Unene wa kupindukia

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Obesity
Mwainisho na taarifa za nje
SpecialtyEndocrinology Edit this on Wikidata
ICD-10E66.
ICD-9E
OMIM601665
DiseasesDB9099
MedlinePlus003101
eMedicinemed/1653
MeSHC23.888.144.699.500

Unene wa kupindukia (kwa Kiingereza "obesity" kutokana na neno la Kilatini obesitas, linalomaanisha "gumu, nono au nene” [1]; jina la kisayansi kwa Kilatini ni "adipositas") ni hali mbaya ambapo mafuta ya ziada ya mwili hulimbikizana hadi kiwango kinachoweza kuathiri vikubwa afya, ikipelekea ongezeko la maradhi na kupungua kwa matarajio ya kuishi. [2][3]

Kipimo cha mwili kuwa mnene na mzito mno ni uwiano kati ya urefu wa mtu na uzito wake. Watu hutajika kuwa na unene wa kupindukia wakati nambapeo ya mata ya mwili (NMM), kipimo kinachopatikana kwa kugawanya uzito wa mtu kwa kilogramu kwa mraba wa urefu wake katika mita, kimezidi 30 kg/m2.[4]

Kuwa mneme mno kunaleta hatari ningi kwa afya na kusababisha au kuongeza uwezekano wa magonjwa kama vile:

Watu wakinenepa mno hufa mapema na kuwa na magonjwa mengi kuliko watu wembamba wanaokula kiasi tu, jinsi wanavyohitaji chakula. Tatizo la unene duniani hukumba wanaume zaidi ya wanawake.

Unene wa kupindukia mara nyingi husababishwa na ujumuisho wa kula chakula kilicho na nguvu nyingi, ukosefu wa mazoezi ya mwili, na urithi wa jeni maalumu, ingawa visa vichache vina msingi wa jeni, matatizo ya kiendrosini, matibabu au maradhi ya akili.

Ushahidi wa kuthibitisha dhana kuwa baadhi ya watu hunenepa ingawa hula kiasi kidogo hautoshi; kwa wastani, watu wanene hutumia nguvu nyingi kuliko watu wenye mwili mdogo kwa sababu ya nguvu zinazohitajika kuimarisha mata kubwa ya mwili.[6][7]

Chakula bora na mazoezi ya mwili ndiyo njia kuu za kutibu unene wa kupindukia. Ubora wa chakula unaweza kuimarishwa kwa kutumia vyakula vilivyo na nguvu nyingi, kama vile vyakula vilivyo na kiwango cha juu cha mafuta na sukari, na kwa kutumia unyuzi wa chakula kwa wingi zaidi.

Dawa za kukabiliana na unene zinaweza kutumiwa kupunguza hamu ya chakula au kuzuia ufyonzaji wa mafuta, huku mtu akila chakula kinachofaa. Iwapo chakula bora, mazoezi na matibabu hayatoshi, mpira wa utumboni unaweza kusaidia kupunguza uzito wa mwili, au upasuaji unaweza kufanywa ili kupunguza ukubwa na/au urefu wa matumbo. Upasuaji huo hupelekea mtu kushiba upesi na kupunguza uwezo wa kufyonza virutubishi vilivyomo katika chakula.[8][9]

Unene wa kupindukia ni kisababishi kinachozuilika cha kifo kilicho kikuu ulimwenguni kote, huku kiwango chake cha ueneaji kikiongezeka kwa watu wazima na watoto. Viongozi huamini kuwa hili ni mojawapo ya matatizo makuu zaidi ya afya ya umma katika karne ya 21.[10]

Unene wa kupindukia hufedheheshwa katika sehemu nyingi za ulimwengu wa kisasa (hasa katika Ustaarabu wa Magharibi[11]), ingawa hali hii ilitazamwa na watu wengi kama ishara ya utajiri na afya bora katika nyakati za awali za historia, na pia huonekana hivyo katika baadhi ya sehemu za dunia.[3][12]

Uainishaji[hariri | hariri chanzo]

Unene wa kupindukia ni hali ya kimatibabu ambapo mafuta ya mwili ya ziada hulimbikizana hadi kiwango kinachoathiri afya kwa vikubwa.[2] Hali hii hufasiliwa kwa Kielezo cha Uzani wa Mwili na kukadiriwa zaidi kwa kupima ugawaji wa mafuta kupitia kwa uwiano wa kiuno na nyonga na ujumla wa vipengele hatari vya magonjwa ya mishipa na moyo.[13][14]

Kielezo cha Uzani wa Mwili kinahusiana kwa karibu na asilimia ya mafuta ya mwili na jumla ya mafuta ya mwili.[15]

mtazamo wa mbele na upande wa kiwiliwili cha mwanamume aliye "mnene kupindukia". Alama za kuvutika kwa ngozi zinaonekana pamoja na jinakomastia.
Mwanamume "mnene kupindukia" aliye na Kielezo cha Uzani wa Mwili cha 47 kg/m2: uzito 146 kg (322 lb), urefu sentimita 177  (5 ft 10 in)

Katika watoto, uzito ulio bora hutofautiana kwa sababu ya umri na jinsia. Katika watoto na vijana baleghe, unene wa kupindukia hufasiliwa si kwa nambari kamili, lakini kulingana na kundi la kawaida la wakati huo, hivi kwamba unene wa kupindukia ni wa Kielezo cha Uzani wa Mwili kilichozidi asilimia 95 [16]Data ya marejeleo ambayo ilitumiwa kukadiria hesabu hii ni ya kutoka mwaka 1963 hadi 1994, hivyo haijaathiriwa na ongezeko la uzito la hivi karibuni.[17]

BMI Classification
< 18.5 underweight
18.5–24.9 normal weight
25.0–29.9 overweight
30.0–34.9 class I obesity
35.0–39.9 class II obesity
≥ 40.0   class III obesity  

Kielezo cha Uzani wa Mwili hukadiriwa kwa kugawanya uzito wa mtu kwa kipeo cha uzito wake, na kwa kawaida huandikwa aidha kwa Mfumo wa mita au kwa vipimo vya Marekani:

Metric:
US customary and imperial:

ambapo ni uzito wa mtu katika pauni na ni urefu wa mtu katika inchi.

Fasili zinazotumika mara nyingi, ambazo zilitolewa na Shirika la Afya Duniani mwaka wa 1997 na kuchapishwa mwaka wa 2000, hutoa ukadiriaji kama ilivyoorodheshwa katika jedwali lililo upande wa kulia.[4]

Baadhi ya mashirika yamerekebisha kidogo fasili zilizotolewa na SAD. Habari ya kiupasuaji hugawanya unene wa kupindukia wa "daraja la 3" katika vikundi zaidi, ambavyo ukadiriaji wake ungali unakumbwa na utata.[18]

  • Any BMI ≥ 35 or 40 is severe obesity
  • A BMI of ≥ 35 or 40–44.9 or 49.9 is morbid obesity
  • A BMI of ≥ 45 or 50 is super obesity

Kwa sababu watu wa asili ya Asia wameendelea kuathiriwa vibaya katika kiwango cha KUM cha chini kuliko kile cha Wazungu, baadhi ya mataifa yamefasili upya unene wa kupindukia; Wajapani wameufasili kama kiwango chochote cha KUM kinachozidi 25[19] huku China ikitumia kipimo cha KUM cha juu ya 28.[20]

Madhara ya kiafya[hariri | hariri chanzo]

Uzito uliozidi huhusianishwa na magonjwa mengi, hasa magonjwa ya moyo na mishipa, kisukari aina ya 2, apnea pingani ya usingizi, aina fulani za saratani, osteoathritisi[3] na pumu[21][3]. Matokeo yake ni kwamba unene wa kupindukia umetambulika kupunguza matarajio ya kuishi.[3]

Hatari ya kufa[hariri | hariri chanzo]

Relative risk of death over 10 years for White men (left) and women (right) who have never smoked in the United States by BMI.[22]

Unene wa kupindukia ni kati ya visababishi vya kifo vinavyozuilika kote ulimwenguni.[10][23][24] Utafiti mkuu wa Ulaya na Marekani umeonyesha kuwa hatari ya kufa iko chini zaidi katika kiwango cha KUM cha 20–25 kg/m2[22][25] katika watu wasiovuta sigara na 24–27 kg/m2 katika watu wanaoendelea kuvuta sigara, huku hatari hii ikiongezeka na mabadiliko kuelekea pande zote mbili.[26][27]Kipimo cha Kielezo cha Uzani wa Mwili cha zaidi ya 32 kimehusishwa na ongezeko la mara mbili la vifo kwa wanawake kwa muda wa miaka 16.[28] Nchini Marekani, inakisiwa kuwa unene wa kupindukia husababisha zaidi ya vifo 111,909 hadi 365,000 kila mwaka,[3][24] huku milioni 1 (7.7%) ya vifo katika nchi za Ulaya husababishwa na uzito uliozidi.[29][30] Kwa wastani, unene hupunguza muda wa maisha miaka 6 hadi 7:[3][31]Kielezo cha Uzani wa Mwili cha 30–35 hupunguza miaka 2 hadi 4 matarajio ya kuishi[25] ilhali unene uliokithiri (Kielezo cha Uzani wa Mwili > 40) hupunguza miaka 10 matarajio ya kuishi [25]

Hali ya kuugua[hariri | hariri chanzo]

Unene wa kupindukia huongeza hatari ya hali nyingi za kimwili na kiakili. Ambatani hizi kwa kawaida huonyeshwa sana katika dalili za magonjwa ya metaboli,[3] kama: kisukari aina ya 2, shinikizo la juu la damu, kolestro, and hypertriglyceridemia.[32]

Matatizo aidha husababishwa na unene moja kwa moja au kwa njia isiyo ya moja kwa moja inayohusiana kupitia utaratibu ulio na sababu sawa kama vile lishe duni au uzembe maishani. Uhusiano mkuu kati ya unene na hali maalum inatofautiana. Mojawapo ni kisukari aina ya 2. Mafuta ya ziada mwilini ndiyo kisababishi cha 64% ya kisukari kwa wanaume na 77% kwa wanawake.[33]

Madhara ya kiafya huwa katika vikundi viwili vipana:

Fumbo kuhusu kuendeleza uhai[hariri | hariri chanzo]

Ingawa madhara ya kiafya ya unene wa kupindukia miongoni mwa jumla ya watu imeungwa mkono na ushahidi uliopo, matokeo ya kiafya katika vikundi mahususi yanaonekana kuboreka kwa kiwango cha Kielezo cha Uzani wa Mwili kinachoongezeka. Tukio hilo linajulikana kama fumbo kuhusu kuendelea kuishi kwa watu walio na unene wa kupindukia.[38]

Mara ya kwanza fumbo hili lilielezwa mwaka 1999, likiwakumba watu wenye unene wa kupindukia waliokuwa wakisafishwa damu,[38] kisha kupatikana katika watu waliokuwa na mshtuko wa moyo na ugonjwa wa ateri za pembeni (UAP).[39]

Katika watu waliokuwa na mshtuko wa moyo, wale wenye kipimo cha Kielezo cha Uzani wa Mwili cha kati ya 30.0. na 34.9 walikuwa na kima cha vifo cha chini kuliko wenye uzito wa kawaida. Hii ni kwa sababu watu mara nyingi hupoteza uzito kadiri wanavyoendelea kuwa wagonjwa.[40]

Matokeo sawa na haya yamepatikana katika aina nyingine za magonjwa ya moyo. Watu walio na unene wa kupindukia wa daraja la 1 na magonjwa ya moyo hawana kima cha matatizo ya moyo kuliko watu walio na uzito wa kawaida ambao wana matatizo ya moyo. Hata hivyo, katika watu walio na viwango vikubwa zaidi vya unene, hatari ya kutokea kwa matatizo ya ziada huongezeka.[41][42] Hata baada ya upasuaji wa kipenyo cha moyo, hakuna ongezeko la vifo linalotambulika katika watu walio na uzito mkubwa.[43]

Utafiti mmoja ulionyesha kuwa ongezeko la muda wa kuishi kwa watu wenye unene wa kupindukia husababishwa na matibabu madhubuti ambao watu hao hupata baada ya tukio la tatizo la moyo.[44] Utafiti mwingine unaonyesha kuwa mtu anapouchukulia kwa makini ugonjwa wa muda mrefu wa kuzibika kwa mapafu (COPD) kwa walio na PDA, manufaa ya unene wa kupindukia hayapo tena.[39]

Visababishi[hariri | hariri chanzo]

Katikia kiwango cha mtu binafsi, ujumlisho wa kula chakula kinachotoa nguvu na kutofanya mazoezi ya kimwili hudhaniwa kusababisha visa vingi zaidi vya unene wa kupindukia.[45]Matukio machache sana husababishwa hasa na jeni, sababu za kimatibabu au ugonjwa wa akili.[46] Kinyume na matarajio, inakisiwa kuwa viwango vya unene wa kupindukia vinavyoongezeka katika jamii vinasababishwa na urahisi wa kupata chakula kinachovutia,[47]ongezeko la kutegemea gari na uzalishaji wa bidhaa kwa kutumia mitambo.[48][49]

Uhakiki mmoja wa 2006 ulionyesha mambo mengine kumi yanayochangia katika ongezeko la unene wa kupindukia wa hivi majuzi:

  1. kukosa usingizi wa kutosha,
  2. matatizo ya mfumo wa mwili (vichafuzi vya mazingira vinavyotatiza umetaboli wa lipidi),
  3. upungufu wa mabadiliko ya halijoto ya mazingira,
  4. upungufu wa viwango vya kuvuta sigara, kwa sababu uvutaji sigara hugandamiza hamu ya chakula,
  5. kuendelea kutumia dawa zinazoweza kusababisha ongezeko la uzito wa mwili (kwa mfano, dawa ya kuzuia magonjwa ya akili yasiyo ya kawaida),
  6. ongezeko la vikundi vya kikabila na umri vinavyoweza kukita zaidi,
  7. ujauzito wa miaka ya uzeeni (jambo ambalo linaweza kusababisha hatari ya unene wa kupindukia katika watoto),
  8. hatari za kijenetikiazinazoweza kupitishwa kutoka kizazi hadi kingine,
  9. uteuzi wa kiasili kwa watu wenye kima cha juu zaidi cha Kielezo cha Uzito wa Mwili, na
  10. kujamiiana kiubaguzi jambo ambalo huongeza vipengele hatari vya unene wa kupindukia (hii inaweza kuongezea idadi ya watu wanene sana kwa kuongezea kiwango cha tofauti kati ya idadi ya watu na uzito).[50] Ingawa kuna utafiti wa kutosha unaoonyesha jinsi taratibu hizi zinavyopelekea ongezeko la kutokea kwa unene wa kupindukia, utafiti huu bado haujaweza kutoa hitimisho kamili. Watafiti walioufanya wanasema kuwa inawezekana kuwa taratibu hizi zina athari ya kiwango cha chini kuliko zile zilizojadiliwa katika aya iliyotangulia.

