Nenda kwa yaliyomo

Siku ya Kimataifa ya Kutokomeza Ukeketaji

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Siku ya Kimataifa ya Kutokomeza Ukeketaji (kwa Kiingereza: International Day of Zero Tolerance for Female Genital Mutilation) ni siku ya kimataifa ya Umoja wa Mataifa ambayo husherehekewa tarehe 8 Februari ya kila mwaka ikiwa na malengo ya kutokomeza ukeketaji.

Siku hiyo ilianza kuadhimishwa mwaka 2003.[1]

Historia

[hariri | hariri chanzo]

Moja ya imani inayounga mkono siku hii ni kwamba tamaduni hubadilika kila mara, na kutokana na hatari kubwa zinazohusiana na ukeketaji, ni muhimu sana desturi hii kukomeshwa haraka. Harakati hizi zinalenga kutetea haki za wanawake juu ya miili yao na kulinda afya yao ya mwili, ambayo inaweza kuathiriwa sana baadaye maishani. Juhudi hizi zinachangia mapambano dhidi ya ukatili kwa wanawake na wasichana kwa ujumla.

Kulingana na Every Woman, Every Child (harakati ya kimataifa), ukeketaji haufanywi Afrika na Mashariki ya Kati tu bali pia unaendelea kufanyika katika baadhi ya nchi za Asia na Amerika Kusini. Aidha, umeendelea kuripotiwa katika jamii za wahamiaji waliopo Ulaya Magharibi, Amerika Kaskazini, Australia na New Zealand. Nchini Marekani pekee, idadi ya wanawake na wasichana waliokumbwa na ukeketaji imeongezeka mara tatu ukilinganisha na ripoti ya mwaka 1990.[2]

Shirika la Afya Duniani (WHO) linakadiria kuwa kati ya wanawake milioni 120 hadi 140 wamekeketwa, na takriban wasichana milioni 3 wako hatarini kila mwaka. WHO pia imesema kuwa, licha ya ukeketaji kuendelea kwa zaidi ya miaka elfu moja, ushahidi unaonesha kuwa unaweza kukomeshwa kabisa ndani ya kizazi kimoja. Lengo kuu ni kuhamasisha dunia kuhusu madhara ya ukeketaji na kuutokomeza kabisa.[3]


  1. Charlotte Feldman-Jacobs, "Commemorating International Day of Zero Tolerance to Female Genital Mutilation" Archived 2010-02-13 at the Wayback Machine, Population Reference Bureau, February 2009.
  2. "International Day of Zero Tolerance to Female Genital Mutilation". World Health Organization (kwa Kiingereza (Uingereza)). Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo Oktoba 28, 2016. Iliwekwa mnamo 2016-02-05.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  3. "Statement on the International Day Against Female Genital Mutilation, UNFPA". Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2010-03-10. Iliwekwa mnamo 2014-02-05.