Jorge Luis Borges

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Jorge Luis Borges
Jorge Luis Borges
Jorge Luis Borges
Alizaliwa 24 Agosti 1899
Alikufa 14 Juni 1986
Nchi Argentina
Kazi yake mwandishi wa fasihi kutoka nchi ya Argentina

Jorge Luis Borges (24 Agosti 1899 - 14 Juni 1986) alikuwa mwandishi wa fasihi kutoka nchi ya Argentina. Wataalamu wengi wa fasihi wanaamini kuwa Borges alikuwa mmojawapo wa waandishi mashuhuri sana katika karne iliyopita.

Mwaka 1914, familia yake ilihamia nchini Switzerland ambapo aliweza kujiunga na shule na baadaye kusafiri nchini Hispania. Alivyorudi nchini Argentina mnamo mwaka 1921, Borges alianza kuchapisha vitabu vya fasihi na insha kadhaa. Pia alishawahi kufanya kazi kama mkutubi na mhadhiri wa umma. Mwaka 1955, alichaguliwa kuwa mkurugenzi wa Maktaba ya Taifa (Biblioteca Nacional) na mwalimu wa Fasihi katika Chuo Kikuu cha Buenos Aires.

Mwaka 1961 alikuja katika uzingativu wa watu kimataifa pale alipopata Tuzo ya Waandishi wa Kimataifa kwa ajili ya Prix Formentor. Mwaka 1971 alijishindia Tuzo ya Jerusalem. Kazi zake zilitafsiriwa na kuchapishwa zaidi nchini Marekani na huko barani Ulaya. Borges yeye mwenyewe alikuwa anajua lugha kadhaa kwa ufasaha kabisa. Alifariki mjini Geneva, Switzerland, mnamo mwaka 1986.

Borges hasa alijulikana kwa kutunga hadithi fupi za kubuniwa zilizoangazia masuala magumu kama vile "Wakati, Uwanda na Vioo" (kwa Kiingereza, Time, space and mirrors).

Mifano ya hadithi fupi alizoziandika ni kama "Shamba Panda" ambayo kwa Kiingereza ni The Garden of forking paths, na "Maktaba ya Babeli", au kwa Kiingereza, The Library of Babel.

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mwandishi fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Jorge Luis Borges kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.