya nasaba ya Bhārata". Kulingana na ushuhuda wa Mahabharata inapanuliwa kutoka toleo fupi zaidi linaloitwa Bhārata lenye mistari 24,000.[1]

Kijadi, uandishi wa Mahabharata ulihusishwa na Vyasa. Kumekuwa na jitihada nyingi za kugundua ukuajia wake wa kihistoria na vipengele mbalimbali ndani yake. Vipengele vyake vya kwanza kabisa labda vinaanza katika kipindi cha Kivedi (karne ya 8 KK)[2] na pengine utendo huo ulifikia fomu yake ya mwisho wakati kipindi cha Gupta kilipoanza mnamo (karne ya 4KK).[3]

Ikiwa na karibu mistari laki moja, vifungu virefu vya kinathatari, na karibu maneno milioni 1.8 kwa jumla, Mahabharata ndilo shairi ndefu zaidi la utendi Duniani.[4] Ni takriban mara kumi urefu wa Utendi wa Iliadi na Odisei zinapouanganishwa,[5] utendi huo una urefu ambao ni karibu mara tano zaidi wa Kichekesho cha Kimungu cha Dante na karibu mara nne urefu wa Ramayana. ikijumuisha Harivaṃśa, utendi wa Mahabharata una jumla ya mistari 90,000.

Mawanda[hariri | hariri chanzo]

Krishna, Arjuna katika eneo la Kurukshetra,katika mchoro huu uliofanywa kati ya karne ya 18 na 19.

Mbali na hadithi yake ya utendi kuhusu viota vya Kurukshetra na hatma ya Wakaurava ma Wapandava, utendi wa Mahabharata una mambo mengi ya kifalsafa na ibada, kama vile Shrimad Bhagavad Gita (6.36-42) yenye kiwango cha juu sana cha maudhui ya kifalsafa na kidini, au majadiliano kuhusu "malengo manne ya maisha " au purusharthas (12.161). Kipengele hiki cha mwisho kinaorodheshwa kama dharma (kitendo chema), artha (kusudi), kama (radhi), na moksha (ukombozi).

Bali na kuwa na mambo mengi ya thamani ya kifalsafa na kidini, utendi wa Mahabharata pia unaonyesha utata wa uhusiano wa kibinadamu katika vipimo mbalimbali vonavyoweza kuhusishwa na utata wa kisasa wa uhusiano wa binadamu.

Mahabharata inadao kujumuisha watu wote katika mwanzo wa kitabu chake cha kwanza cha "parva": "Kile kinachopatikana hapa, kinaweza kupatikana kwingine. Kile ambacho hakipatikani hapa hakitapatikana kwingine." Miongoni mwa maandiko makuu na hadithi ambazo ni sehemu za Mahabharata ni hizi zifuatazo (ambazo hudhaniwa kuwa kazi tofauti):

  • Bhagavad Gita katika kitabu cha 6 (Bhishmaparva): Krishna anamshauri na kumfunza Arjuna wakati ambapo ana mashaka mengi.
  • hadithi ya Damayanti, ambayo wakati mwingine hutiwa (Nala na Damayanti) katika kitabu cha 3 (Aranyakaparva), ni hadithi ya mapenzi.
  • Toleo lililofupishwa la Ramayana, katika kitabu cha 3 (Aranyakaparva)
  • Rishyasringa, mvulana mwenye pembe na rishi , katika kitabu cha 3 (Aranyakaparva)

Arshia Sattar anasema kuwa kaulimbiu ya Mahabharata, na hata Ramayana, ni kufichwa na Umungu wa Krishna na Ram na kufichuliwa kwake mtawalia.[6]

Historia ya nakala na muundo wake[hariri | hariri chanzo]

Utendi unahusishwa na Vyasa, ambaye pia ni mmoja wa wahusika wakuu wa kinasaba katika utendi wa Mahabharata. Sehemu ya kwanza ya Mahabharata inataja kuwa ilikuwa Ganesha ambaye, aliandika nakala wakati Vyasa alipomuomba kufanya hivyo. Ganesha anasemekana kukubali kuandika nakala ile ikiwa tu Vyasa hangesita kuongea. Vyasa alikubali, ikiwa tu Ganesha angechukua muda wake kuelewa kile kilichokuwa kikisemwa kabla ya kukiandika.

Utendi wa Mahabharata unatumia muundo wa hadithi ndani ya hadithi, ambayo pia hujulikana kana hadithi za kifremu, amabazo ni maarufu katika maadiko mengi ya Kihindi ya kidini na maandikio ya kawaida pia. Inasomewa mflame Janamejaya ambaye ni kitukuu cha Arjuna, kutoka Vaisampayana, mfuasi wa Vyasa. Kusomwa kwa Vaisampayana kwa Janamejaya pia unasomwa tena na mtoaji hadithi mtaalamu anayeitwa Ugrasrava Sauti, miaka mingi baadaye mbele ya mkusanyiko wa wahenga

Kwa kawaida, inadhaniwa kuwa urefu kamili wa utendi wa Mahabharata umeongezeka katika kipindi kirefu.[who?] Utendi wa Mahabharata wenyewe (1.1.61) unatofautisha sehemu ya msingi yenye mistari 24,000, Bharata yenyewe, kinyume na vipengele zaidi vilivyoongzwa, huku Ashvalayana Grhyasutra (3.4.4) unafanya tofauti sawa bayana. Kulingana na Adi-parva ya Mahabharata (shloka za 81, 101-102), nakala hapo awali ilikuwa na mistari 8,800 wakati uilipotungwa na Vyasa na ilijulikana kama Jaya (Ushindi), ambayo baadaye ilikuja kuwa mistari 24,000 katika Bharata iliyosomwa na Vaisampayana, na mwishowe zaidi ya mistari 90,000 katika Mahabharata iliyosomwa na Ugrasrava Sauti.[7]

Utafiti kuhusu utendi wa Mahabharata umefanya juhudi kubwa ya kutambua na kujua wakati ambao wa vipengele mbalimbali katika nakala vilivyoandikwa.

Hali ya nakala imetazamwa na wasomin wa mapema kuhusu utamaduni wa Kihindi kama yenye kukosa mpangilio maalum na yenye kuundwa kishaghalabaghala. Hermann Oldenberg (1922) alifikiri kuwa shairi la hapo awali lazima lilikuwa na "nguvu nyingi za kitanzia", lakini alikataa matazamo kuwa nakala zima ilikuwa "shaghalabaghala "[onesha uthibitisho]

Marejeo ya mwanzo kabisa kuhusu utendi wa Mahabharata na maandiko yake ya kimsingi ya Bharata yanarudi nyuma hadi wakati wa Ashtadhyayi (sutra 6.2.38) of Pāṇini (fl. Karne ya 4 KK), na katika "Ashvalayana Grhyasutra (3.4.4).[onesha uthibitisho] Hili linaweza kudokeza kuwa mistari 24,000 ya kimsingi, inayojulikana kama Bharata, na hata toleo la awali la Mahabharata lilikuwa na vipengele vilivyoongezwa, yaliandikwa katika karne ya 4KK. Sehemu za mistari 8,800 ya Jaya' ya awali pengine inarudi nyumahadi miaka ya kati ya karne ya 9 na 8 KK.[2]

