Mjao

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Mjao (kwa Kiingereza volume) unaeleza ukubwa wa gimba la hisabati (mchemraba, tufe, mcheduara) kwa kupima nafasi ya yaliyomo yake.

Hupimwa katika vizio vya ujazo kama mita ujazo (m³) au sentimita ujazo (cm³).

Kila gimba lenye urefu, upana na kimo huwa na mjao.

Alama yake ni V.

Hali halisi ni kwamba nje ya hisabati kuna njia mbili za kuangalia mjao wa gimba:

  • ujazo wa nje kwa jumla (kwa mfano kama kitu kinazamwa katika kiowevu kinasukuma kiasi gani cha kiowevu hiki?)
  • ujazo wa ndani (kwa mfano yaliyomo ya boksi au tangi)

Mifano ya kukadiria mjao wa magimba kadhaa[hariri | hariri chanzo]

Kadirio ya mjao ni Urefu x Upana x Kimo.

mchemraba mwenye urefu wa ukingo "a":

mchemstatili mwenye urefu wa kingo "a", "b" na "c":

tufe lenye rediasi "r"::

mcheduara au mche mwenye eneo la kitako "A" na kimo "h":

Makala hii kuhusu mambo ya sayansi bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mjao kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.