Nenda kwa yaliyomo

Mercy Myra

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Mercy Myra ni mwanamuziki wa R & B, kutoka nchini Kenya.

Mwaka wa 1996 alijiunga na kundi la Calabash Band lakini aliliacha kundi hilo mwaka uliyofuata na kujiunga na kundi la R & B la Destinee, na mwaka wa 1997 alijiunga na bendi iitwayo Black Ice. Kisha akaamua kuacha mambo ya vikundi na bendi ya muziki na kuanza kuimba pekee yake kama mwanamuziki wa kibinafsi. Alitoa wimbo wake wa kwanza uliokuwa unaitwa "Sitaki" (akishirikisha kundi la K-South) katika mwisho wa mwaka wa 1998, iliyotayarishwa na Samawati Studios.

Amewatumbuiza wapenzi wa muziki katika matamasha mbalimbali nje ya nchi, yakiwemo mwaka 2004 tamasha la filamu ya kimataifa ya Zanzibar mwaka wa 2004 na tamasha la Mundial mjini Tilburg, Uholanzi miaka wa 2002 na 2003.

Mercy Myra alikuwa sehemu ya kundi la The Divas of the Nile ambayo ilishirikisha wanamuziki wanne wa kike wa Kenya. Wanamuziki wake wengine walikuwa Suzzana Owiyo, Achieng Abura na Princess Jully. Kundi hili liliwatumbuiza wageni waliohudhuria tamasha la Mundial mwaka wa 2007.

Alihamia nchi ya Marekani mwaka wa 2005, na hivyo basi akasahaulika na vyombo vya habari na wapenzi wa muziki. Mwaka 2009 yeye alishinda Best Female Artiste jamii katika Msanii Awards, kuheshimu US-makao wanamuziki wa Kenya.

Albamu:

  • Taba Samu (2001)
  • Nyisri Malong'o (2003)
  • Tuzo za Kisima za mwaka wa 2003 - Msanii bora wa R & B wa mwaka.
  • Tuzo za Kisima za mwaka wa 2003 - Msanii bora wa kike.

Kuteuliwa:

  • Tuzo za Kisima za mwaka wa 2003 - Msanii bora wa kike.

Viungo vya nje

[hariri | hariri chanzo]