Utendi wa Mahabharata unadhananiwa kuundwa kabla ya utendi wa Kigiriki wa Iliadi, na baadhi ya vipengele vya utendi wa Mahabharata vinasemekana kufanana kwa karibu na hadithi la Iliad. Christian Lassen, katika kitabu chake Indische Alterthumskunde, alidhani kuwa marejeo mwishowe ni kuhusu huzuni wa Dhritarashtra's, majonzi ya Gandhari na Draupadi, na ujasiri wa Arjuna na Duryodhana au Karna.[8]Tafsiri hii, inayoungwa mkono katika marejeo muhimu kama vile Historia ya Fasihi ya Uhindi ya Albrecht Weber, mara nyingi imerudiwa.[9]

Baadaye, maandishi juu ya bati la shaba katika Maharaja Sharvanatha (533-534) kutoka Khoh (Wilaya ya Satna, Madhya Pradesh) inaelezea utendi wa Mahabharata kama "mkusanyiko wa mistari 100,000" (shatasahasri samhita). Ufupisho wa mwili huu mkubwa wa nakala ulifanywa na baada ya kanuni rasmi, zikitilia mkazo nambari 18[10] na 12. Kuongezwa kwa sehemu za mwisho unaweza kutufanya tujue tarehe yake kwa kuangalia kutokuwepo kwa Anushasana-parva kutoka kwa MS Spitzer, nakala nzee zaidi iliyopo ya Kisanskriti ya kifalsafa iliyoandikwa wakati wa karne ya kwanza. Mganwanyiko mbadala kwa 20 parvas unaonekana kuwepo kwa kipindi kirefu. Mgawanyiko wa parva ndogo 100(zinazotajwa katika Mbh.1.2.70) ni nzee zaidi, na parva nyingi zinapewa majini yanayoambatana na mojawapo ya parva ndogo ndani yake. Harivamsa ina sehemu mbili za mwisho za parva ndogo 100, na ilitazamwa kama tamatisho la (khila) la utendi wa Mahabharata wenyewe na wafupishaji wa parva 18.[onesha uthibitisho]

Parva 18[hariri | hariri chanzo]

Mgawanyiko wa parva 18 ni kama ifuatavyo:

Parva mada parva ndogo yaliyomo
1 Adi Parva (Kitabu cha Mwanzo) 1-19 Jinsi Mahabharata ilipoanza kuhadithiwa na Sauti kwa marishi waliokusanyika katika eneo la Naimisharanya. Kuhadithiwa kwa utendi wa Mahabharata katika sarpasattra ya Janamejaya na Vaishampayana katika Takṣaśilā. Historia ya Jamii ya Kibharata inaelezewa kwa kina na parva pia inafuata historia ya jamii ya Kinhrigu. Kuzaliwa na maisha ya mapema ya wana wa wafalme wa Kuru. (adi inamaanisha ya kwanza)
2 Sabha Parva (Kitabu cha Eneo la Kukusanyika) 20-28 Maya Danava anajenga ikulu na mahakama (sabha), katika eneo la Indraprastha. Maisha katika ikulu, Yudhishthira's Rajasuya Yajna, mchezo wa daisi, na hatimaye uhamisho wa Mapandava.
3 Vana Parva pia Aranyaka-parva, Aranya-parva (Kitabu cha Msitu) 29-44 Miaka kumi na miwili uhamishoni msituni (aranya).
4 Virata Parva (Kitabu cha Virata) 45-48 Mwaka mahakama ya Virata. Mhusika alivaa nguo zilizomfanya asitambulike.
5 Udyoga Parva (Kitabu cha Jitihada) 49-59 Maandalizi ya vita na jitihadaza kufanya amani kati ya Makuru na Mapandava ambayo mwishowe hazifanikiwi (udyoga ni neon linalonaanisha jitihada au kazi).
6 Bhishma Parva (Kitabu cha Bhishma) 60-64 Sehemu ya kwanza ya vita vikuu, huku Bhishma akiwa kamanada wa vita wa Makaurva na kuanguka kwake katika kitanda chenye mishale.
7 Drona Parva (Kitabu cha Drona) 65-72 Vita vinaendela, huku Drona akiwa kamanda. Hiki ndicho kitabu kikuu kuhusu vita. Wengi wa mashujaa wakuu wanakufa kufikia mwisho wa kitabu hiki.
8 Karna Parva (Kitabu cha Karna) 73 Vita tena, huku Karna akiwa ndiye Kamanda.
9 Shalya Parva (Kitabu cha Shalyas) 74-77 Siku ya mwisho ya vita huku Shalya akiwa kamanda. Pia safari ya kidini ya Balarama inaelezewa kwa kina kuelekea mto Sraswati na vita vya rungu kati ya Bhima na Duryodhana ambavyo vinafanya vita kusiha, kwa sababu Bima anuwa Duryodhana kwa kumgonga mapajani kwa kutumia rungu.
10 Sauptika Parva (Kitabu cha Mashujaa Wanaolala) 78-80 Ashvattama, Kripa na Kritavarma wanauwa jeshi lililosalia la Kipandava likiwa usingizini. Ni mashujaa wasabi tuu ambao wanaobaki katika upande wa Pandava na watatu katika upande wa Kaurava.
11 Stri Parva (Kitabu cha Wanawake) 81-85 Gandhari, Kunti na wanawake (stri) za Makuru na Mapandava wanaomboleza waliokufa.
12 Shanti Parva (Kitabu cha Amani) 86-88 Yudhisthira anafanywa kuwa mfalme wa Hastinapua, na maagizo kutoka Bhishama kwa mfalme aliyetakaswa upya kuhusu jamii, uhcumi na siasa. Hiki ndicho kitabu kirefu zaidi cha utendi wa Mahabharata (shanti ni neon linalomaanisha amani).
13 Anushasana Parva (Kitabu cha Maelekezo) 89-90 Maelekezo ya mwisho (anushasana) kutoka Bhishama.
14 Ashvamedhika Parva (Kitabu cha Kafara ya Farasi)[11] 91-92 Sherehe ya kifalme ya Ashvamedha (Kafara ya farasi) iliyofanywa na Yudhisthira. Ushindi wa Dunia Arjuna. Anugita anaambiwa na Krishna kuenda sArjuna.
15 Ashramavasika Parva (Kitabu cha Uhamishoni) 93-95 Vifo vya Dhritarashtra, Gandhari na Kunti kutokana na mto wa msitu wakati wanapoishi uhamishoni katika milima ya Himalaya. Vidula anakufa kabla yao na Sanjaya anaenda kuishi katika eneo la juu zaidi la Himalaya anapoombwa kufanya hivyo na na Dhritarashtra.
16 Mausala Parva (Kitabu cha Rungu) 96 Mzozano wa ndani baina ya Mayadava wakitumia rungu (mausala) na hatimaye kuangamia kwa Mayadava.
17 Mahaprasthanika Parva (Kitabu cha Safari Kuu) 97 Safari kuu ya Yudhisthira na ndugu zake kote nchini na mwishowe wao kupanda milima ya Himalaya ambapo kila Pandava anaanguka isipokuwa Yudhisthira.
18 Svargarohana Parva (Kitabu cha Kuinuka kuelekea Mbinguni) 98 Mtihani wa mwisho wa Yudhisthira na kurudi kwa Mapandava kwa ulimwengu wa kiroho (svarga).
khila Harivamsa Parva (Kitabu cha orodha ya ukoo wa Hari) 99-100 Maisha ya Krishna ambayo hayaguziwi katika parva 18 za Mahabharata.

