Cape Town Tigers

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Cape Town Tigers ni klabu ya mpira wa kikapu nchini Afrika Kusini yenye makao yake jijini Cape Town.[1] Timu hiyo inapatikana katika kitongoji cha Gugulethu.[2] Ilianzishwa mwaka 2019, makocha ni Raphael Edwards na Vincent Ntunja. Mwaka 2021, klabu ilishinda ubingwa wa kitaifa Afrika Kusini ukiwa msimu wake wa kwanza katika mashindano hayo.

Mataji[hariri | hariri chanzo]

Michuano ya kitaifa Afrika Kusini

  • Mabingwa (2): 2021, 2022

Ligi ya Mpira wa Kikapu Afrika

  • Mshindi wa Robo fainali[3] (1): 2022

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. "We Are The Tigers". www.capetowntigers.com (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2022-09-02. 
  2. "Cape Town Tigers", Wikipedia (kwa Kiingereza), 2022-08-23, iliwekwa mnamo 2022-09-02 
  3. "Cape Town Tigers at the ROAD TO BAL 2022 2021". FIBA.basketball (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2022-09-02.