Chakula bora[hariri | hariri chanzo]

Map of dietary energy availability per person per day in 1961 (left) and 2001–2003 (right) in kcal/person/day.

     no data      <1600      1600–1800      1800–2000      2000–2200      2200–2400      2400–2600

     2600–2800      2800–3000      3000–3200      3200–3400      3400–3600      >3600

A graph showing a gradual increase in global food energy consumption per person per day between 1961 and 2002.
Average per capita energy consumption of the world from 1961 to 2002[51]

Kima cha ugavi wa nguvu za kimlo kwa kila mtu hutofautiana pakubwa katika maeneo na nchi mbali mbali. Kima hiki pia kimebadilika pakubwa kwa muda mrefu sasa.[51] Kutoka mwanzoni wa miaka ya 1970 hadi mwishoni wa kiaka ya 1990, wastani wa kalori kwa kila mtu kila siku (kiwango cha chakula kilichonunuliwa) uliongezeka katika maeneo yote duniani ila Mashariki mwa Uropa. Nchi ya Marekani ilikuwa na kima cha juu zaidi cha upatikanaji, ikiwa ni kalori 3,654 kwa kila mtu katika mwaka wa 1996. Kima hiki kiliongezeka zaidi hadi 3,754 katika mwaka wa 2003.[51] Katika miaka ya mwisho ya 1990 Uropa ilikuwa na kalori &nbsp3,394; kwa kila mtu. Katika maeneo yanayostawi kiuchumi ya Asia kulikuwa na kalori&nbsp2,648; kwa kila mtu na katika kusin mwa jangwa la Sahara, watu walikuwa na kalori &nbsp 2,176;kwa kila mtu.[51][52] Jumla ya kalori inayotumika imetambulika kuwa inahusiana na unene wa kupindukia.[53]

Upatikanaji mkubwa wa vielekezo kuhusu lishe[54]haujafaulu kutatua shida za kula kupita kiasi na uamuzi mbaya kuhusu lishe.[55] Kutoka mwaka wa 1971 hadi 2000, viwango vya unene wa kupindukia viliongezeka kutoka 14.5% hadi 30.9%.[56] Katika kipindi hicho pia, wastani wa matumizi ya chakula kinachotoa nguvu yaliongezeka. Katika wanawake, wastani wa ongezeko hili ulikuwa kalori 335 kwa siku (1,542 mwaka wa 1971 na kalori 1,877 mwaka wa 2004), ilhali katika wanaume, wastani katika ongezeko hilo ulikuwa kalori 168 kwa siku (kalori 2,450 mwaka wa 1971 na kalori 2,618 mwaka wa 2004). Kiwango kikubwa cha nguvu hizi za ziada kilitokana na ongezeko la kutumia kabohidrati badala ya mafuta.[57] Vyanzo vya msingi vya kabohidrati hizi za ziada ni vinywaji vilivyo na sukari ambavyo vinakadiriwa kusababisha karibu 25% ya nguvu za kila siku katika vijana wakomavu Marekani, [58]na chipsi za viazi.[59] Utumiaji wa vinywaji vilivyo na sukari unaaminika kuchangia katika ongezeko la viwango vya unene wa kupindukia.[60][61]

Jinsi jamii nyingi zinavyoendelea kutegemea nguvu nyingi za chakula, viwango vikubwa vya chakula na vyakula duni, ndivyo uhusiano wa utumiaji wa vyakula duni na unene wa kupindukia unavyoendelea kusababisha madhara. [62] Nchini Marekani, utumiaji wa vyakula duni uliongezeka mara tatu huku utumiaji wa chakula chenye nguvu ukiongezeka mara nne kati ya mwaka 1977 na 1995.[63]

Sera za kilimo na ufundisanifu zinazozingatia mazingira nchini Marekani na barani Uropa zimesababisha kushuka kwa bei ya vyakula. Kule Marekani, hatua ya kupunguza bei ya mahindi, soya, ngano na mchele kupitia bili ya ukulima ya Marekani imepelekea kushuka kwa bei ya chakula cha viwandani ikilinganishwa na matunda na mboga.[64]

Wakati mwingi, watu wanene kupindukia hawaripoti vyema jinsi wanavyotumia chakula ikilinganishwa na wale walio na uzito wa kawaida.[65] Utafiti huu ni kwa mujibu wa uchunguzi wa watu uliofanyika katika chumba cha kipima kalori [66] na kwa kutazama moja kwa moja.

Mwenendo wa kuzembea[hariri | hariri chanzo]

Mwenendo wa kuzembea huchangia pakubwa katika unene wa kupindukia.[67] Kote ulimwenguni, watu wengi wamegeukia kazi isiyohusisha nguvu nyingi za kimwili[68][69][70] na kwa wakati huu angalau 60% ya idadi ya watu duniani hupata mazoezi yasiyotosheleza.[69] Hii hasa ni kwa sababu ya ongezeko la kutumia mitambo katika uchukuzi, na teknologia inayosaidia sana kikazi huko nyumbani.T[68][69][70] Katika watoto, viwango vya kufanya mazoezi vinaonekana kushuka kwa sababu ya kutotembea sana na kutohusika katika somo la mazoezi ya mwili.[71] Mienendo ya dunia katika burudani ambapo watu huusika moja kwa mojamazoezi ya mwili inaendelea kufifia. Shirika la Afya Duniani linaonyesha kuwa, ulimwenguni kote, watu wanaendelea kuhusika katika burudani isiyohusisha maoezi, ilhali katika utafiti mmoja huko Finland[72] ulionyesha ongezeko, ilhali utafiti mwingine huko Marekani ulionyesha kuwa mazoezi katika burudani hayajabadilika sana.[73]

Katika watoto na watu wazima, kuna uhusiano kati ya kutazama runinga na hatari ya unene wa kupindukia.[74][75][76] Ukaguzi ulitambua kuwa 63 kati ya tafiti 73 (86%) zilionyesha ongezeko katika kiwango cha unene wa kupindukia wa utotoni pindi watoto wanavyofikia vyombo vya mawasiliano, huku viwango hivi vikiongezeka kulingana na muda unaotumika kutazama runinga.ref>Media + Child and Adolescent Health: A Systematic Review (PDF). Ezekiel J. Emanuel. Common Sense Media (2008). Iliwekwa mnamo April 6, 2009.</ref>

Usomijeni[hariri | hariri chanzo]

Mchoro wa msichana mweusi wa kike mwenye nywele nyeusi, mashavu ya waridi aliye uchi akiegemea meza. Msichana huyu ameshika zabibu na majani ya zabibu katika mkono wake wa kushoto ambayo yamezifunika jenitalia zake.
Mchoro uliochorwa mwaka wa 1680 na Juan Carreno de Miranda, wa msichana aliyedhaniwa kuwa na sindromu ya Prader-Will[77]

Kama magonjwa mengine mengi, unene wa kupindukia hutokana na mwingiliano kati ya vipengele vya kijeni na vya kimazingira. Upolimofi katika jeni nyingi zinazodhibiti [[hamu ya kula[[]] na umetabolihupelekea unene wa kupindukia wakati nguvu za kutosha zinazotoka katika chakula zinapatikana. Katika mwaka wa 2006, zaidi ya 41 za sehemu hizi zimehusishwa na kuendelea kwa unene wa kupindukia wakati mazingira mwafaka yanapokuwepo.[78] Watu walio na aina mbili zajeni ya FTO (jeni inayohusishwa na wingi wa mafuta na unene wa kupindukia) wamepatikana kwa wastani kuwa na uzito wa kilogramu 3-4]]   zaidi na huwa katika hatari mara1.67 zaidi ya kukumbwa na unene wa kupindukia wakilinganishwa na wale wasio na hatari hii aleli.[79] Asilimia ya unene wa kupindukia unaoweza kuhusishwa visababishi vya kijeni ni ya kubadilika kutoka 6% hadi 85% kulingana na idadi ya watu waliochunguzwa.[80]

Unene wa kupindukia ni kipengele kikuu katika sindromu kadhaa kama vile sindromu ya Prader-Willi, sindromu ya Bardet-Biedl, sindromu ya Cohen, na sindromu ya MOMO. Neno unene wa kupindukia usiosababishwa na sindromu hutumika wakati mwingine kuzitenga hali hizi.[81] Kwa watu walio na mwanzo mkali wa mapema wa unene wa kupindukia (unaofasiliwa na mwanzo kabla ya umri wa miaka 10  na kielezo cha uzani wa mwili zaidi ya tatu standard deviation zaidi ya kawaida), 7% huwa na kipimo kimoja cha mgeuko papale [82]

Tafiti zilizolenga mitindo ya urithi badala ya jeni maalum zimetambua kuwa asilimia 80 ya watoto wa watu wawili walio wanene kupindukia walikuwa vilevile na unene wa kupindukia, ikilinganishwa na asilimia chini ya 10 ya watoto wa wazazi wawili waliokuwa na uzito wa kawaida.[83]

Nadharia tete ya jeni yenye mafanikio hudai kuwa watu wana uwezekano mkubwa wa kupatwa na unene wa kupindukia kutokana na ukosefu wa chakula wakati wa mageuko ya binadamu. Uwezo wao wa kujinufaisha katika vipindi visivyo vya kawaida vya wingi kwa kuweka nguvu kama mafuta unaweza kuwafaa katika nyakati ambapo upatikanaji wa chakula si yakini na watu walio na hifadhi kubwa ya mafuta wanaweza kuwa na uwezekano mkubwa wa kuongokanjaa. Hata hivyo, huenda jamii zilizo na chakula kwa wingi zisizoee kujiwekea mafuta.[84] Nadharia hii imeweza kukosolewa sana na kupelelea kupendekezwa kwa nadharia zingine za kimageuko kama vile nadharia tete ya jeni isiyo na mkondo nanadharia tete ya fenotipu yenye mafanikiozilizopendekezwa. [85][86]

Maradhi mengine[hariri | hariri chanzo]

Maradhi mengine ya mwili na akili na dawa za kifamasia zinazotumiwa kuyatibu zinaweza kuongeza hatari ya unene wa kupindukia. Maradhi yanayoongeza hatari ya unene huo ni sindromu kadhaa za kijenetikia zisizo za kawaida (zilizoorodheshwa hapo juu) na aidha magonjwa mengine ya kuzaliwa nayo au ya kujitokeza baada ya kuzaliwa: uhipothiroidi, Sindromu ya Cushing, kukosa homoni ya kukua,[87] na matatizo ya kula: matatizo ya kula yatokanayo na ulevi na sindromu ya kula usiku.[3].Hata hivyo, unene wa kupindukia hauchukuliwi kuwa tatizo la kiakili na kwa hiyo haujaorodheshwa katika Mwongozo wa Utambuzi na Takwimu za Maradhi ya Akili (DSM-IVR) kama maradhi ya akili.[88] Hatari ya uzito wa kupita kiasi na unene wa kupindukia iko juu kwa wagonjwa walio na maradhi ya akili kuliko kwa watu ambao hawana maradhi ya akili.[89]

Matibabu mengine yanaweza kusababisha kuongezeka kwa uzito au mabadiliko katika mchanganyiko wa mwili; nayo ni insulini, salfonyilurea, thiasolidinedioni, dawa za magonjwa ya kiakili, dawa ya unyogovu, steroidi, aina nyingine za dawa za mitukutiko (fenitoini na valproeati), pisotifeni, na za uzuiaji mimba wa kihomoni.[3]

Vigezo vya kijamii[hariri | hariri chanzo]

Ingawa athari za kijenetiki ni muhimu katika kuelewa unene wa kupindukia, haziwezi kuwajibikia mkondo uliopo wa ongezeko katika nchi fulani au duniani.[90] Ingawa imekubalika kuwa utumizi wa nguvu zaidi ya kiasi kinachostahili kutumika husababisha unene wa kupindukia kibinafsi, kisababishi cha mageuko katika vipengele hivi viwili kwa kiwango cha jamii hujadiliwa sana. Kuna nadharia kadhaa zinazohusu visababishi vya unene wa kupindukia. Hata hivyo, nadharia nyingi zimeshikilia kuwa unene husababishwa na mchanganyiko wa vipengele tofauti.

