Mbale, Uganda

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Mbale)
Mahali pa Mbale katika Uganda.

Mbale ni mji wa Uganda ya kusini-mashariki mwenye wakazi 76,000 chini ya mlima Elgon. Ni makao makuu ya wilaya ya Mbale. Umbali na Jinja ni 120 km na 190 km na Kampala.

Uchumi[hariri | hariri chanzo]

Mazingira ya Mbale kuna kahawa nyingi na pia kilimo cha mazao mengine. Hivyo uchumi wa mji umetegemea kilimo na biashara ya mazao. Kuna pia kiwanda cha maziwa.

Utamaduni[hariri | hariri chanzo]

Eneo la Mbale ni nyumbani kwa Wagishu hasa. Chuo Kikuu cha Kiislamu cha Uganda kipo mjini.

Picha kadhaa za filamu "Casino Royale" zilipigwa Mbale.