Mtumiaji:Jackson Mujungu/Lucie Ahl

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Lucie Ahl[hariri | hariri chanzo]

Lucie Ahl (amezaliwa mnamo tarehe 23 Julai mwaka 1974 huko Exeter, Devon) ni kocha wa tenisi na mchezaji wa zamani nguli wa tenisi. Kwa muda mfupi alikuwa namba moja Uingereza, akishikilia wadhifa huo katika wiki 9 zisizo za mfululizo kati ya tarehe 30 Julai mwaka 2001 na Mei 5, mwaka 2002. Alifikia viwango  vya juu zaidi na kushika  nambari 161 duniani tarehe 1 Aprili mwaka 2002.

Katika taaluma yake, Ahl alishinda jumla ya mataji 15 ya ITF Women’s Circuit na pia alishiriki kwenye Ziara ya WTA. Alifanikiwa kuwashinda wachezaji wenzake wa  ITF & WTA Tour Sandra Cacic na Rene Simpson.