Mango

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Mango (wakati mwingine pia: yabisi[1]) ni moja kati ya hali maada. Maana yake ni imara, tofauti na kiowevu (majimaji) au gesi (kama hewa).

Katika hali mango atomu zinakaa mahali pamoja katika gimba, hazichezi wala kusogea ndani yake. Kila atomu ina mahali pake. Gimba mango lina umbo, mjao na uzani maalumu. Umbo mango lina urefu, upana na kimo chake, tofauti na kiowevu kinachobadilika umbo kufuatana na chombo chake au gesi isiyo na umbo wala mjao maalumu.

Kama mango inabadilika kuwa kiowevu tunasema inayeyuka. Kama inabadilika kuwa gesi au mvuke moja kwa moja tunaliita badiliko hili mvukemango.

Maana ya asili ya "mango" ni jiwe gumu jeusi lililotumika kutwanga kumetesha au kukatua kitu. [2]

Atomi katika hali maada mbalimbali[hariri | hariri chanzo]

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. "Mango" ni matumizi jinsi yalivyopendekezwa zaidi katika kamusi za TUKI; pia vitabu vipya vya shule za sekondari Tanzania zinavyoandaliwa kwa Kiswahili, kama vile "Jifunze Fizikia", iliyotolewa na Taasisi ya Taaluma ya Kiswahili, 2015. "Yabisi" inataja zaidi hali ya ugumu kutokana na kukauka. Linganisha Madan, Swahili-English dictionary, Oxford 1903. uk. 433: "Yabisi, a. and Yabis, dry, hard, solid, e. g. udongo yabisi, hard, parched earth. Baridi yabis, rheumatism.Sometimes also as v., be hard, dry, with Nt. yabisika, in same sense, and Cs. yabisi-sha, shwa, make hard, (Ar. Cf. syn. -gtimti, -shupafu.)"
  2. linganisha Madan, Swahili-English dictionary, Oxford 1903. uk. 207 "Mango, n. a hard, black, rounded stone used for pounding, smoothing, and polishing."
Makala hii kuhusu mambo ya fizikia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mango kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.