Mchembe

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Michembe)

Mchembe ni chakula kinachotokana na viazi vitamu vilivyokaushwa. Hukatwa vikiwa vibichi vipande vidogovidogo, halafu huanikwa kwenye jua. Huweza kukaa muda mrefu pasipo kuharibika.

Tofauti na mbute hutengenezwa na zao la muhogo uliomenywa na huvundikwa na baadae kupikwa.

Pia kuna matobolwa ambavyo ni vipande vidogovidogo vilivyotokana na viazi vilivyopikwa kisha kukatwakatwa.

Makala hii kuhusu mambo ya utamaduni bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mchembe kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.