Uhusiano kati ya hadhi ya kijamii na Kielezo cha Uzani wa Mwili huwa tofauti ulimwenguni. Tathmini katika mwaka wa 1989 ilionyesha kuwa wanawake wenye hadhi ya juu ya kijamii katika nchi zinazostawii walikuwa na uwezekano mdogo wa kukumbwa na unene wa kupindukia. Hakuna tofauti muhimu zilizoonekana miongoni mwa wanaume wa hadhi tofauti za kijamii. Katika nchi zinazostawi, wanawake, wanaume na watoto kutoka katika hadhi ya juu ya kijamii walikuwa na viwango vikubwa vya unene wa kupindukia.[91]. Toleo la tathmini hii uliofanyika mwaka wa 2007 ulionyesha uhusiano uo huo lakini ulikuwa dhaifu. Upungufu katika uthabiti wa uhusiano huo ulihisika kuwa uliotokana na utandawazi.[92] Katika nchi zilizostawi, viwango vya unene wa kupindukia kwa watu wazima, na asilimia ya watoto waliobalehe walio na uzani wa kupindukia vinahusiana na tofauti za kimapato. Uhusiano kama huu hunekana katika majimbo ya Marekani: watu wengi wazima, hata walio katika matabaka ya juu katika jamii wana unene wa kupindukia hata katika majimbo yaliyo na tofauti za kimapato.[93]

Maelezo mengi yametolewa yakilinganisha Kielezo cha Uzani wa Mwili na hadhi ya kijamii. Inadhaniwa mwilia mwilizo wa kumudu vyakula bora zaidi, nao huwa katika shinikizo zaidi la kusalia wembamba kutoka kwa jamii, na wana nafasi na matumaini makubwa ya kudumisha siha njema ya kimwili. Katika nchi zisizostawi inaaminika kuwa uwezo wa kumudu chakula, utumizi mkubwa wa nguvu katika kufanya kazi za sulubu, na tamaduni zinazothamini miili mikubwa huchangia katika kuleta mitindo hii.[92] Mitazamo inayoshikiliwa na watu kuhusu ukubwa wa mwili maishani pia inaweza kuchangia unene wa kupindukia. Uhusiano wa mabadiliko katika Kielezo cha Uzani wa Mwili kwa muda mrefu umeonekana miongoni mwa marafiki, ndugu na wachumba.[94] Stress and perceived low social status appear to increase risk of obesity.[93][95][96]

Uvutaji sigara huathiri pakubwa uzani wa mtu. Watu wanaokoma kuvuta sigara huongeza uzito kwa wastani wa kilo 4.4  9.7 lb) katika wanaume na kilo 5.0 (11.0 lb) katika wanawake kwa muda wa miaka kumi.[97] Hata hivo mabadiliko katika viwango vya uvutaji yamekuwa na matokeo duni kwa viwango vya jumla vya unene wa kupindukia.[98]

Nchini Marekani, idadi ya watoto alionao mtu inahusiana na hatarisho lao la unene wa kupindukia. Hatari ya mwanamke huongezeka kwa 7% kwa kila mtoto, ilhali hatarisho la mwanamume huongezeka kwa 4%.[99] Hii inaweza kuelezwa kwa kiasi fulani kutokana na ukweli kwamba kuwa na watoto wanaokutegemea hupunguza shughuli za kimwili kwa wazazi katika nchi za Ulaya na Marekani.[100]

Katika nchi zinazostawi, ukuaji wa miji unachangia katika kiwango kinachoongezeka cha unene wa kupindukia. Nchini Uchinaviwango vya jumla vya unene wa kupindukia viko chini ya asilimia 5; hata hivyo, katika miji mingine, viwango vya unene wa kupindukia ni zaidi ya asilimia 20.[101]

Utapiamlo mwanzoni mwa maisha umeaminika kuchangia katika viwango vinavyoongezeka vya unene wa kupindukia katikanchi zinazostawi.[102]Mabadiliko ya endokrini yanayotokea katika vipindi vya utapiamlo yanaweza kuendeleza uhifadhiwaji wa mafuta mara tu chakula zaidi kiletacho nguvu kinapopatikana.[102]

Sawa na data za epidemiolojia tambuzi, na tafiti nyingi huthibitisha kuwa unene wa kupindukia unahusiana na upungufu katika utambuzi. [103] Iwapo unene wa kupindukia husababisha upungufu katika utambuzi kwa vyovyote vile bado haijulikani kwa sasa.

Vikolezo viambukizi[hariri | hariri chanzo]

Utafiti wa jinsi vikolezo viambukizi vinavyoathiri umetaboli ungali katika hatua zake za kwanza. Flora ya utumbo imeonekana kutofautiana kati ya watu wembamba na wale walio na unene wa kupindukia. Kuna ishara kuwa flora ya utumbo katika watu wanene kupindukia na wale wembamba inaweza kuathiri uwezo wa umetaboli. Mabadiliko haya dhahiri katika uwezo wa umetaboli yanaaminika kuchangia kwa kiwango kikubwa katika kuvuna nguvu zinazosababisha unene wa kupindukia. Iwapo tofauti hizi ndizo visababishi vya moja kwa moja au ndiyo matokeo ya unene wa kupindukia, bado haijabainishwa kwa kiasi kisichopotosha[104]

Uhusiano kati ya virusi na unene wa kupindukia umeonekana kwa wanadamu na spishi kadhaa za wanyama. Kiasi ambacho ushirikiano huu unaweza kuwa umechangia katika kuongezeka kwa kiwango cha unene wa kupindukia bado hakijabainishwa.[105]

Pathofiziolojia[hariri | hariri chanzo]

Panya wawili weupe wenye masikio yanayotoshana, macho meusi na pua za waridi. Hata hivyo upana wa mwili wa panya aliye kushoto ni takribani mara tatu zaidi ya ule wa panya wa kulia aliye na ukubwa wa kawaida.
Ulinganisho wa panya asiyeweza kutoa leptini na hatimaye kupelekea unene wa kupindukia (kushoto) na panya wa kawaida (kulia)

Flier anafupisha taratibu nyingi za pathofiziolojia zinazohusika katika ukuaji na udhibiti wa unene wa kupindukia.[106] Kitengo hiki cha utafiti kilikuwa hakijaangaziwa hadi mwaka wa 1994leptini ilipogunduliwa. Tangu ugunduzi huu ulipofanyika, taratibu zingine nyingi za homoni zinazohusika katika udhibiti wa hamu ya kula na ulaji, mitindo ya uhifadhi ya tishu ya mafuta na ukuaji wa ukinzani kwa insulini zimefumbuliwa. Tangu kuvumbuliwa kwa leptini, grelin, insulini, oreksini, PYY 3-36, kolesistokinini,adiponektini, na vipengele vinginevyo zimechunguzwa. Adipokini ni chembe zinazoundwa na tishu ya mafuta; utendakazi wake unadhaniwa kubadilisha magonjwa mengi yanayohusiana na unene wa kupindukia.

Inachukuliwa kuwa leptini na grelini hufanya kazi pamoja katika jinsi zinavyoathiri hamu ya kula; huku grelini, inayotolewa na tumbo, ikirekebisha uthibiti wa muda mfupi wa hamu ya kula (yaani kula wakati ambapo tumbo liko tupu na kukoma tumbo inapotanuka). Leptini hutolewa na tishu ya mafuta kuchochea hifadhi za mafuta mwilini na kupatanisha uthibiti wa muda mrefu wa hamu ya kula (yaani, kula kwa wingi ambapo hifadhi za mafuta ziko chini na kula kiasi kidogo zinapokuwa juu). Ingawa utoaji wa leptini unaweza kufaa katika kikundi kidogo cha watu wenye unene wa kupindukia walio na upungufu wa leptini, watu wengi wenye unene huu hufikiriwa kuwa wenye ukinzani wa leptini na wamepatikana kuwa na viwango vya juu vya leptini.[107] Ukinzani huu hufikiriwa kueleza kwa kiasi fulani sababu inayofanya utoaji wa leptini usionekane kufaa katika kukandamiza hamu ya kula kwa watu wengi walio na unene wa kupindukia.[106]

Modeli ya mitazamo mitatu iliyo na jozi mbili za nguzo mkabala zilizopinda na kushikanishwa pamoja kwenye miisho na sehemu zingine zilizopangwa katika mistari.
Kielelezo cha molekuli ya leptini

Ingawa leptini na grelini hutolewa pembezoni, zinadhibiti hamu ya kula kupitia jinsi zinavyoathirimfumo mkuu wa neva. Hasa, leptini na grelini, na homoni zingine zinazohusiana na hamu ya kula huichochea hipothalamasi, sehemu ya ubongo iliyo muhimu zaidi katika kudhibiti ulaji na utumiaji wa nguvu. Kuna mizunguko kadhaa katika hipothalamasi inayochangia kwenye jukumu lake katika kuongeza na kudumisha hamu ya kula, ambapomelanokotini ndiyo njia inayoeleweka vizuri sana.[106] Mzunguko huu huanzia katika sehemu ya hipothalamasi iitwayo kiini akueti, ambayo matokeo yake huenda kwenye hipothalamasi ya pembeni na hipothalamasi inayotambua shibe, sehemu za ubongo zinazodhibiti kula na shibe mtawalia.[108]

Kiini akueti kina makundi mawili tofauti ya nyuroni.[106] Kundi la kwanza hudhirisha nuropeptaidi Y na peptaidi inayohusiana na agouti kwa pamoja na kuchangia katika kuichochea hipothalamasi ya pembeni na kuikandamiza hipothalamasi inayotambua shibe. Kundi la pili hudhihirisha pro-opiomelanokotini na nakala inayodhitiwa na kokeni na amfetamini (NIKA) na huchangia katika kuichochea hipothalamasi inayotambua shibe na kuikandamiza hipothalamasi ya pembeni. Kwa hiyo, nyuroni za nuropetaidi Y/peptaidi inayohusiana na agouti (NPY/AgRP) huchochea kula na kuzuia kushiba, ilhali nuroni za POMC/NIKA huchochea kushiba na kuzuia kula. Makundi yote mawili ya nuroni za kiini akueti nuroni hudhibitiwa kwa kiasi fulani na leptini. Leptini hukandamiza kundi la nuropetaidi Y/peptaidi inayohusiana na agouti (NPY/AgRP) huku ikilichochea kundi la POMC/NIKA. Kwa hivyo, ukosefu wa uchochelezi wa leptini, iwe ni kutokana na ukosefu wa leptini au ukinzani kwa leptin, hupelekea kula zaidi na inaweza kusababisha unene wa kupindukia wa kijenetikia na wa kupatikana maishani.[106]

Afya ya umma[hariri | hariri chanzo]

Shirika la Afya Duniani (WHO) linatabiri kuwa hivi karibuni, uzito wa kupita kiasi na unene wa kupindukia unaweza kuchukua nafasi ya matatizo ya jadi ya afya ya umma kama vile utapiamlo na magonjwa ya kuambukiza kama visababishi vikuu vya afya duni.[109] Unene wa kupindukia ni tatizo la afya ya umma na la kisera kwa sababu yaueneaji wake, gharama na athari za kiafya.[110] Juhudi za afya ya umma hulenga kuelewa na kurekebisha mazingira yanayochangia kukithiri kwa unene wa kupindukia miongoni mwa watu. Suluhisho hutazamia kubadilisha mambo yanayosababisha utumiaji zaidi wa vyakula viletavyo nguvu na kukandamiza shughuli/mazoezi ya mwili. Juhudi ni programu za milo zinazofadhiliwa na serikali katika shule, kupunguza uuzaji wachakula visivyo bora kwa watoto, [111] na kupunguza upatikanaji wa vinywanji vyenye sukari katika shule.[112] Juhudi zimefanywa katika uundaji wa mazingira ya miji ili kuongeza ufikiaji wa bustani na kutengeneza njia za waendao kwa miguu.[113]

