Mto Umfolozi

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mto Msunduzi unaonekana upande wa kushoto (kusini), Umfolozi katikati, na mifereji ya maji tangu kutelekezwa, na mto wa Mtakatifu Lucia kulia (kaskazini).

Mto Umfolozi unapatikana katika jimbo la KwaZulu-Natal, Afrika Kusini. Mto huu unafahamika pia kama Imfolozi au Mfolozi. ImFolozi ni jina lenye asili ya Kizulu na linafafanua mwonekano wa mto ulivyo: hujipinda ukifuatiwa na vijito vyake.[1]

Mto huu hutiririsha maji yake kuelekea bahari ya Hindi upande wa mashariki. Asili ya kujipinda kwa mto huu huanzia maeneo tambarare ya monzi kisha hujigawanya katika mifereji mingi yenye tabia ya kutiririsha maji taratibu na kuchangia upatikanaji wa aina mbalimbali za viumbehai katika eneo hilo.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. du Plessis, E.J. (1973). Suid-Afrikaanse berg- en riviername. Tafelberg-uitgewers, Cape Town. uk. 273. ISBN 0-624-00273-X. 
Makala hii kuhusu maeneo ya Afrika Kusini bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Mto Umfolozi kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.