Tao (usanifu)

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Tao.
Tao la kuchongoka.

Tao ni sehemu ya jengo ambako kuna uwazi uliofunikwa juu kwa umbo la upinde.

Tao linaweza kuwa na umbo la sehemu ya duara au la kuchongoka.

Linatumika sana katika majengo ya dini, lakini asili yake ni tofauti, kwa sababu lilikuwepo tangu zamani sana, hata kabla ya ustaarabu wa Ugiriki wa Kale.