Nchi nyingi pamoja na vikundi vimechapisha ripoti zinazohusu unene wa kupindukia. Mnamo mwaka wa 1998, miongozo ya kwanza ya serikali ya shirikisho ya Marekani ilichapishwa kwa jina "Clinical Guidelines on the Identification, Evaluation, and Treatment of Overweight and Obesity in Adults: The Evidence Report" (Mwongozo wa Kitabibu kuhusu Utambuzi, Utathmini na Matibabu ya Unene na Unene wa Kupindukia katika Watu Wazima).[114] Mnamo mwaka wa 2006 Mfumo wa Unene wa Kupindukia wa Kanada ulichapisha "Canadian Clinical Practice Guidelines (CPG) on the Management and Prevention of Obesity in Adults and Children" [Taratibu za Kitabibu za Kanada zinazohusu Udhibiti na uzuiaji wa Unene wa Kupindukia kwa Watu Wazima na Watoto] Huu ni utaratibu wa kina unaozingatia ushahidi ili kushughulikia udhibiti na uzuiaji wa uzani wa kupita kiasi na unene wa kupindukia kwa watu wazima na watoto.[115]

Mnamo mwaka wa 2004 nchini Uingereza, Chuo cha Mafizishiani cha Royal, Kitengo cha Afya ya Umma na Chuo cha Pediatria na Afya ya Watoto vilitoa ripoti, “Kuhifadhi Matatizo", iliyodokeza kuhusu kuongezeka kwa tatizo la unene wa kupindukia nchini Uingereza. [116] Mwaka huohuo, Kamati Teule ya Afya ya Bunge la Uingereza ilichapisha "uchunguzi wake wa kina zaidi [...] uliowahi kufanywa kuhusu athari ya unene wa kupindukia kwa afya na jamii nchini Uingereza na njia mwafaka zinazoweza kutumiwa katika kutatua tatizo hili.[117] Mwaka wa 2006, Taasisi ya Kitaifa ya Afya na Ubora wa Kitabibu ilitoa utaratibu wa kutambua na kutibu unene wa kupindukia na vilevile athari za kisera kwa mashirika yasiyo ya kiafya kama vile mabaraza ya mitaa[118] Ripoti iliyotolewa na Bwana Derek Wanless mwaka wa 2007 kwa Hazina ya Mfalme ilionya kuwa iwapo hatua zaidi hazitachukuliwa, unene wa kupindukia una uwezo wa kulemaza Huduma ya Afya ya Kitaifakifedha.[119]

Hatua za kina zinabuniwa ili kuthibiti viwango vinavyoongezeka vya unene wa kupindukia. Mfumo wa Sera ya Kukabiliana na Unene wa Kupindukia hugawanya hatua kwa sera za ‘juu’, sera za ‘katikati’ na sera za ‘chini’. Sera za ‘juu’ zinalenga kubadilisha jamii, sera za ‘kati’ hujaribu kubadilisha mienendo ya watutu ili kuzuia unene wa kupindukia nazo sera za ‘chini’ hujaribu kuwahudumia wale ambao tayari wameathirika.[120]

Udhibiti[hariri | hariri chanzo]

Kifurushi cha kadibodi kinachotumika kupakia aina mbili za dawa zinazotumika kutibu unene wa kupindukia. Orlistat imeonyeshwa hapo juu chini ya jina la chapa la Xenical kwa kifurushi cheupe kilicho na nembo ya Roche kwa kona hapo chini upande wa kulia (jina Roche lililo kwenye pembe sita). Sibutramine iko hapo chini, chini ya chapa Meridia. Kifurushi kina rangi nyeupe upande wa juu na samawati upande wa chini zilizotenganishwa na utepe wa kupima. Herufi A ya Abbott iko kwenye nusu ya chini ya kifurushi.
Orlistat (Xenical), tiba inayotumika sana katika kutibu unene wa kupindukia, na sibutramine(Meridia) dawa iliyoondolewa hivi karibuni kutokana na athari zake kwa moyo

Matibabu makuu ya unene wa kupindukia ni kudhibiti jinsi unavyokula and mazoezi ya mwili.[45]Mipango ya lishe inaweza kupelekea kupoteza uzitokwa kipindi cha muda mfupi[121] lakini kudumisha kiwango hiki cha kupoteza uzito mara nyingi huwa vigumu na hivyo huhitaji kudumisha mwenendo wa maisha ya mazoezi ya kimwili na kula chakula kilicho na kiwango cha chini cha nguvu.[122][123]Kufanikiwa kudumisha kiwango cha kupoteza uzani na mabadiliko katika mienenbo ni chini mno kati ya asilimia 2 - asilimia 20.[124]Mabadiliko ya kilishe na kimienendo ni muhimu katika kudhibiti uongezaji wa kupita kiasi wa uzani katika ujauzito na kuboresha hali ya mama na mtoto.[125]

Aina moja ya dawa, Orlistat (Xenical), inapatikana kwa urahisi na imeidhinishwa kwa matumizi ya muda mrefu. Hata hivyo, kupoteza uzito ni jambo la kadri kwa wastani wa kilogramu 2.9  kg (6.4 lb) kwa mwaka 1 hadi 4 na kuna habari kidogo kuhusu jinsi dawa hizi zinavyoathiri matatizo ya muda mrefu ya unene wa kupindukia.[126] Matumizi yake yanahusiana na viwango vya juu vya athari kwa utumbo [126] and concerns have been raised about negative effects on the kidneys.[127] Aina zingine mbili za dawa pia zinapatikana Lorcaserin(Belviq) hupelekea upotezaji wa uzito kwa wastani kilogramu 3.1  (asilimia 3 ya uzani wa mwili) zaidi ya plasebo kwa muda wa mwaka mmoja.[128] Mchanganyiko wa phentermine na topiramate (Qsymia) pia ni bora kwa kiwango fulani.[129]

Njia mwafaka zaidi ya kutibu unene wa kupindukia ni upasuaji wa kibariatriki. Upasuaji kwa mujibu wa unene mkali wa kupindukia unahusiana na upotezaji wa uzito kwa muda mrefu na upunguaji katika vifo kwa ujumla. Utafiti mmoja ulitambua upotezaji wa uzito wa kati wa asilimia 14 na 25 (kulingana na utaratibu uliofuatwa) kwa miaka 10  na upunguaji wa asilimia 29 katika vifo vitokanavyo na unene huu ikilinganishwa na hatua za kawaida za upotezaji wa uzito.[130] Hata hivyo, kutokana na gharama yake na hatari ya matatizo, watafiti wanatafuta tiba zingine mwafaka ilhali zisizo na madhara.

Epidemiolojia[hariri | hariri chanzo]

World obesity prevalence among males (left) and females (right).[131]

     <5%      5–10%      10–15%

     15–20%      20–25%      25–30%

     30–35%      35–40%      40–45%

     45–50%      50–55%      >55%

Kabla ya karne ya 20, unene wa kupindukia ulikuwa wa nadra;[132] in 1997 the WHO formally recognized obesity as a global epidemic.[58] As of 2005 the WHO estimates that at least 400 million adults (9.8%) are obese, with higher rates among women than men.[133] Kiwango cha unene wa kupindukia pia huongezeka kulingana na umri kwa angalau kufikia umri wa miaka 50 au 60  [134] na unene mkali wa kupindukia nchini Marekani, Australia, na Canada unaongezeka haraka kuliko kiwango cha jumla cha unene wa kupindukia.[18][135][136]

Ijapokuwa uliwahi kuchukuliwa kama tatizo la nchi zilizo na mapato ya juu pekee, viwango vya unene wa kupindukia vinaongezeka ulimwenguni kote na kudhuru nchi zilizostaw na aidha zinazostawi[29].Ongezeko hili limeonekana sana katika maeneo ya miji.[133] Sehemu inayobakia ulimwenguni ambayo unene wa kupindukia sio jambo la kawaida nimataifa ya kusini mwa sahara.[3]

Historia[hariri | hariri chanzo]

Mwanamume mwenye unene zaidi wa kupindukia aliye na kidevu chenye sehemu mbili, masharubu, na kuvalia nguo nyeusi huku akiwa na kitara kwenye upande wake wa kushoto.
KatikaEnzi za Kati nakipindi cha mvuvumko, mara nyingi unene wa kupindukia ulionekana kama ishara ya utajiri na ulikuwa umekithiri kwa tabaka aali: The Tuscan General Alessandro del Borro, attributed to Charles Mellin, 1645[137]
Kisanamu kilichochongwa kutoka kwa jiwe kilionyesha mwanamke mwenye unene wa kupindukia.
Venus of Willendorf kilichotengenezwa 24,000–22,000 BC

Wagiriki ndio waliokuwa wa kwanza kutambua unene wa kupindukia kama tatizo la kiafya.[132] "Hippocrates aliandika kuwa "Unene wa kupindukia si ugonjwa kivyake tu, bali ni dalili ya magonjwa mengine".[3] Daktari Mhindi wa upasuaji Sushruta (karne ya 6 BCE) alihusisha unene wa kupindukia na kisukari na matatizo ya moyo.[138] He recommended physical work to help cure it and its side effects.[138]Katika historia ya watu, wanadamu wamekumbwa sana na ukosefu wa chakula.[139]Kwa hivyo, kihistoria, unene wa kupindukia umeonekana kama ishara ya utajiri na ustawi. Ulikuwa umekithiri kwa maafisa wakuu barani Uropa katika Enzi za Kati na Kipindi cha Mvuvumko[137] as well as in Ancient East Asian civilizations.[140]

Kwa kuwepo kwa mwanzo wa mvuvumko wa viwanda, iligunduliwa kuwa uwezo wa kijeshi na kiuchumi wa mataifa ulitegemea ukubwa wa mwili na nguvu za wanajeshi na wafanyikazi.[58] Kuongeza wastani wa kielezo cha uzito wa mwili kutoka kile kinachofikiriwa kuwa uzito wa chini hadi kwa kile kilicho anuwai ya kawaida kulichangia pakubwa katika ustawi wa jamii zilizo na viwanda.[58] Kutokana na hayo, kimo na uzito viliongezeka katika karne ya 19  katika nchi zilizostawi. Katika karne ya 20, watu walipofikia kikamilifu uwezo wao wa kijenetiki wa kimo, uzito ulianza kuongezeka sana zaidi ya kimo na kupelekea unene wa kupindukia.[58]Katika miaka ya 1950, kuongezeka kwa utajiri katika nchi zilizostawi kulipunguza vifo vya watoto. Hata hivyo, uzito ulipoongezeka, ugonjwa wa moyo na figo ulikithiri.[58][141] Katika kipindi hiki, kampuni za bima ziligundua uhusiano kati ya uzito na matarajio ya muda wa kuishi na hivyo basi zikaongeza malipo ya bima kwa walio na unene wa kupindukia.[3]

Tamaduni nyingi katika historia zimeona unene wa kupindukia kama ambayo inatokana na makosa ya kimienendo. Mwigizaji aliyekuwa na obesus au mafuta katikauigizaji wa Kigriki aliwakilisha ulafi na utani. Katika nyakati za Ukristo, chakula kilichukuliwa kama njia inayoelekeza kwenye dhambi za uzembenatamaa.[12] Katika tamaduni za kisasa za Ulaya na Marekani, unene wa kupita kiasi unachukuliwa kama jambo lisilovutia na unene wa kupindukia mara nyingi huhusishwa na mambo kadhaa mabaya yasiyo na uasili. Watu wa umri tofauti wanaweza kufedheheshwa na kulengwa na wadhalimu au kutengwa na wenzao. Unene wa kupindukia kwa mara nyingine ni sababu ya ubaguzi[142]

Fahamu za umma katika jamii ya Ulaya na Marekani kuhusu uzito bora wa mwili zinatofautiana na zile zinazohusu uzito unaofikiriwa kuwa bora  – na zote zimebadilika tangu mwanzo wa karne ya 20. Uzito unaochukuliwa kuwa bora umekuwa chini tangu miaka ya 1920. Marekani uliongezeka kwa asilimia 2 kutoka mwaka wa 1922 hadi 1999 ilhali wastani wa uzito wao ulipungua kwa asilimia 12.[143] Kwa upande mwingine, mitazamo ya watu kuhusu uzito bora imebadilika na kuchukua mkondo pinzani. Nchini Uingereza, uzito ambapo watu walijiona kuwa na uzito wa kupita kiasi ulikuwa juu kwa kiasi cha haja katika mwaka wa 2007 kuliko 1999.[144] Mabadiliko haya yanaaminika kusababishwa na viwango vinavyoongezeka vya uadiposi (unene), hali inayopelekekea ukubalifu wa mafuta ya ziada mwilini kama jambo la kawaida.[144]

Unene wa kupindukia ungali unachukuliwa kuwa ishara ya utajiri na ufanisi katika sehemu nyingi za Afrika. Hili limekuwa jambo la kawaida hasa tangu kuzuka kwa janga la VVUlilianza. [3]

Sanaa[hariri | hariri chanzo]

Sanaa ya kwanza ya uchongaji iliyoleta mfano wa mwili wa binadamu kati ya miaka 20,000 - 35,000   iliyopita ilionyesha wanawake walio na unene wa kupindukia. Baadhi ya watu huihusisha sanamu ya Zuhurana juhudi za kusisitiza uwezo wa kuzaa ilhali wengine huhisi kuwa wao husimamia “unene” kwa watu wa wakati huo.[12] Hata hivyo, unene wa kupindukia haupo katika sanaa ya Wagiriki na Waroma, yamkini kwa kudumisha ulimbwende wao kwa mujibu wa kiasi. Haya yaliendelea katika sehemu kubwa ya historia ya ukristo barani Uropa ambapo wale tu walio na mapato ya chini wakichukuliwa kuwa wenye unene wa kupindukia.[12]

Katika Kipindi cha Mvuvumko, baadhi ya watu katika tabaka la juu walianza kuuringia ukubwa wao jinsi inavyoonekana katika picha za Henry wa nane na Alessandro del Borro.[12]Rubens (1577–1640) alionyesha wanawake wenye miili mikubwa katika picha zake, ambapo anatoa neno Rubenesque. Hata hivyo, wanawake hawa bado walilidumisha umbo la shisha na uhusiano wake na uwezo wa kuzaa.[145] Katika karne ya 19   mitazamo kuhusu unene wa kupindukia ilibadilika katika nchi za Ulaya na Amerika. Baada ya karne kadhaa ambapo unene wa kupindukia ulihusiana na mali na hadhi ya kijamii katika jamii, wembamba ulianza kuonekana kama kipimo kifaacho.[12]

Jamii na utamaduni[hariri | hariri chanzo]

Athari za kiuchumi[hariri | hariri chanzo]

Pamoja na athari zake za kiafya, unene wa kupindukia husababisha matatizo mengi yakiwemo ugumu katika ajira [146][147] na gharama za juu za biashara. Athari hizi zinazikumba sekta zote za jamii kutoka kwa watu binafsi, hadi kwa mashirika, na hadi kwa serikali.

