Utaifa

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Utaifa ni itikadi ya mtu kupenda taifa lake kupita kiasi, hata kudharau watu wa mataifa mengine. Hivyo ni tofauti na uzalendo unaomfanya mtu apende nchi yake kwa kutambua mema mengi aliyopata kutoka kwake. [1]

Mara nyingi unajitokeza pia kama dharau kwa wananchi walio tofauti na kawaida kwa utamaduni, lugha n.k.

Katika ngazi ya chini, tunakuta ukabila.

Bendera ya taifa, wimbo wa taifa na alama nyingine za utambulisho ni muhimu katika kuchochea uzalendo, lakini mara nyingine zinachangia utaifa.[2][3][4][5]

Elimunafsia inaeleza kwamba pendo kwa taifa linatokana na haja ya kuhusiana na wengine, lakini ni tofauti na mapendo mengine, k.mf. pendo kwa dini au kwa mchumba.

Kwa vyovyote ukomavu unadai mtu ajali wenzake asiwaone kama maadui kwa sababu tu ni tofauti naye.

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. Rothi, Despina et al. (2005). National attachment and patriotism in a European nation: A British study. Political Psychology, 26, 135 - 155.
  2. Billig 1995, p. 72.
  3. Gellner, Ernest (2005). Nations and Nationalism (2nd ed.). Blackwell. ISBN 1405134429. 
  4. Canovan, Margaret (1996). Nationhood and Political Theory. Cheltenham, UK: Edward Elgar. ISBN 1-85278-852-6. 
  5. Miller 1995, p. 160

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Marejeo mengine[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]