Sima Qian

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Sima Qian

Sima Qian (Kichina:司马迁) alikuwa mtaalamu wa historia wakati wa nasaba ya Han chini ya Kaisari Wu. Alizaliwa mjiniXia Yang (katika jimbo la leo la Shaanxi. Babake Sima Tan alikuwa mwanahistoria pia.

Anatazamiwa kama "baba wa historia ya China" kwa sababu aliandika historia ya kwanza ya taifa lake alipojumlisha miaka 2000 kuanzia "Kaisari wa Manjano" hadi Kaisari Wu wa nasaba ya Han. Kitabu hiki kimekuwa msingi kwa wanahistoria wote wa China waliomfuata hadi leo.

Maisha[hariri | hariri chanzo]

  • Sima Qian alipofikia umri wa miaka 10 aliweza kusoma vitabu vilivyoandikwa kwa alama za mwandiko wa Kichina.
  • Alipofikia umri wa miaka 20 alisafiri pande nyingi za China na kutembelea mahali pengi mashuhuri.
  • Mnamo mwaka 108 KK baada ya kifo cha babake alipewa cheo cha mwanahistoria rasmi wa milki ya Han.
  • mnamo mwaka 104 KK alihariri matengenezo ya kalenda ya China.
  • mwaka 99 KK Sima Qian alishtakiwa kwenye mahakama ya Kaisari kwa sababu alimtetea jenerali Li Ling aliyewahi kushindwa vitani dhidi ya makabila ya kaskazini-magharibi. Kaisari Wu alikasirika na Sima Qian alihukumiwa kufa lakini kwa nafasi ya kulipa faini kubwa. Alishindwa kulipa akakubali ahdabu badala ya hasi.
  • baada ya kupokea adhabu watu welimtegemea ya kwamba angejiua jinsi ilivyokuwa kawaida kwa watu wenye cheo walioadhibiwa hivyo. Lakini Sima Qian alichagua kuishi maisha ya towashi kwa sababu alitaka kumaliza historia yake.