Katika mwaka wa 2005, gharama za kimatibabu zinazoweza kuhusishwa na unene wa kupindukia nchini Marekani zilikuwa takribani dola bilioni  190.2   au asilimia 20.6 ya gharama zote za kimatibabu,[148] [149][150] while the cost of obesity in Canada was estimated at CA$2 billion in 1997 (2.4% of total health costs).[45] Jumla ya gharama ya unene wa kupindukia nchini Kanada ilikuwa imekadiriwa kuwa dola bilioni 2 za Australia katika mwaka wa 2005. Waustralia walio na uzito wa kupita kiasi na wanene kupindukia pia walipokea dola za Australia bilioni 35.6 kama ruzuku kutoka kwa serikali.[151] Kadiri ya gharama ya bidhaa za lishe imekadiriwa kuwa kati ya dola bilioni 40  hadi dola bilioni 100&nbsp  nchini Marekani pekee.[152]

Miradi ya kuzuia unene wa kupindukia imezinduliwa ili kupunguza gharama ya kutibu magonjwa yanayohusiana na unene huu. Hata hivyo, jinsi watu wanavyoendelea kuishi ndivyo wanavyogharamika zaidi. Kwa hivyo, watafiti huafiki kuwa kupunguza unene wa kupindukia kunaweza kuidumisha afya ya umma lakini huenda isipunguze gharama ya jumla ya afya..[153]

Kiti cha ziada kipana kando ya viti kadhaa vyenye ukubwa wa kawaida.
Ni sharti huduma ziwazingatie watu walio na unene wa kupindukia kwa vifaa maalumu kama vile viti vipana.[154]

Unene wa kupindukia unaweza kusababisha fedheha ya kijamii na ugumu katika ajira.[146] Wakilinganishwa na wenzao walio na uzito wa kawaida, wafanyikazi walio na unene wa kupindukia kwa wastani wana viwango vya juu vya kutokuwa kazini kwao na huchukua likizo ya udhaifu mara kwa mara na kupelekea kuongezeka kwa gharama upande wa waajiri na kupunguka kwa tija.[155] Utafiti wa kuwachunguza wafanyikazi wa chuo kikuu cha Duke ulionyesha kuwa watu walio na kielezo cha uzito wa mwili zaidi ya 40 walijiandikisha kufidiwa katika fidia ya wafanyikazi mara mbili zaidi ya wale ambao kielezo chao cha uzito wa mwili kilikuwa 18.5-24.9. Pia siku zao za kutofika kazini kwao zilikuwa zaidi ya mara 12  ikilinganishwa na wenzao wasio na kielezo cha juu cha uzito wa mwili. Majeraha ya mara kwa mara katika kikundi hiki yalitokana na kuanguka na kunyanyuka hivyo ikiathiri miguu, vifundo vya mikono au mikono, na migongo.[156] Bodi ya Bima ya Wafanyikazi katika Jimbo la Alabama nchini Marekani iliidhinisha mpango tata wa kuwatoza wafanyikazi walio na unene wa kupindukia dola 25 kila mwezi iwapo hawachukui hatua za kuupunguza uzito wao na kudumisha afya yao. Hatua hizi zilianza Januari 2010 na zinalenga wale walio na Kielezo cha Uzito wa Mwili cha zaidi ya kilo 35  kwa kila mita 2 wanaokosa kuboresha afya yao baada ya mwaka mmoja.[157]

Utafiti fulani umeonyesha kuwa watu walio na unene wa kupindukia wana uwezekano mdogo wa kuajiriwa na pia wana uwezekano mdogo wa kupandishwa cheo.[142] Watu hawa pia hulipwa mshahara wa chini kuliko wenzao wasio na unene huu wa kupindukia kwa kazi sawa. Wanawake na wanaume walio na unene wa kupindukia kwa wastani hupata asilimia 6 na 3 chini mtawalia.[158]

Nyanja mahususi kama vile shirika la ndege, afya na nyanja za vyakula, zina matatizo maalumu. Kutokana na viwango vinavyoongezeka vya unene wa kupindukia, mashirika ya ndege yanakumbwa na gharama ya juu ya mafuta na shinikizo la kuongeza upana wa viti.[159] Katika mwaka wa 2000, uzito wa ziada wa abiria wenye unene wa kupindukia uliyagharimu mashirika ya ndege dola za Marekani milioni 275 .[160] Ulimwengu wa afya umelazimika kuwekeza katika vifaa maalumu vya kuwashughulikia wagonjwa walio na unene zaidi wa kupindukia vikiwemo vifaa maalumu vya kunyanyua na ambyulensi ya kibariatrikis.[161]Gharama za hoteli zimeongezwa na mahakama kwa shutma za kusababisha unene wa kupindukia.[162] Mnamo mwaka wa 2005, bunge la Marekani lilijadili utungaji sheria ya kuzuia kesi za raia dhidi ya sekta ya vyakula kwa mujibu wa unene wa kupindukia; hata hivyo, haikufanikiwa kuwa sheria..[162]

Ukubalifu wa ukubwa[hariri | hariri chanzo]

Rais wa Marekani William Howard Taft alidhihakiwa mara nyingi kwa kuwa na uzito wa kupita kiasi

Lengo kuu la vuguvugu la ukubalifu wa unene ni kupunguza ubaguzi dhidi ya watu walio na unene na uzito wa kupindukia.[163][164] Hata hivyo, wengine katika vuguvugu hilo pia wanajaribu kupinga uhusiano uliothibitishwa kati ya unene wa kupindukia na athari mbaya za kiafya.[165]

Kunayo mashirika kadhaa yanayoendeleza ukubalifu wa unene wa kupindukia. Umaarufu wa mashirika haya umeongezeka katika nusu ya hivi karibuni ya karne ya 20  .[166]Shirika la Kitaifa la Kuendeleza Ukubalifu wa Unene]] nchini Marekani [[lilianzishwa mwaka wa 1969 na hujieleza kama shirika la haki za raia linalolenga kukomesha ubaguzi wa ukubwa.[167] Hata hivyo, uhamasishaji juu ya unene umebaki harakati za pembeni.[168]

Shirika la Kimataifa la Ukubalifu wa Ukubwani shirika lisilo la kiserikali lililoanzishwa mnamo mwaka wa 1997. Shirika hili ni la kimataifa na hueleza lengo lake kama kuendeleza ukubalifu wa ukubwa na kusaidia kukomesha ubaguzi kwa misingi ya uzito.[169] Vikundi hivi mara nyingi hupigania kutambulika kwa unene wa kupindukia kama ulemavu chini ya Sheria ya Wamarekani Walio na Ulemavu Hata hivyo, mfumo wa kisheria wa Marekani umeamua kuwa gharama zitakazokuwa za afya ya umma zinazidi faida za kueindeleza sheria hii ya dhidi ya ubaguzi kujumlisha unene wa kupindukia.[165]

Unene wa utotoni[hariri | hariri chanzo]

Kielezo cha Uzito wa Mwili mwafaka hutofautiana kulingana na umri na jinsia ya mtoto. Unene katika watoto na vijana huelezwa kama Kielezo cha Uzito wa Mwili cha zaidi ya  asilimia.[16]95. Data ya marejeo yenye ndio mzingi wa asilimia hizi ni kutoka 1963 hadi 1994 na hivyo haijaathiriwa na ongezeko la kiwango cha unene cha hivi karibuni.[17] Unene wa utotoni umefika kiwango cha mlipuko katika karne ya 21  , kukiwa na ongezeko la kiwango katika nchi zimeendelea na zinazoendelea. Kima cha unene kwa wavulana chini Kanada imeongezeka kutoka 11% miaka ya 1980s hadi zaidi ya 30% miaka ya 1990, bali kwa kipindi cha muda huu kiwango kiliongezeka kutoka 4 hadi 14% katika watoto wa Brazili.[170]

Kama ilivyo na unene katika watu wazima, hali nyingi tofauti huchangia kwa viwango vingi ongezeko la unene utotoni. Ubadilishaji wa lishe na upungufu wa mazoezi ya mwili huaminika kuwa ndizo visababishi viwili vya hivi karibu muhimu zaidi vya ongezeko la viwango.[171] Kwa sababu unene wa utotoni huendelea hadi wakati wa utu uzima na unahusishwa na magonjwa mengi yanayodumu, watoto walio wanene mara nyingi huchunguzwashinikizo la juu la damu, Ugonjwa wa kisukari, hipalipidimia, na ini yenye mafuta.[45] Matibabu yanayotumika kwa watoto hasa ni hatua ya hali ya maisha na mbinu za mwenendo, hata hivyo bidii za kuongezea mazoezi kwa watoto zimekuwa na mafanikio madogo.[172]Nchini Marekani, dawa hazikubaliwi na Muungano wa Chakula na Dawa kutumika katika kikundi hiki cha umri.[170]

Katika wanyama[hariri | hariri chanzo]

Unono katika mifugo ni jambo la kawaida katika nchi nyingi. Kiwango cha unono uliozidi katika mbwa kule Marekani ni kutoka 23% hadi 41%, 5.1% yao wakiwa ni wanono.[173]Rates of obesity in cats was slightly higher at 6.4%.[173]Nchini Australia kiwango cha unene wa kupindukia katika mbwa kwa muktadha wa utabibu wa mifugo imepatikana kuwa 7.6%.[174] Hatari za unono kwa mbwa inahusiana na unene wa wamiliki; hata hivyo, hakuna uhusiano kama huo baina ya paka na wamiliki.[175]

