Nenda kwa yaliyomo

Tamasha la Adae

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Tamasha la Adae ni sherehe inayoadhimishwa katika Mkoa wa Ashanti. Inachukuliwa kama siku ya kupumzika, na ni desturi ya zamani sana ya kihistoria ya watu wa Ashanti.

Kutekelezwa[hariri | hariri chanzo]

Ndani ya mzunguko wa wiki sita, Adae ina siku mbili za sherehe, mara moja Jumapili (Akwasidae) na tena Jumatano (Awukudae). Mzunguko wa Adae unarudiwa mara tisa katika mwaka mmoja. Kulingana na kalenda ya Akan, Tamasha la Adae la tisa, linaloitwa Tamasha la Adae Kese (Adae kubwa), hutokea wakati wa sherehe ya Mwaka Mpya. Kwa hivyo, sherehe hii hufanyika kushukuru miungu na mababu kwa mavuno mapya.[1] Matamasha ndani ya Adae hayawezi kubadilishwa badilishwa, kwa sababu yalifungwa tangu enzi za kale.


Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. Asante, Molefi Kete; Mazama, Ama (26 Novemba 2008). Encyclopedia of African Religion. SAGE. ku. 36–. ISBN 978-1-4129-3636-1. Iliwekwa mnamo 21 Novemba 2012.{{cite book}}: CS1 maint: date auto-translated (link)