Majadiliano:Chuo cha Mt. Petro, Auckland

Yaliyomo ya ukurasa hayatumiki katika lugha nyingine.
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Ninamashaka na kipengele hiki hapa:

Anwani: 23 Mountain Rd, Epsom, Auckland 3 Simu: +64 9 524 8108 Kipepesi: +64 9 524 9459

Barua pepe: admin@st-peters.school.nz

Mkuu: K.F. Fouhy

Swali: Je, huu ni mfumo wa sera za uhandishi wa kamusi elezo? Yaani, kutaja anwani ya barua pepe,sanduku la posta, na namba ya simu. Sidhani kama hili liko sawa. Ninapendekeza kipengele hicho kifutwe. Au wenzangu mnaonaje?--Muddyb MwanaharakatiLonga 13:08, 8 Oktoba 2009 (UTC)[jibu]

Ahsante, Bw Muddyb! Swali zuri machoni mwangu. Ukiangalia makala kwenye wikipedia ya Kiingereza lakini utaona kwamba kuna kigezo kinachotoa anwani na hata tovuti mtandaoni kwa kila chuo. Ndiyo sababu ningeshauri tuache hivi. Wasalaam, --Baba Tabita (majadiliano) 13:38, 8 Oktoba 2009 (UTC)[jibu]
Sawa. Lakini wao hawataja sanduku la posta, barua pepe - wala namba za simu. Tukifanya hivyo, tutakuwa tunatangaza biashara. Hali ya kuwa kamusi elezo si mahali pa matangazo. Hapo je?--Muddyb MwanaharakatiLonga 13:58, 8 Oktoba 2009 (UTC)[jibu]
Sawa. Nimeondoa barua pepe na simu. Mtu akitaka kuzipata ataweza kuangalia kwenye tovuti ya chuo. Asante kwa rekebisho hilo! --Baba Tabita (majadiliano) 14:25, 8 Oktoba 2009 (UTC)[jibu]