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. Ēsus is the past participle of edere (to eat), with ob (over) added to it. Online Etymology Dictionary: Obesity. Douglas Harper. Iliwekwa mnamo December 31, 2008.; Kamusi ya Kingereza ya Oxford ilichapisha kutumika kwake kwa mara ya kwanza mnamo mwaka wa 1611 na Randle Cotgrave. Obesity, n. Oxford English Dictionary 2008. Iliwekwa mnamo March 21, 2009.
  2. 2.0 2.1 WHO 2000 p.6
  3. 3.00 3.01 3.02 3.03 3.04 3.05 3.06 3.07 3.08 3.09 3.10 3.11 3.12 3.13 3.14 3.15 3.16 Haslam DW, James WP (2005). "Obesity". Lancet 366 (9492): 1197–209. PMID 16198769. doi:10.1016/S0140-6736(05)67483-1. 
  4. 4.0 4.1 WHO 2000 p.9
  5. http://www.medicalnewstoday.com/releases/24118.php
  6. Kushner, Robert (2007). Treatment of the Obese Patient (Contemporary Endocrinology). Totowa, NJ: Humana Press. p. 158. ISBN 1-59745-400-1. Retrieved April 5, 2009. 
  7. Adams JP, Murphy PG (July 2000). "Obesity in anaesthesia and intensive care". Br J Anaesth 85 (1): 91–108. PMID 10927998. doi:10.1093/bja/85.1.91. 
  8. NICE 2006 p.10–11
  9. Imaz I, Martínez-Cervell C, García-Alvarez EE, Sendra-Gutiérrez JM, González-Enríquez J (July 2008). "Safety and effectiveness of the intragastric balloon for obesity. Uchanganuzi wa kina". Obes Surg 18 (7): 841–6. PMID 18459025. doi:10.1007/s11695-007-9331-8. 
  10. 10.0 10.1 Barness LA, Opitz JM, Gilbert-Barness E (December 2007). "Obesity: genetic, molecular, and environmental aspects". Am. J. Med. Genet. A 143A (24): 3016–34. PMID 18000969. doi:10.1002/ajmg.a.32035. 
  11. Huko wengine wanalazimika kutumia vifaa maalum (butt wipers]) kushililia karatasi shashi wakiwa msalani
  12. 12.0 12.1 12.2 12.3 12.4 12.5 Woodhouse R (2008). "Obesity in art: A brief overview". Front Horm Res. Frontiers of Hormone Research 36: 271–86. ISBN 978-3-8055-8429-6. PMID 18230908. doi:10.1159/000115370. 
  13. Sweeting HN (2007). "Measurement and Definitions of Obesity In Childhood and Adolescence: A field guide for the uninitiated". Nutr J 6 (1): 32. PMC 2164947. PMID 17963490. doi:10.1186/1475-2891-6-32. 
  14. NHLBI p.xiv
  15. Gray DS, Fujioka K (1991). "Use of relative weight and Body Mass Index for the determination of adiposity". J Clin Epidemiol 44 (6): 545–50. PMID 2037859. doi:10.1016/0895-4356(91)90218-X. 
  16. 16.0 16.1 Healthy Weight: Assessing Your Weight: BMI: About BMI for Children and Teens. Center for disease control and prevention. Iliwekwa mnamo April 6, 2009.
  17. 17.0 17.1 Flegal KM, Ogden CL, Wei R, Kuczmarski RL, Johnson CL (June 2001). "Prevalence of overweight in US children: comparison of US growth charts from the Centers for Disease Control and Prevention with other reference values for body mass index". Am. J. Clin. Nutr. 73 (6): 1086–93. PMID 11382664. 
  18. 18.0 18.1 Sturm R (July 2007). "Increases in morbid obesity in the USA: 2000–2005". Public Health 121 (7): 492–6. PMC 2864630. PMID 17399752. doi:10.1016/j.puhe.2007.01.006. 
  19. Kanazawa M, Yoshiike N, Osaka T, Numba Y, Zimmet P, Inoue S (December 2002). "Criteria and classification of obesity in Japan and Asia-Oceania". Asia Pac J Clin Nutr. 11 Suppl 8: S732–S737. PMID 12534701. doi:10.1046/j.1440-6047.11.s8.19.x. 
  20. Bei-Fan Z; Cooperative Meta-Analysis Group of Working Group on Obesity in China (December 2002). "Predictive values of body mass index and waist circumference for risk factors of certain related diseases in Chinese adults: study on optimal cut-off points of body mass index and waist circumference in Chinese adults". Asia Pac J Clin Nutr. 11 Suppl 8: S685–93. PMID 12534691. doi:10.1046/j.1440-6047.11.s8.9.x. 
  21. http://www.medicalnewstoday.com/releases/24118.php
  22. 22.0 22.1 Berrington de Gonzalez A (December 2010). "Body-Mass Index and Mortality among 1.46 Million White Adults". N. Engl. J. Med. 363 (23): 2211–9. PMC 3066051. PMID 21121834. doi:10.1056/NEJMoa1000367. 
  23. Mokdad AH, Marks JS, Stroup DF, Gerberding JL (March 2004). "Actual causes of death in the United States, 2000" (PDF). JAMA 291 (10): 1238–45. PMID 15010446. doi:10.1001/jama.291.10.1238. 
  24. 24.0 24.1 Allison DB, Fontaine KR, Manson JE, Stevens J, VanItallie TB (October 1999). "Annual deaths attributable to obesity in the United States". JAMA 282 (16): 1530–8. PMID 10546692. doi:10.1001/jama.282.16.1530. 
  25. 25.0 25.1 25.2 Whitlock G; Lewington S; Sherliker P et al. (March 2009). "Body-mass index and cause-specific mortality in 900 000 adults: collaborative analyses of 57 prospective studies". Lancet 373 (9669): 1083–96. PMC 2662372. PMID 19299006. doi:10.1016/S0140-6736(09)60318-4. 
  26. Calle EE, Thun MJ, Petrelli JM, Rodriguez C, Heath CW (October 1999). "Body-mass index and mortality in a prospective cohort of U.S. adults". N. Engl. J. Med. 341 (15): 1097–105. PMID 10511607. doi:10.1056/NEJM199910073411501. 
  27. Pischon T; Boeing H; Hoffmann K et al. (November 2008). "General and abdominal adiposity and risk of death in Europe". N. Engl. J. Med. 359 (20): 2105–20. PMID 19005195. doi:10.1056/NEJMoa0801891. 
  28. Manson JE; Willett WC; Stampfer MJ et al. (1995). "Body weight and mortality among women". N. Engl. J. Med. 333 (11): 677–85. PMID 7637744. doi:10.1056/NEJM199509143331101. 
  29. 29.0 29.1 Tsigosa Constantine; Hainer, Vojtech; Basdevant, Arnaud; Finer, Nick; Fried, Martin; Mathus-Vliegen, Elisabeth; Micic, Dragan; Maislos, Maximo; Roman, Gabriela (April 2008). "Management of Obesity in Adults: European Clinical Practice Guidelines". The European Journal of Obesity 1 (2): 106–16. PMID 20054170. doi:10.1159/000126822. Archived from the original on 2012-04-26. Retrieved 2013-11-28. 
  30. Fried M; Hainer V; Basdevant A et al. (April 2007). "Inter-disciplinary European guidelines on surgery of severe obesity". Int J Obes (Lond) 31 (4): 569–77. PMID 17325689. doi:10.1038/sj.ijo.0803560. 
  31. Peeters A, Barendregt JJ, Willekens F, Mackenbach JP, Al Mamun A, Bonneux L (January 2003). "Obesity in adulthood and its consequences for life expectancy: A life-table analysis" (PDF). Ann. Intern. Med. 138 (1): 24–32. PMID 12513041. 
  32. Grundy SM (2004). "Obesity, metabolic syndrome, and cardiovascular disease". J. Clin. Endocrinol. Metab. 89 (6): 2595–600. PMID 15181029. doi:10.1210/jc.2004-0372. 
  33. Seidell 2005 p.9
  34. 34.0 34.1 Bray GA (2004). "Medical consequences of obesity". J. Clin. Endocrinol. Metab. 89 (6): 2583–9. PMID 15181027. doi:10.1210/jc.2004-0535. 
  35. Shoelson SE, Herrero L, Naaz A (May 2007). "Obesity, inflammation, and insulin resistance". Gastroenterology 132 (6): 2169–80. PMID 17498510. doi:10.1053/j.gastro.2007.03.059. 
  36. Shoelson SE, Lee J, Goldfine AB (July 2006). "Inflammation and insulin resistance". J. Clin. Invest. 116 (7): 1793–801. PMC 1483173. PMID 16823477. doi:10.1172/JCI29069. 
  37. Dentali F, Squizzato A, Ageno W (July 2009). "The metabolic syndrome as a risk factor for venous and arterial thrombosis". Semin. Thromb. Hemost. 35 (5): 451–7. PMID 19739035. doi:10.1055/s-0029-1234140. 
  38. 38.0 38.1 Schmidt DS, Salahudeen AK (2007). "Obesity-survival paradox-still a controversy?". Semin Dial 20 (6): 486–92. PMID 17991192. doi:10.1111/j.1525-139X.2007.00349.x. 
  39. 39.0 39.1 U.S. Preventive Services Task Force (June 2003). "Behavioral counseling in primary care to promote a healthcite journal y diet: recommendations and rationale". Am Fam Physician 67 (12): 2573–6. PMID 12825847. 
  40. Habbu A, Lakkis NM, Dokainish H (October 2006). "The obesity paradox: Fact or fiction?". Am. J. Cardiol. 98 (7): 944–8. PMID 16996880. doi:10.1016/j.amjcard.2006.04.039. 
  41. Romero-Corral A; Montori VM; Somers VK et al. (2006). "Association of bodyweight with total mortality and with cardiovascular events in coronary artery disease: A systematic review of cohort studies". Lancet 368 (9536): 666–78. PMID 16920472. doi:10.1016/S0140-6736(06)69251-9. 
  42. Oreopoulos A, Padwal R, Kalantar-Zadeh K, Fonarow GC, Norris CM, McAlister FA (July 2008). "Body mass index and mortality in heart failure: A meta-analysis". Am. Heart J. 156 (1): 13–22. PMID 18585492. doi:10.1016/j.ahj.2008.02.014. 
  43. Oreopoulos A, Padwal R, Norris CM, Mullen JC, Pretorius V, Kalantar-Zadeh K (February 2008). "Effect of obesity on short- and long-term mortality postcoronary revascularization: A meta-analysis". Obesity (Silver Spring) 16 (2): 442–50. PMID 18239657. doi:10.1038/oby.2007.36. 
  44. Diercks DB; Roe MT; Mulgund J et al. (July 2006). "The obesity paradox in non-ST-segment elevation acute coronary syndromes: Results from the Can Rapid risk stratification of Unstable angina patients Suppress ADverse outcomes with Early implementation of the American College of Cardiology/American Heart Association Guidelines Quality Improvement Initiative". Am Heart J 152 (1): 140–8. PMID 16824844. doi:10.1016/j.ahj.2005.09.024. 
  45. 45.0 45.1 45.2 45.3 Lau DC, Douketis JD, Morrison KM, Hramiak IM, Sharma AM, Ur E (April 2007). "2006 Canadian clinical practice guidelines on the management and prevention of obesity in adults and children summary". CMAJ 176 (8): S1–13. PMC 1839777. PMID 17420481. doi:10.1503/cmaj.061409. 
  46. Bleich S, Cutler D, Murray C, Adams A (2008). "Why is the developed world obese?". Annu Rev Public Health 29: 273–95. PMID 18173389. doi:10.1146/annurev.publhealth.29.020907.090954. 
  47. Drewnowski A, Specter SE (January 2004). "Poverty and obesity: the role of energy density and energy costs". Am. J. Clin. Nutr. 79 (1): 6–16. PMID 14684391. 
  48. Nestle M, Jacobson MF (2000). "Halting the obesity epidemic: a public health policy approach". Public Health Rep 115 (1): 12–24. PMC 1308552. PMID 10968581. doi:10.1093/phr/115.1.12. 
  49. James WP (March 2008). "The fundamental drivers of the obesity epidemic". Obes Rev 9 (Suppl 1): 6–13. PMID 18307693. doi:10.1111/j.1467-789X.2007.00432.x. 
  50. Keith SW; Redden DT; Katzmarzyk PT et al. (2006). "Putative contributors to the secular increase in obesity: Exploring the roads less traveled". Int J Obes (Lond) 30 (11): 1585–94. PMID 16801930. doi:10.1038/sj.ijo.0803326. 
  51. 51.0 51.1 51.2 51.3 EarthTrends: Nutrition: Calorie supply per capita. World Resources Institute. Iliwekwa mnamo Oct. 18, 2009.
  52. USDA: frsept99b. United States Department of Agriculture. Iliwekwa mnamo January 10, 2009.
  53. Diet composition and obesity among Canadian adults. Statistics Canada.
  54. National Control for Health Statistics. Nutrition For Everyone. Centers for Disease Control and Prevention. Iliwekwa mnamo 2008-07-09.
  55. Marantz PR, Bird ED, Alderman MH (March 2008). "A call for higher standards of evidence for dietary guidelines". Am J Prev Med 34 (3): 234–40. PMID 18312812. doi:10.1016/j.amepre.2007.11.017. 
  56. Flegal KM, Carroll MD, Ogden CL, Johnson CL (October 2002). "Prevalence and trends in obesity among US adults, 1999–2000". JAMA 288 (14): 1723–1727. PMID 12365955. doi:10.1001/jama.288.14.1723. 
  57. Wright JD, Kennedy-Stephenson J, Wang CY, McDowell MA, Johnson CL (February 2004). "Trends in intake of energy and macronutrients—United States, 1971–2000". MMWR Morb Mortal Wkly Rep 53 (4): 80–2. PMID 14762332. 
  58. 58.0 58.1 58.2 58.3 58.4 58.5 Caballero B (2007). "The global epidemic of obesity: An overview". Epidemiol Rev 29: 1–5. PMID 17569676. doi:10.1093/epirev/mxm012. 