Adi-parva inajumuisha kafara ya nyoka (sarpasattra) ya Janamejaya, ikieleza msukumo wake, na kueleza kwa undani mbona nyoka wote ambao ni hai walifaa kuharibiwa, na kwa nini licha ya hayo, bado kuna nyoka hadi wa leo. Kipengele hiki cha sarpasattra mara nyingi kilitazmwa kama hadithi inayojitegemea pekee yake iliyoongezwa katika toleo la "Mahabharata" kupitia "mvuto wa kimaudhui" (Minkowski 1991), na inaonekana kuwa na uhusiano wa karibu sana na fasihi ya Kibrahmana ya Kivedi, hasa Panchavimsha Brahmana inayoelezea sarpasattra kama ilivyofanywa hapo awali na nyoka, ambazo kati yao ni nyoka wanaoitwa Dhrtarashtra na Janamejaya, wahusika wawili muhimu wa sarpasattra ya Mahabharata, na Takshaka, jina la nyoka ambaye pia anapatikana katika Mahabharata. Shatapatha Brahmana inatoa maelezeo kuhusu Ashvamedha inayofanywa na Janamejaya Parikshit.

Kulingana na kile ambacho mhusika mmoja anasema katika Mbh. 1.1.50, kulikuwa na matoleo matatu ya Utendi, ya kwanza ikiwa ni Manu (1.1.27) iliyofuatiwa na Astika (1.3, sub-parva 5) au Vasu (1.57), mtawalia. Matoleo haya yengeweza kuhusiana na ongezeko la ' fremu' moja halafu nyingine ya majadiliano. Toleo la Vasu liliondoa muktadha wa kifremu na kuanza na hadithi kuhusu kuzaliwa kwa Vyasa. Toleo la astika liliongeza vipengele vya sarpasattra na ashvamedha kutoka fasihi ya Kibrahama, na kuanzisha neno Mahabharata, na kumtambua Vyasa kama mwandishi wa kazi hiyo.Wafupishaji wa matoleo haya pengine walikuwa wasomi wa Kipancharatrin ambao kwa mujibu wa Oberlies (1998) huenda waliweza kuwa na udhibiti wa nakala hiyo hadi kufupishwa kwake kwa mwisho. Hata hivyo, kutajwa kwa Huna katika Bhishma-parva kunaonekana kuashiria kuwa parva hii huenda ilihaririwa katika kipindi cha karne cha 4.

Muktadha wa kihistoria[hariri | hariri chanzo]

Mapu ya "Bharatvarsha" (Milki ya Uhindi) wakati wa Mahabharata na Ramayana. (Majina ya maeneo ni yameandikwa kwa lugha ya Kiingereza.)

Historia ya Vita vya Kurukshetra haieleweki. Wanahistoria wengi kama vile AL Basham alitabiri kuwa tarehe ya vita vya Kurukshetra ilikuwa Zama za Chuma za Uhindi za karne ya 10 KK. [12]

Wanahistoria wengine kama vile M Witzel pia wameonyesha ushahidi kuwa muktadha wa jumla wa utendi unarudi nyuma hadi Zama za Chuma za Uhindi ya Kivedi, ambapo milki ya Kuru ilikuwa msingi wa nguvu za kisiasa wakati wa kipindi cha kama miaka 1200 hadi 800 KK.[13] Mgogoro wa kinasaba wa wa kipindi hicho huenda ukawa msukumo uliofanya Jaya kuandikwa, msingi ambapo shana ya Mahabharata ilijengwa, huku kukiwa na vita ambavyo vilitazmwa kama tukio muhimu la zama hiyo.

Fasihi ya Kipurani inatoa orodha za koo zinazohusishwa na hadithi ya Mahabharata.

Ushahidi wa Puranas ni wa aina mbili. Katika ule aina ya kwanza, kuna taarifa ya moja kwa moja kuwa kulikuwa na miaka 1015(au 1050) kati ya kuzaliwa kwa Parikshit (mjukuu wa Arjuna) na wakati ambapo Mahapadma Nanda alipochukua mamlaka, ambayokwa kawaida hujulikana kuwa tarehe 382 KK, ambayo inaweza kutupa makadirio ya karibu 1400 KK kwa vita vya Bharata. [14] Hata hivyo, hili linaweza kuashiria kuwa vipindi virefu uongozini kwa wastani vya wafalme wanaotajwa katika orodha za koo.[15] Aina ya pili ya uchambuzi unaangalia orodha ya koo ambazo ni sambamba katika Puranas wakati wa Adhisimakrishna (kitukuu cha Parikshit) na Mahapadma Nanda. Pargiter ipasavyo alikisia vizazi 26 kwa kufanya hesabu ya wastani ya orodha 10 za kinasaba, na kuchukua miaka 18 kuwa kipindi cha wastani cha utawala, ambapo alipata makisio ya 850KK kwa Adhisimakrishna, na kwa hivyo karibu mwaka wa 950 KK kwa vita vya Bharata.[16]

B. B. Lal pia alitumia mbinu sawa lakini akitumia dhana ya kihifadhina zaidi ya utawala wa wastani kupata makisio ya mwaka 836 KK, na kulinganisha hili na ushahidi wa Kiakeolojia kutoka maeneo ya vyombo vilivyopangwa rangi ya kijivu, uhusiano ukiwa mkubwas kati ya vifaa kutoka maeneo yenye vyombo vilivyopakwa rangi ya kijivu na maeneo yaliyotajwa katika utendi.[17]

Majaribio ya kutoa tarehe kuhusu matukio kwa kutumia mbinu za akiolojia zinazojumuishwa na mbinu za kifalaki zimetoa, ikitegemea na vifungu vinavyochaguliwa na jinsi vinavyotafsiriwa, makisio kati ya wakati wa mwisho wa milenia ya 4 hadi wakati wa katikati wa milenia ya 2 KK.[18] Tarehe ya kipindi cha mwisho cha Milenia ya 4 kinarudi nyuma katika kupiga hesabu ya enzi ya Kaliyuga, kwa kuzingatia mipangilio maalum kisayari ya Aryabhata (6th century). Tarehe yake ya 18 Februari, mwaka wa 3102 KK imekuja kutumika sasna katika tamaduni za Kihindi (kwa mfano, maandishi ya Aihole inscription ya Pulikeshi II, ni ya tarehe Saka 556 = 634 KK, yanadai kuwa miaka 3735 imepita tangu vita vya Bharata kufanyika.[19]) Shule nyingine ya jadi ya wanafalaki na wanahistoria, ikiwakilishwa na Vriddha-Garga, Varahamihira (,mwandishi wa Brhatsamhita) na Kalhana (mwandishi wa Rajatarangini), wanadai kuwa vita vya Bharata viLifanyika miaka 653 baada ya zama za Kaliyuga, inayowiana na mwaka wa 2449 KK.[20]

Ushahidi wa kukisia tarehe ya vita vya Mahabharata upo. Hii ni pamoja na: maandiko ya Aihole, maandiko ya Hisse Borala ya Deva Sena na rekodi ya balozi wa Kigiriki Megasthenes. P.V. Vartak anatoa muhtasari wa kina wa ushahidi tofauti unaoweza kupatikana ili kujua tarehe ya viota vya Mahabharata.[21]

Baadhi ya wasomi wametambua usambamba kati ya Mahabharata, Ubakaji wa wanawake wa Kisabine katika Mitholojia ya Kirumi, na vita vya Æsir–Vanir katika Mythologia ya Kinorsi.[22]

Muhtasari[hariri | hariri chanzo]

Msingi wa hadithi ni mzozano kati ya nasaba mbalimbali ili kupata kudhibiti milki ya Hastinapura, miliki inayowatwaliwa na koo ya Kuru. Matawi mawili ya kidhamana ya familia yanayoshiriki katika mzozano huyo ni Kaurava na Pandava. Ingawa Kaurava ndilo tawi mwandamizi la familia, Duryodhana, Kaurava mwenye umri mwingi zaidi, ni mdogo wa Yudhisthira, Pandava mwenye umri mwingi zaidi. Duryodhana na Yudhisthira wanadai kuwa wa kwanza katika orodha ya urithi wa milki.

Mzozano unafikia kilele ambapo vita vikuu vya Kurukshetra vinatokea, ambapo Mapandava wanaibuka washindi. Vita hivyo vinaibua migogoro ya kijamaa na kirafiki, matukio ya uaminifu wa kifamilia na wajibu ukifanywa kuwa muhimu zaidi kuliko kile ambacho ni sawa, na pia kinyume cha hiki.

Mahabharata yenyewe inaisha na kifo cha Krishna, na baadaye kuisha kwa nasaba yake, na kuinuka kwa ndugu wa Kipandava kuelekea mbinguni. Pia inaonyesha mwanzo wa zama za Kihindu za Kali(Kali Yuga), zama ya nne nay a mwisho ya binadamu, ambapo maadili makuu na mawazo ya kiutu yamepotea, na binadamu anaelekea hali ya kupotea kabisa kwa haki, hatua, maadili na wema.

Vizazi vya awali[hariri | hariri chanzo]

Kiapo cha Bhishma, mchoro wa
Raja Ravi Varma

Mmoja wa mababu wa Janamejaya anayeitwa Shantanu, mfalme wa Hastinapura ana ndoa fupi na mungu wa kike anayeitwa Ganga na mwana, Devavrata (ambaye baadaye anapewa jina Bhishma), ambaye anakuwa mrithi dhahiri.

Miaka mingi baadaye, wakati ambapo mfalme anaenda uwindaji, anamuona Satyavati, binti ya mvuvi na anamuomba baba yake ruhusa kumuoa. Baba yake anakataa kukubali ndoa ile isipokuwa Shantanu akubali ahadi ya kufanya mwana yeyote atakayezaliwa na Satyavati kuwa mfalme wakati atakapokufa. Ili kutatua mtanziko wa mfalme, Devavrata anakubali kuwa hatayachukua mamlaka. Kwa sababu mvuvi hana uhakika ikiwa watoto wa mfalme wataweka ahadi hiyo, Devavrata pia anafanya nadhiri ya useja maisha yake yote kuhakikisha ahadi ya baba yake. Shantanu ana watoto wawaili na Satyavati, Chitrangada na Vichitravirya. Baada ya kifo cha Shantanu, Chitrangada anakuwa mfalme. Anaishi maisha mafupi sana ambayo hayana matukio mengi ya maana kasha anakufa. Vichitravirya, mwana mwenye unmri mdogo anatawala Hastinapura. Wakato uo huo, Mfalme wa Kāśī anapanga arranges swayamvara kwa mabinti wake watatu. Hata hivyo, hahaliki familia ya kifalme ya Hastinapur. Ili kupanga ndoa ya Vichitravirya ambaye ana umri mdogo, Bhishma anaenda Kāśī kufanya swayamvara ya mabinti watatu wa mfalme, Amba, Ambika na na Ambalika, bila kualikwa. Kwa kuwa ana nguvu, anawateka nyara kwa hasira bila kujali nia yao. Ambika na Ambalika wanakubali kuolewa na Vichtravirya. Binti wa mfalme anayeitwa Amba, anamfahamisha Bhishma kuwa angependa kumuoa Shalvaraj (mfalme wa Shalva) ambaye Bhishma alishinda katika eneo la swayamvar. Bhishma anamuwacha aende kumuoa Shalvaraj lakini Shalvaraj anakataa kumuoa, na analengwa na machozi jinsi alivyoaibishwa mbele ya Bhishma. Amba basi anarudi kumuoa Bhishama lakini anakataa kwa sababu ya nadhiri yake ya useja. Amba baada ya hapo anakasirika na anakuwa adui mkubwa wa Bhishma, na kumlaumu kwa shida yake. Baadaye anazaliwa upya kwa Mfalme Drupada kama Shikhandi (au Shikhandini) na anasababisha kumwangusha Bhishma kwa usaidizi wa Arjuna katika vita vya Kurukshetra.

Wana wa mfalme wa Pandava Kaurava s[hariri | hariri chanzo]

Wakati Vichitravirya anapokufa vila warithi wowote, Satyavati anamuomba mwanawe wa kwanza anayeitwa Vyasa kupata watoti na wajane. Ambika ambaye sasa ni mzee anafunga macho yake anapomuona, na mwanawe Dhritarashtra anazaliwa kipofu. Ngozi ya Ambalika inabadilika kuwa rangi ya kijivu na bila damu, na mwanawe Pandu anazaliwa akiwa na rangi ya kijivu na afya mbaya (neno Pandu huenda likamaanisha pia kuwa na ugonjwa ambapo mwili unabadilika rangi [1] Archived 26 Januari 2008 at the Wayback Machine.). Kutokana na changamoto za watoto wawili wa kwanza, Satyavati anamuuliza Vyasa kujaribu tena. Hata hivyo, Ambika na Ambalika wanamtuma mjakazi wao kwa chumba cha Vyasa. Vyasa anamfanya mjakazi kumzalia mwana wa tatu anayeiywa Vidura. Anzaliwa na afya nzuri na anakuwa mojawapo wa wahusika waadilifu zaidi katika Mahabharat. Anakuwa Waziri Mkuu (Mahamantri au Mahatma)kwa mfalme Pandu na Mfalme Dhritarashtra.

Wakati ambapo wana wa mfalme wanakuwa wakubwa, Dhritarashtra anakaribia kufanywa kuwa mfalme na Bhishma. Hata hivyo, Vidura anaingilia kati na kutumia maarifa yake ya siasa kufikia hitimisho kuwa kipofu hawezi kuwa mfalme. Hili ni kwa sababu mfalme ambaye ni kipofu hawezi kuwadhibiti wala kuwalinda raia wake. Ufalme unapewa Pandu kwa sababu Dhritarashtra ni kipofu. Pandu anaoa mara mbili, mke wa kwanza ni Kunti na wa pili ni Madri. Dhritarashtra anamuoa Gandhari, binti wa mfalme kutoka eneo la Gandhara, ambaye anajifuna kitambaa machoni ili ahisi uchungu anaohisi mumewe. Ndugu ya Gandhari, Shakuni, anakasirika kwa sababu ya nadhiri hizi na anaamua kulipiza kisasi kwa kuidhuru familia ya Kuru. Siku moja, wakati Panda anapopumuzika msituni, anasikia sauti ya mnyama mnyama wa pori. Analenga mshale katika mwelekeo ambapo sauti inatoka. Hata hivyo mshale unamchoma mzee mwenye maarifa anayeitwa Kindama. Kindama anamlaani Pandu kwa kumwambia kuwa ikiwa atashiriki kitendo cha ngono, atakufa. Pandu anawacha wadhifa wake na kuishi msituni pamoja na wake zake wawili, na nduguye Dhritarashtra anayachukua mamlaka, livha ya kuwa kipofu.

