Baja California (jimbo)

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Isla Partida,Baja California
Nembo ya Sonora
Mahali pa Baja California katika Mexiko

Baja California (tamka ba-kha ka-li-for-ni-a, kwa maana Kalifornia ya Chini) ni moja kati ya majimbo 31 ya Mexiko upande wa kaskazini-magharibi ya nchi. Jimbo lina wakazi wapatao 2,844,469 (2005) wanaokalia katika eneo la kilomita za mraba zipatazo 69,921.

Mji mkuu ni Mexicali na mji mkubwa ni Tijuana. Iko kwenye pwani la Pasifiki na Ghuba ya California (au Bahari ya Cortez).

Imepakana na Marekani (jimbo la Kalifornia), halafu majimbo ya Meksiko Sonora na Baja California Sur.

Gavana wa jimbo ni José Guadalupe Osuna Millán.

Lugha rasmi ni Kihispania.

Miji Mikubwa[hariri | hariri chanzo]

  1. Tijuana (1,286,187)
  2. Mexicali (1,000,010)
  3. Ensenada (460.075)
  4. Tecate (91,034)
Pori ya Kati, Baja California

Viungo vya Nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu maeneo ya Mexiko bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Baja California (jimbo) kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.