  59. Mozaffarian, D; Hao, T, Rimm, EB, Willett, WC, Hu, FB (2011 Jun 23). "Changes in Diet and Lifestyle and Long-Term Weight Gain in Women and Men". The New England Journal of Medicine 364 (25): 2392–404. PMC 3151731. PMID 21696306. doi:10.1056/NEJMoa1014296.  Check date values in: |date= (help)
  60. Malik VS, Schulze MB, Hu FB (August 2006). "Intake of sugar-sweetened beverages and weight gain: a systematic review work=Statistics Canada" 84 (2). pp. 274–88. PMC 3210834. PMID 16895873.  Text " J. Clin. Nutr. " ignored (help);
  61. Olsen NJ, Heitmann BL (January 2009). "Intake of calorically sweetened beverages and obesity". Obes Rev 10 (1): 68–75. PMID 18764885. doi:10.1111/j.1467-789X.2008.00523.x. 
  62. Rosenheck R (November 2008). "Fast food consumption and increased caloric intake: a systematic review of a trajectory towards weight gain and obesity risk". Obes Rev 9 (6): 535–47. PMID 18346099. doi:10.1111/j.1467-789X.2008.00477.x. 
  63. Lin BH, Guthrie J and Frazao E (1999). "Nutrient contribution of food away from home". In Frazão E. Agriculture Information Bulletin No. 750: America's Eating Habits: Changes and Consequences. Washington, DC: US Department of Agriculture, Economic Research Service. pp. 213–239. Archived from the original on 2002-06-11. Retrieved 2013-11-28. 
  64. Pollan, Michael. "You Are What You Grow", New York Times, 22 April 2007. Retrieved on 2007-07-30. 
  65. Kopelman and Caterson 2005:324.
  66. You must specify title = and url = when using {{cite web}}. (registration required). John Schieszer. The Medical Post.
  67. Seidell 2005 p.10
  68. 68.0 68.1 WHO: Obesity and overweight. World Health Organization. Jalada kutoka ya awali juu ya 2008-12-18. Iliwekwa mnamo January 10, 2009.
  69. 69.0 69.1 69.2 WHO | Physical Inactivity: A Global Public Health Problem. World Health Organization. Iliwekwa mnamo February 22, 2009.
  70. 70.0 70.1 Ness-Abramof R, Apovian CM (February 2006). "Diet modification for treatment and prevention of obesity". Endocrine 29 (1): 5–9. PMID 16622287. doi:10.1385/ENDO:29:1:135. 
  71. Salmon J, Timperio A (2007). "Prevalence, trends and environmental influences on child and youthphysical activity". Med Sport Sci. Medicine and Sport Science 50: 183–99. ISBN 978-3-318-01396-2. PMID 17387258. doi:10.1159/000101391. 
  72. Borodulin K, Laatikainen T, Juolevi A, Jousilahti P (June 2008). "Thirty-year trends of physical activity in relation to age, calendar time and birth cohort in Finnish adults". Eur J Public Health 18 (3): 339–44. PMID 17875578. doi:10.1093/eurpub/ckm092. 
  73. Brownson RC, Boehmer TK, Luke DA (2005). "Declining rates of physical activity in the United States: what are the contributors?". Annu Rev Public Health 26: 421–43. PMID 15760296. doi:10.1146/annurev.publhealth.26.021304.144437. 
  74. Gortmaker SL, Must A, Sobol AM, Peterson K, Colditz GA, Dietz WH (April 1996). "Television viewing as a cause of increasing obesity among children in the United States, 1986–1990". Arch Pediatr Adolesc Med 150 (4): 356–62. PMID 8634729. doi:10.1001/archpedi.1996.02170290022003. 
  75. Vioque J, Torres A, Quiles J (December 2000). "Time spent watching television, sleep duration and obesity in adults living in Valencia, Spain". Int. J. Obes. Relat. Metab. Disord. 24 (12): 1683–8. PMID 11126224. doi:10.1038/sj.ijo.0801434. 
  76. Tucker LA, Bagwell M (July 1991). "Television viewing and obesity in adult females" (PDF). Am J Public Health 81 (7): 908–11. PMC 1405200. PMID 2053671. doi:10.2105/AJPH.81.7.908. 
  77. Mary Jones. Case Study: Cataplexy and SOREMPs Without Excessive Daytime Sleepiness in Prader Willi Syndrome. Is This the Beginning of Narcolepsy in a Five Year Old?. European Society of Sleep Technologists. Iliwekwa mnamo April 6, 2009.
  78. Poirier P; Giles TD; Bray GA et al. (May 2006). "Obesity and cardiovascular disease: pathophysiology, evaluation, and effect of weight loss". Arterioscler. Thromb. Vasc. Biol. 26 (5): 968–76. PMID 16627822. doi:10.1161/01.ATV.0000216787.85457.f3. 
  79. Loos RJ, Bouchard C (May 2008). "FTO: the first gene contributing to common forms of human obesity". Obes Rev 9 (3): 246–50. PMID 18373508. doi:10.1111/j.1467-789X.2008.00481.x. 
  80. Yang W, Kelly T, He J (2007). "Genetic epidemiology of obesity". Epidemiol Rev 29: 49–61. PMID 17566051. doi:10.1093/epirev/mxm004. 
  81. Walley AJ, Asher JE, Froguel P (June 2009). "The genetic contribution to non-syndromic human obesity". Nat. Rev. Genet. 10 (7): 431–42. PMID 19506576. doi:10.1038/nrg2594. 
  82. Farooqi S, O'Rahilly S (December 2006). "Genetics of obesity in humans". Endocr. Rev. 27 (7): 710–18. PMID 17122358. doi:10.1210/er.2006-0040. Archived from the original on 2010-07-10. Retrieved 2013-11-28. 
  83. Kolata,Gina (2007). Rethinking thin: The new science of weight loss – and the myths and realities of dieting. Picador. p. 122. ISBN 0-312-42785-9. 
  84. Chakravarthy MV, Booth FW (2004). "Eating, exercise, and "thrifty" genotypes: Connecting the dots toward an evolutionary understanding of modern chronic diseases". J. Appl. Physiol. 96 (1): 3–10. PMID 14660491. doi:10.1152/japplphysiol.00757.2003. 
  85. doi:10.1038/ijo.2009.175
    This citation will be automatically completed in the next few minutes. You can jump the queue or expand by hand
  86. doi:10.1002/ajhb.21100
    This citation will be automatically completed in the next few minutes. You can jump the queue or expand by hand
  87. Rosén T, Bosaeus I, Tölli J, Lindstedt G, Bengtsson BA (1993). "Increased body fat mass and decreased extracellular fluid volume in adults with growth hormone deficiency". Clin. Endocrinol. (Oxf) 38 (1): 63–71. PMID 8435887. doi:10.1111/j.1365-2265.1993.tb00974.x. 
  88. Zametkin AJ, Zoon CK, Klein HW, Munson S (February 2004). "Psychiatric aspects of child and adolescent obesity: a review of the past 10 years". J Am Acad Child Adolesc Psychiatry 43 (2): 134–50. PMID 14726719. doi:10.1097/00004583-200402000-00008. 
  89. Chiles C, van Wattum PJ (2010). "Psychiatric aspects of the obesity crisis". Psychiatr Times 27 (4): 47–51. 
  90. Yach D, Stuckler D, Brownell KD (January 2006). "Epidemiologic and economic consequences of the global epidemics of obesity and diabetes". Nat. Med. 12 (1): 62–6. PMID 16397571. doi:10.1038/nm0106-62. 
  91. Sobal J, Stunkard AJ (March 1989). "Socioeconomic status and obesity: A review of the literature". Psychol Bull 105 (2): 260–75. PMID 2648443. doi:10.1037/0033-2909.105.2.260. 
  92. 92.0 92.1 McLaren L (2007). "Socioeconomic status and obesity". Epidemiol Rev 29: 29–48. PMID 17478442. doi:10.1093/epirev/mxm001. 
  93. 93.0 93.1 Wilkinson, Richard; Pickett, Kate (2009). [[The Spirit Level: Why More Equal Societies Almost Always Do Better]]. London: Allen Lane. pp. 91–101. ISBN 978-1-84614-039-6.  Wikilink embedded in URL title (help)
  94. Christakis NA, Fowler JH (2007). "The Spread of Obesity in a Large Social Network over 32 Years". New England Journal of Medicine 357 (4): 370–379. PMID 17652652. doi:10.1056/NEJMsa066082. 
  95. Bjornstop P (2001). "Do stress reactions cause abdominal obesity and comorbidities?". Obesity Reviews 2 (2): 73–86. PMID 12119665. doi:10.1046/j.1467-789x.2001.00027.x. 
  96. Goodman E, Adler NE, Daniels SR, Morrison JA, Slap GB, Dolan LM (2003). "Impact of objective and subjective social status on obesity in a biracial cohort of adolescents". Obesity Reviews 11 (8): 1018–26. PMID 12917508. doi:10.1038/oby.2003.140. 
  97. Flegal KM, Troiano RP, Pamuk ER, Kuczmarski RJ, Campbell SM (November 1995). "The influence of smoking cessation on the prevalence of overweight in the United States". N. Engl. J. Med. 333 (18): 1165–70. PMID 7565970. doi:10.1056/NEJM199511023331801. 
  98. Chiolero A, Faeh D, Paccaud F, Cornuz J (1 April 2008). "Consequences of smoking for body weight, body fat distribution, and insulin resistance". Am. J. Clin. Nutr. 87 (4): 801–9. PMID 18400700. 
  99. Weng HH, Bastian LA, Taylor DH, Moser BK, Ostbye T (2004). "Number of children associated with obesity in middle-aged women and men: results from the health and retirement study". J Women's Health (Larchmt) 13 (1): 85–91. PMID 15006281. doi:10.1089/154099904322836492. 
  100. Bellows-Riecken KH, Rhodes RE (February 2008). "A birth of inactivity? A review of physical activity and parenthood". Prev Med 46 (2): 99–110. PMID 17919713. doi:10.1016/j.ypmed.2007.08.003. 
  101. Obesity and Overweight (PDF). World Health Organization. Iliwekwa mnamo February 22, 2009.
  102. 102.0 102.1 Caballero B (March 2001). "Introduction. Symposium: Obesity in developing countries: biological and ecological factors". J. Nutr. 131 (3): 866S–870S. PMID 11238776. 
  103. <Please add first missing authors to populate metadata.>. doi:10.1111/j.1467-789X.2011.00920.x (inactive 1-1-2012) http://onlinelibrary.wiley.com/doi/10.1111/j.1467-789X.2011.00920.x/abstract.  Check date values in: |doi_brokendate= (help); Missing or empty |title= (help)
  104. DiBaise JK, Zhang H, Crowell MD, Krajmalnik-Brown R, Decker GA, Rittmann BE (April 2008). "Gut microbiota and its possible relationship with obesity". Mayo Clinic proceedings. Mayo Clinic 83 (4): 460–9. PMID 18380992. doi:10.4065/83.4.460. 
  105. Falagas ME, Kompoti M (July 2006). "Obesity and infection". Lancet Infect Dis 6 (7): 438–46. PMID 16790384. doi:10.1016/S1473-3099(06)70523-0. 
  106. 106.0 106.1 106.2 106.3 106.4 Flier JS (2004). "Obesity wars: Molecular progress confronts an expanding epidemic Molecular progress confronts an expanding epidemic". Cell 116 (2): 337–50. PMID 14744442. doi:10.1016/S0092-8674(03)01081-X. 
  107. Hamann A, Matthaei S (1996). "Regulation of energy balance by leptin". Exp. Clin. Endocrinol. Diabetes 104 (4): 293–300. PMID 8886745. doi:10.1055/s-0029-1211457. 
  108. Boulpaep, Emile L.; Boron, Walter F. (2003). Medical physiologya: A cellular and molecular approach. Philadelphia: Saunders. p. 1227. ISBN 0-7216-3256-4. 
  109. Loscalzo, Joseph; Fauci, Anthony S.; Braunwald, Eugene; Dennis L. Kasper; Hauser, Stephen L; Longo, Dan L. (2008). Harrison's principles of internal medicine. McGraw-Hill Medical. ISBN 0-07-146633-9. 
  110. Satcher D (2001). The Surgeon General's Call to Action to Prevent and Decrease Overweight and Obesity. U.S. Dept. of Health and Human Services, Public Health Service, Office of Surgeon General. ISBN 978-0-16-051005-2. 
  111. Brook Barnes. "Limiting Ads of Junk Food to Children", New York Times, 2007-07-18. Retrieved on 2008-07-24. 
  112. Fewer Sugary Drinks Key to Weight Loss -healthfinder.gov. U.S.. Department of Health and Human Services. Jalada kutoka ya awali juu ya 2012-11-16. Iliwekwa mnamo Oct 18,2009.
  113. Brennan Ramirez LK; Hoehner CM; Brownson RC et al. (December 2006). "Indicators of activity-friendly communities: An evidence-based consensus process". Am J Prev Med 31 (6): 530–32. PMID 17169714. doi:10.1016/j.amepre.2006.07.026. 
  114. National Heart, Lung, and Blood Institute (1998). Clinical Guidelines on the Identification, Evaluation, and Treatment of Overweight and Obesity in Adults (PDF). International Medical Publishing, Inc. ISBN 1-58808-002-1. 
  115. Lau DC, Douketis JD, Morrison KM, Hramiak IM, Sharma AM, Ur E (April 2007). "2006 Canadian clinical practice guidelines on the management and prevention of obesity in adults and children summary". CMAJ 176 (8): S1–13. PMC 1839777. PMID 17420481. doi:10.1503/cmaj.061409. 
  116. Storing up problems; the medical case for a slimmer nation. London: Royal College of Physicians. 2004-02-11. ISBN 1-86016-200-2. 
