Goguryeo

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Goguryeo
Ufalme wa Korea
Goguryeo
  1. Dongmyeong 37-19 KK
  2. Yuri 19 KK-18 BK
  3. Daemusin 18-44
  4. Minjung 44-48
  5. Mobon 48-53
  6. Taejo 53-146
  7. Chadae 146-165
  8. Sindae 165-179
  9. Gogukcheon 179-197
  10. Sansang 197-227
  11. Dongcheon 227-248
  12. Jungcheon 248-270
  13. Seocheon 270-292
  14. Bongsang 292-300
  15. Micheon 300-331
  16. Gogug-won 331-371
  17. Sosurim 371-384
  18. Gogug-yang 384-391
  19. Gwanggaeto the Great 391-413
  20. Jangsu 413-490
  21. Munja-myeong 491-519
  22. Anjang 519-531
  23. An-won 531-545
  24. Yang-won 545-559
  25. Pyeong-won 559-590
  26. Yeong-yang 590-618
  27. Yeong-nyu 618-642
  28. Bojang 642-668

Goguryeo ni nasaba ya kwanza ya Korea ya kale ambayo ilianzishwa na Jumong (주몽朱蒙) mnamo 37 KK. Ilianzishwa karibu na eneo la mto Dongga (동가강佟佳江) ambapo ni tawi mkondo wa Abrok (압록강). Korea inajivunia sana Goguryeo kama mwanzo wa taifa la Korea.[1]

Kuundwa na Uenezi wa Goguryeo[hariri | hariri chanzo]

Hadithi ya kuzaliwa kwa taifa inaeleza kwamba Jumong alizaliwa nje ya yai na kulelewa na mfalme Kuemywa (금와왕) wa Buyeo Mashariki (동부여). Jina la Jumong, linamaana ya mtu mwenye uwezo mkubwa wa kupiga mishale. Kama jinsi jina linavyoonyesha, alikuwa mkali katika mishale na kwa sababu ya uwezo wake, mtoto wa mfalme Daeso (대소왕자) alimwonea gele sana Jumong. Kwa hiyo, Jumong akajionea tabu na kuamua kutoroka Buyeo Mashariki akiwa na marafiki zake watatu. Akaenda zake huko Jolbon Buyeo (졸본부여) na kumwoa Bi. Sosuno (소서노) ambaye alikuwa binti wa mfalme katika taifa hilo. Jumong akarithi ufalme na kubadili jina la nchi na kuliita Goguryeo baada ya jina la mzee wake.

Tangu mfalme wa kwanza, mfalme Dongmyungsung (동명성왕), Goguryeo ilivamiwa kivita mara kadhaa na nchi kama Han (한나라), kabila la Sunbi (선비족). Lakini, kwa utawala wa mfame wa 11, Gogurye ilifanikiwa kuipola mamlaka nchi kama Yodong (요동). Hadi kipindi cha mfalme wa 24, ilikuwa na waziri wake mkuu, ikapanua safu ya nchi yake na kutimua mashambulizi yote kutoka nje. Mfalme maarufu ni Guangaeto (광개토대왕).

Kuangamizwa kwa Goguryeo[hariri | hariri chanzo]

Hata hivyo, wakati ipo chini ya utawala wa mfalme wa 27, Youngryou (영류왕), Goguryeo ilionekana kama imejisalimisha kwa Dang (당나라) kwa hiyo mfalme akauawa na Yoengaesomoon (연개소문) na mfalme Bojang (보장왕) akarithi cheo. Baada ya kufa kwa Yoengaesomoon, watu wakawa hawashirikiani na taifa lao vizuri na kupelekea taifa kuwa dhaifu, lilikuja kuangamizwa na nguvu ya muungano baina ya Shinla (신라) na Dang.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. Goguryeo. Proud History of Korea. www.mygoguryeo.net. Jalada kutoka ya awali juu ya 2009-06-26. Iliwekwa mnamo 2009-06-12.

Viungo vya Nje[hariri | hariri chanzo]