Orlando Owoh

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Orlando Owoh (14 Februari 1932 - 4 Novemba 2008)[1] ni mwanamuziki na kiongozi wa bendi nchini Nigeria.

Wasifu[hariri | hariri chanzo]

Alizaliwa kwa jina la Stephen Oladipupo Olaore Owomoyela katika eneo la Osogbo, Nigeria mnamo 14 Februari 1932 mama yake alikuwa akitokea Owo. Baadaye alifahamika kwa mashabiki wake kama Chief Dr. Orlando Owoh. Akiwa kijana Owoh alianza biashara ya useremala mwaka 1958, alipoajiriwa na Kundi la Maonyesho la Kola Ogunmola nchini Nigeria kwaajili ya kucheza ngoma na kuimba. Dr. Orlando Owoh na bendi yake ya Omimah mnamo mwaka 1960. Zaidi ya miaka arobaini alikuwa mmoja wa watetezi wa muziki wa highlife. Akiwa na bendi kama vile Omimah Band na baadaye Young Kenneries na African Kenneries International, Owoh bado alikuwa maarufu nchini Nigeria na hata ladha yake ilihamia katika mitindo mipya ya jùjú na fuji. [2]Alikuwa na zaidi ya albamu 45 za Studio yake. Orlando Owoh alikufa tarehe 4 Novemba 2008 na alizikwa katika makao yake makuu mjini Lagos, Nigeria.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. "Orlando Owoh: A decade after". TheCable. 22 November 2018. Iliwekwa mnamo 2 October 2021.  Check date values in: |date=, |accessdate= (help)
  2. Colin Larkin (mhariri). The Guinness Encyclopedia of Popular Music. 
Makala hii kuhusu mwanamuziki fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Orlando Owoh kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.