Infraredi
Infraredi (pia: inforedi, miali chini ya upinde) ni aina ya nuru isiyoonekana kwa macho ya kibinadamu lakini kuna wanyama wanaoweza kuiona. Inasikika kama joto. Kifizikia ni aina ya mnururisho wa sumakuumeme (ing. electromagnetic waves) mwenye mawimbi marefu kuliko nuru ambayo inaonekana kwa binadamu na mawimbi ambayo ni mafupi zaidi kuliko mikrowevu.
Historia ya utambuzi
Miali ya infraredi ilitambuliwa mara ya kwanza na mwanaastronomia Friedrich Wilhelm Herschel aliyefanya utafiti wa nuru ya Jua. Alipitisha nuru ya Jua kwenye prisma akapata spektra ya nuru hii. Alianza kupima halijoto za rangi mbalimbali za spektra. Hapo aliona akiweka themomita nje ya sehemu nyekundu ya spektra joto lilipanda tena. [1] [2] Hivyo alitambua ya kwamba spektra ya nuru inaendelea nje ya sehemu aliyoweza kuona kwa macho yake.
Wanyama wenye uwezo wa "kuona" infraredi
Kuna wanyama mbalimbali wenye uwezo wa "kuona" infraredi. Nyoka mbalimbali huwa na milango ya fahamu ya pekee inayowawezesha kutambua tofauti za halijoto katika mazingira yao hivyo kutambua windo la karibu hata gizani.
Kuna pia popo ya Desmodus rotundus hujo Amerika Kusini mwenye mlango wa fahamu wa kutambua windo lake.
Kua pia aina za wadudu wenye milango fahamu za pekee kwa kutofautisha joto.
Kwa wanyama wachache imeonekana ya kwamba wanatumia macho kwa kazi hiyo, kwa mfano samaki za Afrika ya Magharibi aina ya Pelvicachromis taeniatus.
Binadamu hutambua joto kupitia neva za pekee kwenye ngozi laini haziwezi kutofautisha sehemu ja joto tofautitofauti isipokuwa kwa karibu sana.
Mitambo inayotumia infraredi
Kuna njia ya kufanya picha za infraredi kwa kutumia kamera, filamu na mitambo ya pekee.
Kamera zinaweza kutumia filta kali zinazozuia nuru ya kawaida isiingie ndani, na pamoja na filamu za pekee inaweza kushika picha kama ile ya wasichana hpo juu kwenye ukurasa huu.
Ilhali picha hizi zinaweza kupigwa hata penye giza kabisa kunamatumizi mengi katika teknolojia ya usalama na upelelezi kwa picha za aina hii.
Siku hizi kuna kamera kwa ajili ya kompyuta zinazopima mawimbi ya infraredi. Teknolojia hii ina matumizi makubwa kwa ajili matumizi ya jeshi na polisi.
Askari wanatumia mitambo midogo inayowawezesha kuona kwenye usiku. Mtu huwa na halijoto tofauti na mazingira yake hivyo anaonekana pia katika giza. Injini za motokaa kama ni joto inaonekana sana gizani kwa infraredi hata kama injini ilizimishwa.
Makombora ya kisasa ya kupiga ndege hutumia "jicho la infraredi" kwa kulenga kwa injini ya ndege nyingine. Hapo ndege za kijeshi wanatumia mabomu madogo yanayolipuka nje ya ndege yenyewe kwa kusudi la kuipa kombora mahali pa joto kali zaidi itakapolenga badala ya ndege yenyewe.
Marejeo
- ↑ Herschel discovers Infrared light. Jalada kutoka ya awali juu ya 2012-02-25. Iliwekwa mnamo 2015-04-05.
- ↑ William Herschel and the discovery of infrared light. Jalada kutoka ya awali juu ya 2015-03-27. Iliwekwa mnamo 2015-04-05.
Tovuti za Nje
- Perception of infrared radiation - University of Arizona Archived 9 Machi 2016 at the Wayback Machine.
- How animals see the world Archived 15 Machi 2015 at the Wayback Machine.
Angalia mengine kuhusu Infraredi kwenye miradi mingine ya Wikimedia: | |
![]() |
Fafanuzi za Kiingereza kutoka Wiktionary |
![]() |
picha na media kutoka Commons |
![]() |
misaada ya kujisomea kwa Kiingereza kutoka Wikiversity |
![]() |
matini za ushuhuda na vyanzo kutoka Wikisource |
![]() |
vitabu kutoka Wikibooks |
- Infrared: A Historical Perspective (Omega Engineering)
- Infrared Data Association, a standards organization for infrared data interconnection
- SIRC Protocol
- How to build an USB infrared receiver to control PC's remotely
- Infrared Waves Archived 14 Januari 2006 at the Wayback Machine.: detailed explanation of infrared light. (NASA)
- Herschel's original paper from 1800 announcing the discovery of infrared light
- The thermographic's library, collection of thermogram