  117. Great Britain Parliament House of Commons Health Committee (May 2004). Obesity– Volume 1 – HCP 23-I, Third Report of session 2003–04. Report, together with formal minutes. London, UK: TSO (The Stationery Office). ISBN 978-0-215-01737-6. Retrieved 2007-12-17. 
  118. Obesity: guidance on the prevention, identification, assessment and management of overweight and obesity in adults and children (PDF). National Institute for Health and Clinical Excellence(NICE). National Health Services (NHS) (2006). Iliwekwa mnamo April 8, 2009.
  119. Wanless, Sir Derek; John Appleby, Anthony Harrison, Darshan Patel (2007). Our Future Health Secured? A review of NHS funding and performance. London, UK: The King's Fund. ISBN 1-85717-562-X. Retrieved 2007-12-17. 
  120. Sacks G, Swinburn B, Lawrence M (January 2009). "Obesity Policy Action framework and analysis grids for a comprehensive policy approach to reducing obesity". Obes Rev 10 (1): 76–86. PMID 18761640. doi:10.1111/j.1467-789X.2008.00524.x. 
  121. Strychar I (January 2006). "Diet in the management of weight loss". CMAJ 174 (1): 56–63. PMC 1319349. PMID 16389240. doi:10.1503/cmaj.045037. 
  122. Shick SM, Wing RR, Klem ML, McGuire MT, Hill JO, Seagle H (April 1998). "Persons successful at long-term weight loss and maintenance continue to consume a low-energy, low-fat diet". J Am Diet Assoc 98 (4): 408–13. PMID 9550162. doi:10.1016/S0002-8223(98)00093-5. 
  123. Tate DF, Jeffery RW, Sherwood NE, Wing RR (1 April 2007). "Long-term weight losses associated with prescription of higher physical activity goals. Are higher levels of physical activity protective against weight regain?". Am. J. Clin. Nutr. 85 (4): 954–9. PMID 17413092. 
  124. Wing, Rena R; Phelan, Suzanne (1 July 2005). "Science-Based Solutions to Obesity: What are the Roles of Academia, Government, Industry, and Health Care? Proceedings of a symposium, Boston, Massachusetts, USA, 10–11 March 2004 and Anaheim, California, USA, 2 October 2004". Am. J. Clin. Nutr. 82 (1 Suppl): 207S–273S. PMID 16002825. 
  125. Thangaratinam, S; Rogozinska, E; Jolly, K; Glinkowski, S; Roseboom, T; Tomlinson, JW; Kunz, R; Mol, BW; Coomarasamy, A; Khan, KS (2012 May 16). "Effects of interventions in pregnancy on maternal weight and obstetric outcomes: meta-analysis of randomised evidence". BMJ (Clinical research ed.) 344: e2088. PMC 3355191. PMID 22596383. doi:10.1136/bmj.e2088.  Check date values in: |date= (help)
  126. 126.0 126.1 Rucker D, Padwal R, Li SK, Curioni C, Lau DC (2007). "Long term pharmacotherapy for obesity and overweight: updated meta-analysis". BMJ 335 (7631): 1194–99. PMC 2128668. PMID 18006966. doi:10.1136/bmj.39385.413113.25. 
  127. Wood, Shelley. Diet Drug Orlistat Linked to Kidney, Pancreas Injuries. Medscape. Medscape News. Iliwekwa mnamo 26 April 2011.
  128. Bays, HE (2011 Mar). "Lorcaserin: drug profile and illustrative model of the regulatory challenges of weight-loss drug development". Expert review of cardiovascular therapy 9 (3): 265–77. PMID 21438803. doi:10.1586/erc.10.22.  Check date values in: |date= (help)
  129. Bays HE, Gadde KM (December 2011). "Phentermine/topiramate for weight reduction and treatment of adverse metabolic consequences in obesity". Drugs Today 47 (12): 903–14. PMID 22348915. doi:10.1358/dot.2011.47.12.1718738. 
  130. Sjöström L; Narbro K; Sjöström CD et al. (August 2007). "Effects of bariatric surgery on mortality in Swedish obese subjects". N. Engl. J. Med. 357 (8): 741–52. PMID 17715408. doi:10.1056/NEJMoa066254. 
  131. Global Prevalence of Adult Obesity (PDF). International Obesity Taskforce. Iliwekwa mnamo January 29, 2008.
  132. 132.0 132.1 Haslam D (March 2007). "Obesity: a medical history". Obes Rev. 8 Suppl 1: 31–6. PMID 17316298. doi:10.1111/j.1467-789X.2007.00314.x. 
  133. 133.0 133.1 Obesity and overweight. World Health Organization. Iliwekwa mnamo April 8, 2009.
  134. Seidell 2005 p.5
  135. Howard, Natasha J.; Taylor, A; Gill, T; Chittleborough, C (March 2008). "Severe obesity: Investigating the socio-demographics within the extremes of body mass index". Obesity Research &Clinical Practice 2 (1): 51–59. doi:10.1016/j.orcp.2008.01.001. 
  136. Tjepkema M (2005-07-06). "Measured Obesity–Adult obesity in Canada: Measured height and weight". Nutrition: Findings from the Canadian Community Health Survey. Ottawa, Ontario: Statistics Canada. 
  137. 137.0 137.1 Zachary Bloomgarden (2003). "Prevention of Obesity and Diabetes". Diabetes Care 26 (11): 3172–3178. PMID 14578257. doi:10.2337/diacare.26.11.3172. 
  138. 138.0 138.1 History of Medicine: Sushruta – the Clinician –Teacher par Excellence (PDF). Dwivedi, Girish & Dwivedi, Shridhar (2007). Jalada kutoka ya awali juu ya 2008-10-10. Iliwekwa mnamo 2008-09-19.
  139. Theodore Mazzone; Giamila Fantuzzi (2006). Adipose Tissue And Adipokines in Health And Disease (Nutrition and Health). Totowa, NJ: Humana Press. p. 222. ISBN 1-58829-721-7. 
  140. Keller p. 49
  141. Breslow L (September 1952). "Public Health Aspects of Weight Control". Am J Public Health Nations Health 42 (9): 1116–20. PMC 1526346. PMID 12976585. doi:10.2105/AJPH.42.9.1116. 
  142. 142.0 142.1 Puhl R, Brownell KD (December 2001). "Bias, discrimination, and obesity". Obes. Res. 9 (12): 788–805. PMID 11743063. doi:10.1038/oby.2001.108. 
  143. Rubinstein S, Caballero B (2000). "Is Miss America an undernourished role model?". JAMA 283 (12): 1569. PMID 10735392. doi:10.1001/jama.283.12.1569. 
  144. 144.0 144.1 Johnson F, Cooke L, Croker H, Wardle J (2008). "Changing perceptions of weight in Great Britain: comparison of two population surveys". BMJ 337: a494. PMC 2500200. PMID 18617488. doi:10.1136/bmj.a494. 
  145. Fumento, Michael (1997). The Fat of the Land: Our Health Crisis and How Overweight Americans Can Help Themselves. Penguin (Non-Classics). p. 126. ISBN 0-14-026144-3. 
  146. 146.0 146.1 Puhl R., Henderson K., and Brownell K. 2005 p.29
  147. Johansson E, Bockerman P, Kiiskinen U, Heliovaara M (2009). "Obesity and labour market success in Finland: The difference between having a high BMI and being fat". Economics and Human Biology 7 (1): 36–45. PMID 19249259. doi:10.1016/j.ehb.2009.01.008. 
  148. Cawley, J; John Cawley, Chad Meyerhoefer (January 2012). "The medical care costs of obesity: An instrumental variables approach". Journal of Health Economics 31 (1): 219–230. PMID 22094013. doi:10.1016/j.jhealeco.2011.10.003. Retrieved 2 August 2012. 
  149. Finkelstein EA, Fiebelkorn IA, Wang G (1 January 2003). "National medical spending attributable to overweight and obesity: How much, and who's paying". Health Affairs. Online (May). 
  150. Obesity and overweight: Economic consequences. Centers for Disease Control and Prevention (22 May 2007). Iliwekwa mnamo 2007-09-05.
  151. Colagiuri, Stephen; Lee, Crystal M. Y.; Colagiuri, Ruth; <Please add first missing authors to populate metadata.> (2009). "The cost of overweight and obesity in Australia". The Medical Journal of Australia. Retrieved 2011-06-18.  Missing |last4= in Authors list (help)
  152. Cummings, Laura. "The diet business: Banking on failure", BBC News, 5 February 2003. Retrieved on 25 February 2009. 
  153. van Baal PH; Polder JJ; de Wit GA et al. (February 2008). "Lifetime Medical Costs of Obesity: Prevention No Cure for Increasing Health Expenditure". PLoS Med. 5 (2): e29. PMC 2225430. PMID 18254654. doi:10.1371/journal.pmed.0050029. 
  154. Bakewell J (2007). "Bariatric furniture: Considerations for use". Int J Ther Rehabil 14 (7): 329–33. Archived from the original on 2011-10-08. Retrieved 2013-11-28. 
  155. Neovius K, Johansson K, Kark M, Neovius M (January 2009). "Obesity status and sick leave: a systematic review". Obes Rev 10 (1): 17–27. PMID 18778315. doi:10.1111/j.1467-789X.2008.00521.x. 
  156. Ostbye T, Dement JM, Krause KM (2007). "Obesity and workers' compensation: Results from the Duke Health and Safety Surveillance System". Arch. Intern. Med. 167 (8): 766–73. PMID 17452538. doi:10.1001/archinte.167.8.766. 
  157. Alabama "Obesity Penalty" Stirs Debate. Don Fernandez. Iliwekwa mnamo April 5, 2009.
  158. Puhl R., Henderson K., and Brownell K. 2005 p.30
  159. Lisa DiCarlo (2002-10-24). Why Airlines Can't Cut The Fat. Forbes.com. Iliwekwa mnamo 2008-07-23.
  160. Dannenberg AL, Burton DC, Jackson RJ (2004). "Economic and environmental costs of obesity: The impact on airlines". American journal of preventive medicine 27 (3): 264. PMID 15450642. doi:10.1016/j.amepre.2004.06.004. 
  161. Lauren Cox (July 2, 2009). Who Should Pay for Obese Health Care?. ABC News. Iliwekwa mnamo 2012-08-06.
  162. 162.0 162.1 109th U.S. Congress (2005–2006) H.R. 554: 109th U.S. Congress (2005–2006) H.R. 554: Personal Responsibility in Food Consumption Act of 2005. GovTrack.us. Jalada kutoka ya awali juu ya 2008-11-01. Iliwekwa mnamo 2008-07-24.
  163. What is NAAFA. National Association to Advance Fat Acceptance. Jalada kutoka ya awali juu ya 2009-03-12. Iliwekwa mnamo February 17, 2009.
  164. ISAA Mission Statement. International Size Acceptance Association. Iliwekwa mnamo February 17, 2009.
  165. 165.0 165.1 Pulver, Adam (2007). An Imperfect Fit: Obesity, Public Health, and Disability Anti-Discrimination Law. Social Science Electronic Publishing. Retrieved January 13, 2009. 
  166. Neumark-Sztainer D (March 1999). "The weight dilemma: a range of philosophical perspectives". Int. J. Obes. Relat. Metab. Disord. 23 Suppl 2: S31–7. PMID 10340803. doi:10.1038/sj.ijo.0800857. 
  167. National Association to Advance Fat Acceptance (2008), We come in all sizes, NAAFA, http://www.naafaonline.com/dev2/, retrieved 2008-07-29
  168. Big Trouble | Bitch Magazine Archived 26 Desemba 2012 at the Wayback Machine., bitchmagazine.org
  169. International Size Acceptance Association – ISAA. International Size Acceptance Association. Iliwekwa mnamo January 13, 2009.
  170. 170.0 170.1 Flynn MA; McNeil DA; Maloff B et al. (February 2006). "Reducing obesity and related chronic disease risk in children and youth: a synthesis of evidence with 'best practice' recommendations". Obes Rev. 7 Suppl 1: 7–66. PMID 16371076. doi:10.1111/j.1467-789X.2006.00242.x. 
  171. Dollman J, Norton K, Norton L (December 2005). "Evidence for secular trends in children's physical activity behaviour". Br J Sports Med 39 (12): 892–7; discussion 897. PMC 1725088. PMID 16306494. doi:10.1136/bjsm.2004.016675. 
  172. Metcalf, B.; Henley, W.; Wilkin, T. (27 September 2012). "Effectiveness of intervention on physical activity of children: systematic review and meta-analysis of controlled trials with objectively measured outcomes (EarlyBird 54)". BMJ 345 (sep27 1): e5888–e5888. doi:10.1136/bmj.e5888. 
  173. 173.0 173.1 Lund Elizabeth M. (2006). "Prevalence and Risk Factors for Obesity in Adult Dogs from Private US Veterinary Practices". Intern J Appl Res Vet Med 4 (2): 177–86. 
  174. McGreevy PD, Thomson PC, Pride C, Fawcett A, Grassi T, Jones B (May 2005). "Prevalence of obesity in dogs examined by Australian veterinary practices and the risk factors involved". Vet. Rec. 156 (22): 695–702. PMID 15923551. 
  175. Nijland ML, Stam F, Seidell JC (June 2009). "Overweight in dogs, but not in cats, is related to overweight in their owners". Public Health Nutr 13 (1): 1–5. PMID 19545467. doi:10.1017/S136898000999022X. 

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

Marejeo mengine[hariri | hariri chanzo]

Viungo vya nje[hariri | hariri chanzo]

Wikimedia Commons ina media kuhusu: