Tawahudi : Tofauti kati ya masahihisho

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Content deleted Content added
Translated from http://en.wikipedia.org/wiki/Autism (revision: 380322410) using http://translate.google.com/toolkit with about 97% human translations.
(Hakuna tofauti)

Pitio la 17:49, 18 Oktoba 2010

Autism
Mwainisho na taarifa za nje
SpecialtyPsychiatry, Elimunafsia, Nyurosaikolojia, pedagogy, Q17749492, Ukuaji wa binadamu Edit this on Wikidata
ICD-10F84.0
ICD-9299.00
OMIM209850
DiseasesDB1142
MedlinePlus001526
eMedicinemed/3202 ped/180
MeSHD001321
GeneReviewsAutism overview

Tawahudi ni ugonjwa wa ukuaji wa neva unaojumuisha kudhoofishwa kwa uwezo wa mwingiliano wa kijamii na mawasiliano, na kwa tabia finyu na ya kujirudiarudia. Ishara hizi huanza kabla ya mtoto kitimiza miaka mitatu.[1] Ugonjwa wa akili kwa watoto huathiri uchakataji wa habari katika ubongo kwa kubadili jinsi seli za neva na sinepsi zake zinavyounganika na kujipanga; jinsi hili hutokea haileleweki vizuri.[2] Ni moja ya matatizo matatu yanayotambulika katika wigo wa Ugonjwa wa akili kwa watoto (ASDs), nyingine mbili zikiwa maradhi ya Aspaja, ambayo haikucheleweshi [3] ukuaji wa kiutambuzi na lugha, na Tatizo la Ukuaji Ulioenea-Usiofafanulika Vinginevyo (kwa kawaida hufupisha Kiingereza kama PDD-NOS ), ambao hutambuliwa kikamilifu wakati vigezo vyote vya kwa kawaida au Aspaja havijatimizwa.[3]

Tawahudi una msingi kamili katika jeni, ingawa mpangilio wa jeni za Ugonjwa wa akili kwa watoto ni changamano na si bayana kama ASD inaelezeka zaidi kwa mabadiliko makuu ya jeni yasiyo ya kawaida, au kwa mchanganyiko usio wa kawaida wa aina tofauti za jeni ya kawaida.[4] Katika matukio nadra, tawahudi unahusishwa sana na visababishi vya kasoro za kuzaliwa.[5] Ubishi unakumba mapendekezo mengine ya visababishi vya kimazingira, kama vile metali nzito, viuadudu au chanjo za utotoni;[6] nadharia tete ya chanjo haiwezekani kibayolojia na zinakosa ushahidi yakinifu wa kisayansi.[7] Uenezi wa tawahudi ni karibu 1-2 kwa kila watu 1,000; uenezi wa ASD ni takriban matukio 6 kwa kila 1,000, huku idadi ya wanaume ikiwa mara nne kuliko ya wanawake. Idadi ya walioaguliwa kuwa na tawahudi umeongezeka kwa kasi tangu miaka ya 1980, kwa kiwangokutokana na mabadiliko katika jinsi ya uaguaji, swali la kama maambukizi shadidi yameongezeka halijafumbuliwa.[8]

Wazazi kawaida hugundua ishara katika miaka miwili ya kwanza ya maisha ya mtoto wao.[9] Dalili hizo kwa kawaida huendelea hatua kwa hatua, lakini baadhi ya watoto wenye Ugonjwa wa akili hukua kwa kawaida kijumla kabla ya ukuaji kubadilika.[10] Ingawa mwingilio wa mapema wa kitabia au wa kitambuzi unaweza kuwasaidia watoto wenye Ugonjwa wa akili kuweza kujuhimili, kupata ujuzi wa kijamii, na mawasiliano, hakuna tiba inayojulikana.[9] Si watoto wengi wenye tawahudi huishi kwa kujitegemea wanapofikia utu uzima, ingawa baadhi huwa wafanisi.[11] Kumeibuka desturi ya tawahudi, huku watu wengine wakitafuta matibabu na wengine wakiamini tawahudi lazima ukubalike kuwa utofauti na wala si ugonjwa.[12]