Mhusika msingi ni Yudhishthira ; watu wawili katika upande wake wa kushoto ni Bhima na Arjuna. Nakula na Sahadeva , mapacha, wamekaa katika upande wake wa kulia. Mke wao, katika upande wa mwisho wa kulia, ni Draupadi. Deogarh, dhehebu la Dasavatar.

Malkia mwenye umri mwingi zaidi wa Pandu, Malkia Kunti hata hivyo, alikuwa amebarikiwa na pewa mzee mwenye maarifa, Durvasa kuwa yeye angeweza kumuita mungu yeyote aliyemhitaji kwa kutumia wimbo maalum. Kunti anamuuliza Dharma mungu wa haki, Vayu mungu wa upepo, na Indra. Mungu wa mbingu wampatie wana; kwa kutumia Baraka aliyopewa na Durvasa. Anawazaa watoto watatu Yudhisthira, Bhima, na Arjuna kupitia miungu hii. Kunti anamwambia malkia mwenye umri mdogo kumliko, Madri, kuhusu wimbo huo maalum na anapata mapacha who Nakula na Sahadeva kupitia mapacha wa Kiashwini. Hata hivyo Pandu na Madri, wanashiriki ngono na Pandu anakufa. Madri anakufa katika moto wa Pandu wa mazishi kwa sababu ya kusononeka. Kunti anawalea mandugu watano, ambao kuanzia muda huo wanatambulika kama mandugu wa Kipandava.

Dhritarashtra anapata wana mia moja kupitia Gandhari, wote wanazaliwa baada ya Yudhishtira. Hawa ndio ndugu wa Kikaurava, mwenye umri mkuu kati yao ni Duryodhana, na wa pili ni Dushasana. Ndugu wengine wa Kikaurava walikuwa ni Vikarna na Sukarna. Uadui kati yao na mandugu wa Kipandava, kuazia ujana wao hadi wakati wapokuwa wanapokomaa unasababisha vita vya Kurukshetra.

Nyumba ya Lac)[hariri | hariri chanzo]

Baada ya vifo vya mama yao (Madri) na baba yao (Pandu); Mandugu wa Kipandava na mama yao Kunti wanarudi katika ikulu ya Hastinaour. Yushisthira anafanywa kuwa mfalme wa milki na Dhritarashtra, chini ya shinikizo kali kutoka milki yake. Dhritarashtra alitaka mwanawe Duryodhana kuwa mfalme to na anafanya tamaa yake imzuie kuhifadhi haki.

Shakuni, Duryodhana na Dusasana wanapanga kuwaangamiza mandugu wa Kipandava. Shakuni anamuita mchora ramani Purvancahan na anamfanya ajenge ikulu kwa kutumia vitu vyenye kushika moto kama vile mafuta ya maziwa na Lac. Baada ya hapo anapanga mandugu wa Kipandava na Mama Malkia Kunti kuishi hapo, akiwa na nia ya kuichoma ikulu ile. Hata hivyo, mandugu wa Kipandava wanaonywa na mjomba wao mwenye busara, Vidura, ambaye anawatumia mchimba migodi kuwachimbia shimo. Wanaweza kutorokea mahali salama na wanakimbia mafichoni. Wakati uo huo, wandugu wa Kipandava ma Kunti wanadhaniwa eti wamefariki.[23]

Ndoa na Draupadi[hariri | hariri chanzo]

Arjuna akichoma jicho la samaki

Walipokuwa mafichoni, mandugu wa familia ya Kipandava wanafahamishwa kuhusu swayamvara inayotendeka kwa kumposa binti wa mfalme wa Pāñcāla, Draupadī. Familia ya Kipandavas inaingia shindano ikijifanya kuwa Mabrahamini. Lengo ni kuunda upinde wenye nguvu na kudunga sehemu juu ya dari, ambayo ni jicho la samaki bandia, huku mlengaji akitazama umbo lake katika mafuta chini yake. Wana wengi wa wafalme wanashindwa, hata kuinua upinde. Hata hivyo Arjuna anafaulu. Mandugu wa Kipandava wanarudi nyumbani ma kumwanbia mama yao kuwa Arjuna ameibuka mshindi na wanamwambia aanaglie kile walichorudisha. Bila kuangalia, Kunti anawauliza kutumia pamjoa chochote ambacho Arjuna ameshinda. Hivyo Draupadi anakuwa bibi ndugu wote watano.

Indraprastha[hariri | hariri chanzo]

Baada ya harusi, mandugu wa Kipandava wanaalikwa kurudi Hastinapura. Wazew wa familia ya Kuru na jamaa wanajadili na wanaamua kupasua milki, huku mandugu wa Kipandava wakipata maeneo mapya. Yudhishtira ana mji mkuu unaojengwa kwa eneo hili katika Indraprastha ambayo kwa wakati wa sasa ni Delhi. Pande za Kipandava na Kaurava hazifurahii mpangilio huu.

Muda mfupi baada ya hili, Arjuna anatoroka na dada ya Krishna, Subhadra na kuolewa naye. Yudhishtira anataka kuongeza nguvu zake za kifalme; anatafuta ushauri wa Krishan. Krishna anamshauri, na baada ya maandalizi kutokana kuondoa baadhi ya upinzani, Yudhishthira anafanya sherehe ya rājasūya yagna; baada ya hapo anatambulika kama mfalme maarufu zaidi kati ya wafalme wote.

Mandugu wa Kipandava wanajengewa ikulu mpya na , Maya ambaye ni Mdanava.[24] Wanawaalika binamu zao wa Kikauraza katika mji wa Indraprastha. Duryodhana anatembea katika ikulu, na anadhani kuwa sakafu iliyong’aa sana ni maji, na anakataa kuikanyaga. Baada ya kuambiwa kuwa amekosea, anaona kidimbwi cha maji, na anadhani kuwa si maji na anatumbukia ndani. Draupadi anamchekelea na anamtania kwa kumwambia kuwa kwa kusema kuwa kukosea kwake ni kwa sababu ya babake Dhritrashtra kuwa kipofu. Duryodhana anaamua kulipiza kisasi kuabishwa kwake.

Mchezo wa daisi[hariri | hariri chanzo]

Draupadi akaibishwa. Mchoro wa Painting Raja Ravi Varma.

Shakuni, mjomba wa Duryodhana, anapanga mchezo wa daisi, akicheza na Yudhishtira kwa kutumia daisi zenye hitilafu. Yudhishtira anapoteza mali yake yote, na baada ya hapo milki yake. Anazidi na mchezo wa bahati na sibu hadi kufikia hali ambapo nduguze, yeye mwenyewe, na mwishowe wake zake wanalazimishwa kuingia utumwani. Makauravas ambao ndio washindi wanawatusi Wapandava katika hali yao hohehahe na hata wanajaribu kumvua nguo Draupadi mbele ya mahakama nzima, lakini heshima yake inaokolewa na Krishna ambaye kimiujiza anaunda nguo ndefu kuchukua nafasi ya zile zinazotolewa.

