Uchaguzi wa Rais wa Marekani, 1932

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Uchaguzi wa Rais wa Marekani, mwaka wa 1932 ulikuwa wa 37 katika historia ya Marekani. Ukafanywa Jumanne tarehe 8 Novemba. Upande wa "Democratic Party", mgombea Franklin D. Roosevelt (pamoja na kaimu wake John Nance Garner) alimshinda mgombea wa "Republican Party" Rais Herbert Hoover (pamoja na kaimu wake Charles Curtis).

Matokeo[hariri | hariri chanzo]

Roosevelt akapata kura 472 na Hoover 59. Ramani yaonyesha kura kwa kila jimbo.