Akina Mama wa Afrika

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Akina Mama wa Afrika (AMwA) ilianzishwa mwaka 1985 nchini Uingereza kama shirika dogo la jumuiya ya wanawake wa Kiafrika. Kwa sasa ni shirika lisilo la kiserikali la kimataifa na la Afrika nzima linalotetea haki za wanawake lenye makao yake makuu mjini Kampala, Uganda.[1][2].

Huduma[hariri | hariri chanzo]

AMwA inaelezwa kama "kituo cha mafunzo" na "injini ya utetezi" kwa vuguvugu la wanawake barani Afrika. Inalenga kuimarisha uwezo wa wanawake kushiriki katika uongozi kupitia programu za elimu, rasilimali na utafiti, kutoa majukwaa ya utetezi na harakati za kushawishi siasa na sheria.

Mnamo mwaka wa 2014, AMwA, pamoja na mashirika mengine ya wanawake, ilifanya mkutano wa kikanda huko Kampala ikiwa na mada "Kuimarisha Sauti za Wanawake wa Kiafrika katika Mchakato wa Baada ya 2015". Mkutano huo ulinuia kutumika kama ukumbusho wa masuala ya kawaida ambayo wanawake wa Kiafrika wanaendelea kukabiliana nayo, ikiwa ni pamoja na unyanyasaji wa kijinsia.

Baadhi ya mashirika ambayo yamesaidia Akina Mama wa Afrika ni pamoja na Mfuko wa Maendeleo ya Wanawake Afrika na Sigrid Rausing Trust.

Taasisi ya Uongozi wa Wanawake Afrika (AWLI)[hariri | hariri chanzo]

AWLI, iliyoanzishwa kwa mara ya kwanza mwaka wa 1996, inazingatia mada kama vile unyanyasaji wa kijinsia, Afya na Haki za Kijinsia na Uzazi, juhudi za kupambana na umaskini na kujenga amani. Imeundwa na viongozi wanawake kutoka Afrika, kwa ajili ya kutoa usaidizi wa kitaalamu, fursa za mitandao na warsha kwa wanaharakati wanawake wenye umri wa miaka 18-45 kutoka kote barani.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. Ray, Audacia. "Not Just Violent Clients Hurt Sex Workers", 15 Desemba 2010. Retrieved on 25 Novemba 2014. 
  2. "Our Interview of the Month with Leah Chatta-Chipepa". www.makeeverywomancount.org. Make Every Woman Count. 5 Novemba 2012. Iliwekwa mnamo 28 Julai 2014.