Dhritarashtra, Bhishma, na wazee wengine wanashangaa tukio hili, lakini Duryodhana anakataa kuwa hakuna nafasi ya wana wawili wa wafalme wenye mamlaka katika milki ya Hastinapura. Kinyume na mapenzi yake, Dhritarashtra anadai mchezo mwingine wa daisi. Mandugu wa Kipandava wanahitajika kuenda uhamishoni kwa miaka 12, na katika mwaka wa 13 watalazimishwa kubaki mafichoni. Ikiwa watapatikana na familia ya Kaurava, watalazimishwa kuenda uhamishoni kwa miaka mingine 12.

Uhamishoni na kurudi[hariri | hariri chanzo]

Mandugu was familia ya Pandava wanakaa uhamishoni kwa miaka kumi na mitatu; visa vingi vya kusisimua vinafanyika wakati huu. Pia wanatayarisha mifungamano wakitazamia migogoro inayoweza kutokea baadaye. Wanatumia mwaka wao wa mwisho wakiwa wamevaa nguo zisizowatambulisha katika mahakama ya Virata, na wanatambulika tu baada ya mwisho wa mwaka.

Baada ya kuisha kwa uhamishoni, wanajaribu kujadili kurudi Indraprastha. Hata hivyo, hili halifaulu, kwani Duryodhana anakataa kuwa waligunduliwa wakiwa mafichoni, na kwamba kulikuwa na ukosefu wa makubalino kuhusu kurejeshewa milki. Vita haviwezi epukika.

Vita katika Kurukshetra[hariri | hariri chanzo]

Bhishma akielekea kufa baada ua kudungwa mishale. Hapa amezingirwa na ndugu wa familia ya Pandava na Krishna – Picha kutoka Razmnama(1761 - 1763), Tafsiri ya Kiajemi ya Mahabharata, iliyoanzishwa kwa amri ya Kaizari Akbar. Ndugu wa familia ya Pandava wamevaa vitambaa na nguo za kijeshi za Kiajemi.[25]

Pande mbili zinaomba majeshi mengi kuwasaidia, na zinajipanga katika eneo la Kurukshetra tayari kufanya vita. Milki za Panchala, Dwaraka, Kasi, Kekaya, Magadha, Matsya, Chedi, Pandya, Telinga, na Yadu za Mathura na koo fulani kama vile Parama Kambojas zilichukua upande wa ndugu wa family ya Pandava. Marafiki wa familia ya Kaurava walijumuisha wafalme wa Pragjyotisha, Anga, Kekaya, Sindhudesa (ikijumuisha Sindhu, Sauviras na Sivi), Mahishmati, Avanti katika Madhyadesa, Madra, Gandhara, Bahlikas, Kambojas na wengi zaidi. Kabla ya vita kutangazwa, Balarama alikuwa amedokeza kutofurahishwa kwake na mgogoro uliokuwa ukiendelea, ana aliwachwa kuenda matembezi ya kidini, kwa hivyo hachukui sehemu yoyote katika vita. Krishna anchukua sehemu ambapo hapigani, kama muendeshaji wa gari la farasi la Arjuna.

Kabla ya vita, Arjuna, anajiona akitazama babu yake mkubwa Bhishma na mwalimu wake Drona katika upande mwingine, na ana wasiwasi kuhusu vita hivyo na anashindwa kuinua upinde wake wa Gāndeeva. Krishna anamuamusha kwa wito wake wa wajibu katika sehemu maarufu ya Bhagavad Gita ya utendi.

Ingawa mwanzoni pande zote mbili zinafuata kanuni za vita, baada ya muda mchache pande zote zinaanza kutumia mbinu za udanganyifu. Kaufikia mwisho wa vita vya siku 18, ni familia za Pandava, Satyaki, Kripa, Ashwathama, Kritavarma, Yuyutsu na Krishna zinazobaki hai.

Mwisho wa familia ya Pandava[hariri | hariri chanzo]

Baada ya "kuona" uharibifu, Gandhari ambaye alikuwa amewapoteza wanawe wote, anamlaani Krishna kuwa shahidi wa kuangamizwa sawa kwa familia yake yote, kwani alikuwa na nguvu za kimungu kwa hivyo alikuwa na huwezo wa kukomesha vita, lakini hakuvikomesha. Krishna anakubali laana hiyo ambayo inatimia miaka 36 baadaye.


Familia ya Pandava ambayo ilikuwa imetawala milki wakati uo huo, iliamua kujinyima kila kitu. Huku ikivaa ngozi na matambara wanastaafu kwa milima ya Himalaya na wanapanda kuelekea mbinguni katika hali hayo ya kimwili. Mbwa koko anawafuata katika safari yao. Mmoja mmoja ndugu hao na Draupadi wanaanguka njiani. Wakati kila mmoja anapoanguka, Yudhishitra anapea walisosalia sababu ya wao kuanguka (Draupadi alifanya mapendeleo na kumsahau Arjuna, Nakula na Sahadeva walijipenda na na kuwa na kiburi kwa sababu ya sura zao, Bhima na Arjuna walikuwa na kiburi kwa sababu ya nguvu yao na ujuzi wao wa ulengaji mishale, mtawalia). Ni tu Yudhisthira, aliyekuwa mtenda mema na aliyejaribu kuzuia vita, na mbwa wanaobaki. Mbwa Yule anajionyesha kuwa mungu Yama (anayejulikana kama Yama Dharmaraja), na anamchukua kuzimu ambapo anawaona watoto wake na mkewe. Baada ya kueleza hali ya mtihani, Yama anamrudisha Yudhishtira mbinguni na anamwelezea kuwa ilikuwa muhimu kuomwonyesha kuzimu kwa sababu (Rajyante narakam dhruvam) kila mtawala lazima atembelee kuzimu angalau mara moja. Yama anamwambia kwamba ndugu zake na mkewe watajiunga naye binguni baada ya kukaa kuzimu kwa kipindi ambacho kingelingana na makosa yao.

Mjukuu wa Arjuna Parikshit anatawala baada ya wao na anakufa baada ya kuumwa na nyoka. Mwanawe, Janamejaya ambaye anakarishwa sana na tukio hilo anaamua kufanya kafara ya nyoka (sarpasattra) ili kuangamiza nyoka wote. Ni wakati wa kafara ambapo anahadithiwa kuhusu mababu zake.

Matoleo, tafsiri na maandiko yanayotokana na utendi wa Mahabharata[hariri | hariri chanzo]

Matoleo mengi halisi ya maandiko ya Mahabharata yaliibuka na wakati, mengi yakitofautiana tu katika maelezo madogo, au yakiwa na mistari au hadithi zaidi zilizoongezwa. Haya ni kama vile matoleo kutoka bara ndogo la Uhindi, kama vile Kakawin Bharatayuddha kutoka Java. Michezo ya uigizaji vbarabarani wa Tamil, terukkuttu, yakitumia maudhui kutoka matoleo ya luigha ya Kitamili ya Mahabharata, yanaolenga Draupadi.[26]

Toleo Maalum[hariri | hariri chanzo]

Kati ya miaka ya 1919 na 1966, wasomi katika Taasisi ya Utafiti ya Mashariki ya Bhandarkar, Pune, walilinganisha nakala mbalimbali za utendi huo kuotoka Uhindi na nchi geni na kutoa Toleo Maalum la Mahabharata, katika kurasa 13,000 na vitabu 19, ikifuatiwa na Harivamsha katika vitabu vingine viwili na viatbu sita maalum. Hii ndiyo nakala inayotumika katika masomo ya sasa ya Mahabharata kama marejeo.[27] This work is sometimes called the 'Pune' or 'Poona' edition of the Mahabharata.

