Mnavu

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mnavu
(Solanum nigrum)
Mnavu
Mnavu
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Plantae (Mimea)
(bila tabaka): Angiospermae (Mimea inayotoa maua)
(bila tabaka): Eudicots (Mimea ambayo mche wao una majani mawili)
(bila tabaka): Asterids (Mimea kama alizeti)
Oda: Solanales (Mimea kama mnavu)
Familia: Solanaceae (Mimea iliyo na mnasaba na mnavu)
Jenasi: Solanum
Spishi: S. nigrum
L.

Mnavu au mnafu (Solanum nigrum) ni mmea katika familia Solanaceae. Kwa kawaida huu ni mmea wa pori, lakini unapandwa mahali pengi katika Afrika ya Mashariki. Mingi ya mimea ya pori ina sumu, matunda mabichi hasa. Kula kwa beri bichi na mara nyingi majani pia kunaweza kusababisha kifo cha watoto na mifugo. Lakini aina za mnavu zinazopandwa zinaweza kuliwa baada ya kuzipika. Majani huuzwa kwa jina la manavu. Matunda mabivu yanaweza kuliwa kwa kawaida bila kupikwa, aina zenye matunda mekundu au yenye rangi ya machungwa hasa (rangi ya kawaida ni nyeusi).

Kuna spishi nyingine, Solanum americanum, ambayo imewasilishwa katika Afrika na ambayo inafanana sana na S. nigrum. Watu wengi hawawezi kulinganua spishi hizi na mbili zote huitwa mnavu. Hata S. americanum hulika.

Picha[hariri | hariri chanzo]

Makala hii kuhusu mmea fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mnavu kama uainishaji wake wa kibiolojia, uenezi au matumizi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.