Kidaku
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
| Kidaku | ||||||||||||||||||
|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
| Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||||||||
|
Vidaku ni ndege wadogo wa jenasi Dioptrornis na Melaenornis katika familia Muscicapidae. Spishi nyingine inaitwa chekiro. Ndege hawa wana rangi kijivu au nyeusi. Wanatokea misitu na maeneo mengine yenye miti katika Afrika. Hula wadudu. Kwa kawaida vidaku hukaa tawi wakiangalia ujirani. Wakiona mdudu huruka ili kumkamata na kurudi tawi. Hujenga tago lao kwa umbo wa kikombe katika tundu la mti au dhidhi ya shina. Jike huyataga mayai 2-6.
Spishi [hariri]
- Dioptrornis brunneus, Kidaku wa Angola (Angola Slaty Flycatcher)
- Dioptrornis chocolatinus, Kidaku Habeshi (Abyssinian Slaty Flycatcher)
- Dioptrornis fischeri, Chekiro (White-eyed Slaty Flycatcher)
- Melaenornis annamarulae, Kidaku wa Nimba (Nimba Flycatcher)
- Melaenornis ardesiacus, Kidaku Macho-njano (Yellow-eyed Black Flycatcher)
- Melaenornis edolioides, Kidaku Kaskazi (Northern Black Flycatcher)
- Melaenornis pammelaina, Kidaku Kusi (Southern Black Flycatcher)