Tafsiri za kisasa[hariri | hariri chanzo]

Krishna anaonyeshwa katika mchoro huu katika Yakshagana kutoka nakala ya Karnataka yenye msingi wake mkubwa katika hadithi za Mahabharata

Malenga wa Kihindi, Maithili Sharan Gupt ameandika shairi la utendi kuhusu siku mbili za vita vya Jayadratha Vadha kifo cha Jayadratha). Malenga mwingine wa Kihindi Ramdhari Singh 'Dinkar' ameandika shairi la utendi kuhusu mandahari mbalimbali za Mahabharata, kama vile: Kurukshetra na Rashmirathi.

Mwandishi wa lugha ya Kikannada, S.L. Bhyrappa aliandika riwaya katika lugha ya Kikannada (ambayo sasa imetafsiriwa hadi ligha nyingi za Kihindi ikijumuisha Kiingereza) iliyoitwa Parva, alitoa ufafanuzi mpya wa hadithi ya Mahabharata. Alijaribu kuelewa mazoea ya kijamii na kimaadili katika maeneo haya na kuyalinganisha na hadithi ya Mahabharata.

Riwaya ya mwandishi wa Kimalayalam M. T. Vasudevan Nair, inayoitwa Randamoozham (tafsiri ya Kiswahili: Zamu ya Pili) inaelezea hadithi ya Mahabharata kutoka mtazamo wa Bhima. Riwaya ya Mrityunjay (Kiswahili: Ushindi Juu ya Vita) iliyoandikwa na Shivaji Sawant ni Riwaya ambapo mhusika mkuu wa Mahabharata ni Karna.

Katika sinema ya India, filamu nyingi kuhusu utendi wa Mahabharata zimetengezwa, kuanzia mwaka wa 1920.[28] Mwongozaji wenye umaarufu wa kimataifa wa filamu sambamba za Kibengali Satyajit Ray pia alinuia kuongoza mchezo kughusu utendi huo, lakini mradi huo haukuwezekana maishani mwake. [29]

Katika miaka ya mwisho ya 1980, kipindi cha runinga cha the Mahabharat , kilichoongzwa na Ravi Chopra,[30] kilionyehswa hasa katika runinga ya kimataifa ya Uhindi (Doordarshan). Katika ulimwengu wa magharibi, uwasilishaji maarufu wa utendi huo ni mchezo wa masaa tisa wa Peter Brook ulioanza katika eneo la Avignon mnamo mwaka wa 1985, na toleo lake la filamu la masaa matano lililoitwa Mahabharata (1989).[31]

Kati ya utafsiri wa kifasihi wa Mahabharata yenye umaarufu zaidi no maandiko makubwa ya Sashi Tharoor kwa jina "Riwaya Kuu ya Uhindi", riwaya ya kina ya kifasihi, kifalsafa na kisiasa ambayo inaweka pamoja matukio makuu ya wakati baada ya uhuru wa Uhindi katika karne ya 20 na kuyalinganisha na matukio makuu katika utendi wa Mahabharata.

Mahabharata pia ilitafsiriwa upya na Shyam Benegal katika filamu ya Kalyug. Kalyug nit oleo la kisasa la Mahabharata.[32]

Tafsiri za Kimagharibi za Mahabharata ni kama vile Mahabharata ya William Buck na Wana Watano Wa Mfalme Pandu ya Elizabeth Seeger.

Tafsiri za Kiingereza[hariri | hariri chanzo]

Tafsiri kamili ya kwanza ya Kiingereza ilikuwa toleo la kinathari la kipindi cha Fasihi cha Victoria lililoandikwa na Kisari Mohan Ganguli,[33] iliyochapishwa katika ya mwaka wa 1883 na mwaka wa 1896 (Wachapishaji wa Munshiram Manoharlal) na ya M. N. Dutt (Wachapishaji wa Motilal Banarsidass). Wakosoaji wengi hutazama tafsiri ya Ganguli kama aminifu kulingana na nakala asilia. Nakala kamili ya tafsiri ya Ganguli inaweza kupatikana na mtu yeyote mtandaoni.[34]

Tafsiri nyingine ya Kiingereza ya utendi wote kamili, yenye msingi wake katika Tolero Maalum, pia inaendelea kuandikwa, na itachapishwa na Kituo cha Uchapishaji cha Chuo Kiukuu cha Chicago. Ilianishwa na msomi wa mambo ya Uhindi J. A. B. van Buitenen (kitabu 1-5) na, kufuatia pengo la miaka 20 lililosababishwa na kifo cha van Buitenen, inaendelezwa na D. Gitomer wa Chuo Kikuu cha Depaul (kitabu cha 6), J. L. Fitzgerald wa Chuo Kikuu cha Brown (kitabu 11-13) na W. Doniger wa Chuo Kikuu cha Chicago (kitabu 14-18). Tafsiri ya kishairi ya utendi wote hadi lugha ya Kiingereza, uliofanywa na malenga P. Lal umekamilika, na mnamo mwaka wa 2005 tafsiri hiyo ilianza kuchapishwa na Semina ya Waandishi, Calcutta. Tafsiri ya P. Lal ni hadithi ya aya mopja hadi nyingione ambapo mishororo ya mwisho haifanani, na ndiyo toleo la kipekee katika lugha yoyote kujumuisha slokas zote katika aina zote za utendi huo (sit u zile Toleo Maalum). Inadhaniwa kuwa kukamilika kwa mradi huo wa uchapishaji utafanyika mwaka wa 2010. Vitabu kumi na visita kati ya vitabu jumla kumi na vinane vinaweza kupatikana kwa sasa:

Mradi wa kutafsiri utendi wote hadi nadhari ya Kiingereza, unaotafsiriwa na watu mbalimbali, ulianza kutokea mnamo mwaka wa 2005 katika Maktaba ya Kisanskriti ya Clay, mradi ulicchapishwa na Kituo cha Uchapishaji cha Chuo Kikuu cha New York. Tafsiri hiyo haina msingi wake katika Toleo Maalum bali msingi wake ni katika toleo linalojulikana na mtoaji maoni aliyeitwa Nīlakaṇṭha. Kwa sasa vitabu 15 vya mradi huo vinaweza kupatikana, huku lengo kuu likiwa vitabu 32.

Matoleo yaliyofupishwa[hariri | hariri chanzo]

Matoleo mengi yaliyofupishwa na yenye kueleza hadithi hiyo kupitia riwaya yamechapishwa kwa lugha ya Kiingereza, ikiwemo maandiko ya William Buck, R.K. Narayan, C. Rajagopalachari, Krishna Dharma, Romesh C. Dutt, na Bharadvaja Sarma.

Toleo la lugha ya Kikawi linapatikana katika kisiwa cha Indonesia cha Bali na lilitafsiriwa na I. Gusti Putu Phalgunadi. Kati ya parva kumi na nane, nane pekee za lugha ya Kikawi zinazoweza kupatikana wa leo.

