Jennifer Kyaka

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Jennifer Kyaka
Amezaliwa 8 Agosti,1983
Kagera
Nchi Tanzania
Majina mengine Odama
Kazi yake mtayarishaji na muongozaji wa filamu.


Jennifer Kyaka (Odama) (alizaliwa mkoani Kagera 8 Agosti 1983) ni mwigizaji, mtayarishaji na muongozaji wa filamu nchini Tanzania.

Mwaka 2010 alianzisha kampuni ya filamu itwayo J-film ambayo malengo yake makuu ni kuzalisha filamu zenye ubora wa kimataifa na kukidhi mahitaji ya watazamaji.[1]

Maisha ya awali na Elimu[hariri | hariri chanzo]

Jennifer Kyaka alisoma shule ya msingi Kienzya iliyopo Kigoma mjini na baadaye elimu ya sekondari katika shule ya sekondari Minja iliyopo Ugweno, Moshi.[2]

Kazi[hariri | hariri chanzo]

Mwaka 2006 alicheza filamu yake ya kwanza amabayo iliitwa Shumilleta iliyoandaliwa na Mussa Banzi. Baadhi ya filamu alizocheza ni kama House Maid, Pain Killer, My Princess, Nipende Monalisa, House Maid, Fake Love na nyingine nyingi.[3]

Tanbihi[hariri | hariri chanzo]

  1. http://www.hashtagsquare.com/jennifer-kyaka-odama-biography/
  2. "Nakala iliyohifadhiwa". Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2019-04-17. Iliwekwa mnamo 2018-12-01. 
  3. "Nakala iliyohifadhiwa". Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2019-04-17. Iliwekwa mnamo 2018-12-01. 
Makala hii kuhusu mwigizaji filamu fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Jennifer Kyaka kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.