Namba za Magari

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
                                                      

Makala hii ina dalili ya kutungwa kwa kutegemea programu ya kompyuta kama vile "Google translation" au "wikimedia special:content translation" bila masahihisho ya kutosha. Watumiaji wanaombwa kuchunguza tena lugha, viungo na muundo wake. Wakiridhika na hali yake wanaweza kuondoa kigezo hiki kinachoonekana kwenye dirisha la kuhariri juu ya matini ya makala kwa kutumia alama za {{tafsiri kompyuta}} .

Namba za magari (maarufu kama pleti namba kutoka plate number) hutumika kutambulisha na kutoshautisha gari moja na nyingine. Yaani muunganiko wa namba hizi na herufi zinazoandikwa kutambulisha gari haziwezi zikafanana katika nchi moja. Na pia Kati ya nchi na nchi hutofautishwa na bendera ya nchi hio na herufi ya kwanza ya hiyo nchi. Kwan kawaida Namba ya gari hua na sehemu kuu tatu ambazo ni nchi, herufi na namba. Ambazo kwa pamoja hutambulisha gari dunia nazima na haziwezi zikafanana.[1]

Historia[hariri | hariri chanzo]

Historia ya namba za magari inafanya turudi nyuma mpaka mnamo mwaka 1808 ambapo gari la kwanza lilitengeneza na kuanzia hapo kutafta kama kunagari ilipewa namba. Kulingana na uchache wa magari wakati ule hawakuweza kuvipa namba. Historia inaonesha kua pleti namba ya kwanza kutolewaa ilikua 1893 huko Ufaranza katika jiji la Paris. Hii taarifa haikuenea sana mpaka pale Uingereza ilipotoa namba ya gari la kwanza mnamo 1903 (A 1) na kufanya watu waamini kua Uingereza ndo nchi ya kwanza kutoa namba ya gari.[2]

Kulingana na mpangilio wa namba zinazotumika sasa hivi hufanya watu wazidi kuamini kua Uingereza ndo nchi ya kwanza, lakini hii si kweli japokua Uingereza ulifanya mapinduzi ya haraka mpaka kufikia huu mpangilio wa sasa:

  • Mwaka wa 1903, Sheria ya Magari ilianzishwa kwa lengo la kusimamia magari barabarani. Katika siku za mwanzo za historia ya magari, mamlaka za mitaa zilikuwa zinahusika na usajili wa magari mapya. Sheria hiyo ilihitaji magari yote kuonyesha nambari ya usajili na lengo lake lilikuwa kufuatilia magari na kuweka kodi ya barabara.
  • Mwaka wa 1932 mfumo mpya wa nambari uliwasilishwa ambao ulihitaji nambari kufuata muundo maalum wa herufi 2 zilizofuatwa na nafasi, ikifuatiwa na hadi nambari 4.
  • Kufikia miaka ya 1960, mamlaka za mitaa zilianza kukosa mchanganyiko wa nambari uliosalia na mfumo mwingine wa nambari uliundwa mwaka wa 1963.
  • Baadaye mwaka wa 1965, Kituo cha Usajili wa Madereva na Magari (DVLC) kilianzishwa huko Swansea kuchukua jukumu la usajili wa magari. Kilipewa jina la Shirika la Usajili wa Madereva na Magari yaani "Driver and Vehicle Licensing Centre (DVLA)" mwaka wa 1990. DVLA ni tawi la utendaji la Idara ya Usafiri.

Na hii historia ndo inaperekea mfumo wa namba zinazotumika leo. Japokua inasadikika kua Uingereza ipo kwenye mchakato wa kutafuta namna nyingine kwani wanaamini ifikapo 2051 watakua wamaushiwa namba za magari.[3]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. "Tanzania Revenue Authority - Number Plates Manufactures". www.tra.go.tz. Iliwekwa mnamo 2024-04-17. 
  2. "Number Game! A Brief History of the Licence Plate". carandbike (kwa English). Iliwekwa mnamo 2024-04-18. 
  3. Jesse Robin (2023-06-28). "A Brief History of Cars and Number Plates". SurePlates (kwa en-GB). Iliwekwa mnamo 2024-04-18.