Ulafi
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Sehemu inayohusu ulafi katika mchoro wa Hieronymus Bosch kuhusu vilema vikuu saba na vikomo vinne vya binadamu.
| Vilema vikuu |
|---|
Ulafi (pamoja na ulevi) ni hamu isiyoratibiwa ya kula (na kunywa).
Tabia hiyo ina madhara makubwa kwa afya ya binadamu.
Inakadiriwa kuwa siku hizi mtu 1 kati ya 3 anakula kuliko mwili wake unavyohitaji, na hivyo anasababisha maradhi mbalimbali yampate.
Upande wa maadili unahesabiwa kuwa kimojawapo kati ya vilema vikuu, ambavyo ni mizizi ya dhambi nyingine.
| Makala bado ni mbegu. Unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuongezea habari. |