Maelezo

  • a: Santanu alikuwa mfalme wa nasaba au milki ya Kuru, na alitenganishwa na babu yake aliyeitwa Kuru kwa vizazi vichache. Ndoa yake na Ganda ilitangulia ndoa yake na Satyavati.
  • b: Pandu na Dhritarashtra walikuwa wanawe Vyasa baada ya kifo cha Vichitravirya. Dhritarashtra, Pandu na Vidura walikuwa wanawe Vyasa kupitia wake zake Ambika na Ambalika na kijakazi mtawalia.
  • c: Karna alizaliwa na Kunti kupityia kuita Surya, kabla ya ndoa kati yake na Pandus.
  • d: Wana wenye jina la Pandava walikuwa wazaliwa wa Pandu lakini walizaliwa baada ya Kunti kuwaomba miungu wengi. Wote walimwoa Draupadi (hajaonyeshwa katika mpangilio wa familia). Hasa:
    • Yama au Dharma (Dharmadeva), kwa Yudhishtira
    • Vayu, kwa Bhima
    • Indra kwa Arjuna
    • Mapacha, Nakula na Sahadeva walizaliwa kwake Madri kupitia maombi yake kwa Maashavini
  • e: Duryodhana na nduguze walizaliwa kwa wakati mmoja, na waliishi kizazi kimoja za binamu zao wa family ya Pandava.

Utaratibu wa kuzaliwa kwa ndugu hao unaonyeshwa ipasavyo katika mpangilio wa familia (kutoka upande wa kushoto kuelekea kulia), isipokuwa Vyasa na Bhishma ambaye mpangilio wake wa kuzaliwa haujaelezewa, na Vichitravirya ambaye alizaliwa baada ya wao. Ukweli kwamba Ambika na Ambalika ni dada haijanyeshwa katika mpangilio wa familia. Kuzaliwa kwa Duryodhana kulifanyika baada ya kuzaliwa kwa Karna, Yudhishtira na Bhima, lakini kabla ya kuzaliwa kwa ndugu wengine wa familia ya Pandava.

Baadhi ya ndugu wa wahusika wachache walioonyeshwa hapa wameachwa nje ili kurahisisha mpangilio na kuufanya ueleweke vyema; hawa nio kama vile Chitrangada, kak

  1. bhārata inamaanisha wazao wa kaizari Bharata, mfalme maarufu aliyenazisha milki ya Bhāratavarsha.
  2. 2.0 2.1 Brockington (1998, p. 26)
  3. Van Buitenen; The Mahabharata - 1; The Book of the Beginning. Introduction (Authorship and Date)
  4. Spodek, Howard. Richard Mason. The World's History. Pearson Education: 2006, New Jersey. 224, 0-13-177318-6
  5. Amartya Sen, The Argumentative Indian. Writings on Indian Culture, History and Identity, London: Penguin Books, 2005.
  6. Sattar 1996, pp. lvi-lvii
  7. SP Gupta and KS Ramachandran (1976), p.3-4
  8. Cited approvingly in Max Duncker, The History of Antiquity (trans. Evelyn Abbott, London 1880), vol. 4, p. 81.
  9. For example, John Campbell Oman, The Great Indian Epics (London 1895), p. 215.
  10. 18 books, 18 chapters of the Bhagavadgita and the Narayaniya each, corresponding to the 18 days of the battle and the 18 armies (Mbh. 5.152.23)
  11. The Ashvamedhika-parva is also preserved in a separate version, the Jaimini-Bharata (Jaiminiya-ashvamedha) where the frame dialogue is replaced, the narration being attributed to Jaimini, another disciple of Vyasa. This version contains far more devotional material (related to Krishna) than the standard epic and probably dates to the 12th century. It has some regional versions, the most popular being the Kannada one by Devapurada Annama Lakshmisha (16th century).The Mahabharata[onesha uthibitisho]
  12. In discussing the dating question, historian A. L. Basham says: "According to the most popular later tradition the Mahabharata War took place in 3102 BCE, which in the light of all evidence, is quite impossible. More reasonable is another tradition, placing it in the 15th century BCE, but this is also several centuries too early in the light of our archaeological knowledge. Probably the war took place around the beginning of the 9th century BCE; such a date seems to fit well with the scanty archaeological remains of the period, and there is some evidence in the Brahmana literature itself to show that it cannot have been much earlier." Basham, p. 40, citing HC Raychaudhuri, Political History of Ancient India, pp.27ff.
  13. M Witzel, Early Sanskritization: Origin and Development of the Kuru state, EJVS vol.1 no.4 (1995); also in B. Kölver (ed.), Recht, Staat und Verwaltung im klassischen Indien. The state, the Law, and Administration in Classical India, München, R. Oldenbourg, 1997, p.27-52
  14. A.D. Pusalker, History and Culture of the Indian People, Vol I, Chapter XIV, p.273
  15. FE Pargiter, Ancient Indian Historical Tradition, p.180. He shows estimates of the average as 47, 50, 31 and 35 for various versions of the lists.
  16. Pargiter, op.cit. p.180-182
  17. B. B. Lal, Mahabharata and Archaeology in Gupta and Ramachandran (1976), p.57-58
  18. Gupta and Ramachandran (1976), p.246, who summarize as follows: "Astronomical calculations favor 15th century BCE as the date of the war while the Puranic data place it in the 10th/9th century BCE. Archaeological evidence points towards the latter." (p.254)
  19. Gupta and Ramachandran (1976), p.55; AD Pusalker, HCIP, Vol I, p.272
  20. AD Pusalker, op.cit. p.272
  21. P.V.Vartak, Swayambhu (in Marathi), Ved Vidnyana Mandal, Pune
  22. Mallory (2005:139).
  23. Book 1: Adi Parva: Jatugriha Parva
  24. Book 2: Sabha Parva: Sabhakriya Parva
  25. Plant Cultures - picture details. Jalada kutoka ya awali juu ya 2007-11-13. Iliwekwa mnamo 2010-01-25.
  26. Srinivas, Smriti (2004) [2001]. Landscapes of Urban Memory. Orient Longman. p. 23. ISBN 8125022546. OCLC 46353272. 
  27. Bhandarkar Institute, Pune Archived 19 Oktoba 2018 at the Wayback Machine.—Virtual Pune
  28. Mahabharat katika Internet Movie Database (1920 film)
  29. C. J. Wallia (1996). IndiaStar book review: Satyajit Ray by Surabhi Banerjee. Jalada kutoka ya awali juu ya 2009-05-03. Iliwekwa mnamo 2009-05-31.
  30. Mahabharat katika Internet Movie Database (1988-1990 TV series)
  31. The Mahabharata katika Internet Movie Database (1989 mini-series)
  32. What makes Shyam special.... Jalada kutoka ya awali juu ya 2011-01-12. Iliwekwa mnamo 2010-01-25.
  33. Several editions of the Kisari Mohan Ganguli translation of the Mahabharata incorrectly cite Pratap Chandra Roy as translator and this error has been perpetuated into secondary citations. See the publishers preface to the current Munshiram Manoharlal edition for an explanation.
  34. The Mahabharata of Krishna-Dwaipayana Vyasa translated by Kisari Mohan Ganguli at the Internet Sacred Text Archive