Sifa bainifu

Tawahudi ni maradhi ya ukuaji wa neva yaliyo na ugeugeu mwingi sana[13]ambayo huonekana kwanza wakati wa ukembe au utoto, na kijumla hufuatavyo mkondo fulani bila kupungua.[14] Dalili za kuonekana huanza polepole baada ya umri wa miezi sita, huwa dhahiri katika umri wa miaka miwili au mitatu,[15] na aghalabu huendelea hadi utu uzima, ingawa mara nyingi katika kimo kilichopungua zaidi.[16] Haitambuliki kwa dalili moja tu, bali kwa sifa bainifu tatu za dalili: udhaifu katika mahusiano ya kijamii; udhaifu katika mawasiliano, hamu finyu ya mambo na tabia ya kujirudiarudia. Vipengele vingine, kama vile ulaji usio wa kawaida, pia ni vya kawaida lakini si muhimu kwa ajili ya uaguzi.[17] Dalili za mtu mwenye tawahudi hutokea katika jamii kijumla na huonekana hajihusishi sana, bila utenganisho wa sifa za kawaida na za kiambukizi.[18]

Ukuaji kijamii

Mapungufu ya kijamii hutofautisha tawahudi na maradhi mengine yaliyo katika wigo unaofafana (ASD, tazama Ainisho) kutoka matatizo mengine ya ukuaji.[16] Watu walio na tawahudi huwa na mapungufu ya kijamii na mara nyingi hukosa uwezo wa kufikiri haraka kuhusu wengine jambo ambalo watu wengi huchukulia kwa mzaha. Temple Grandin mgonjwa wa akili mtambulika alieleza hali yake ya kutoweza kuelewa mawasiliano ya kijamii ya watu wasio na matatizo ya neva, au watu wenye ukuaji wa kawaida wa mfumo neva, kama unaomwacha kujihisi "kama mwanaanthropolojia juu Mirihi".[19]

Ukuaji wa kijamii usio wa kawaida huanza kudhihirika mapema utotoni. Watoto wachanga wenye tawahudi huonyesha makini ndogo kwa michocheo ya kijamii, ni nadra kutabasamu na kuwaangalia wengine, aidha ni nadhra kuitikia jina lao wenyewe. Watoto wachanga wenye tawahudi hukwenda kinyume kabisa na kanuni za kijamii, kwa mfano, hawaangali watu machoni sana wala kujibu wegine katika mazungumzo, na upo uwezekano mkubwa wa kuwasiliana kwa kuchezea mkono wa mwingine.[20] Watoto wa kati ya umri wa miaka mitatu na tao walio na ugonjwa wa akili huenda wasionyeshe uelewa wa masuala ya jamii, huenda wasijue kutangamana moja kwa moja, huiga na kuitikia hisia, hujieleza bila kuzungumza, na hawachangii inapofika zamu yao katika mazungumzo. Hata hivyo, huonyesha mapenzi kwa walezi wao wa kimsingi.[21] Watoto wengi wenye ugonjwa wa akili huonyesha kiasi kidogo cha mapenzi ikilinganishwa na watoto wasio na ugonjwa, ingawa tofauti hii hutoweka kwa watoto walio na ukuaji mkuu wa akili au walio na athari ndogo ya ASD.[22] Watoto wakubwa na watu wazima walio na ASD hufanya vibaya katika mitihani ya utambuzi wa nyuso na hisia.[23]

Watoto walio na kiwango kikubwa cha athari ya tawahudi hukabiliwa na upweke wa kiwango kikubwa na cha mara kwa mara wakilinganishwa na rika lao wasio na ugonjwa wa akili, hii ni licha ya imani ya kawaida kwamba watoto walio na tawahudi hupendelea kuwa pekee yao. Kuanzisha na kudumisha urafiki mara nyingi huwa vigumu kwa walio na tawahudi. Kwa wao, ubora wa urafiki, wala si idadi ya marafiki, huchangia kiwango cha upweke wanachohisi. Urafiki amilifu, kama vile unaojumuisha mwaliko kwa karamu, huweza kuathiri ubora wa maisha kwa undani zaidi.[24]

Kuna taarifa nyingi ya matukio ya kweli, lakini chunguzi chache za kijarabati, kuhusu uchokozi na vurugu unaotekelezwa na watu walio na ADS. Data chache zilizopo zinaonyesha kwamba, kwa watoto wenye akili taahira, tawahudi unahusishwa na uchokozi, uharibifu wa mali, na hamaki. Utafiti mmoja wa 2007 uliowahoji wazazi wa watoto 67 walio na ASD na uliarifu kuwa thuluthi mbili ya watoto hao waliwahi kuwa na hamaki kali, takriban thuluthi moja wakiwa na historia ya uchokozi, huku wakiwa na uwezekano mkubwa wa hamaki kuliko kwa watoto wasio na ugonjwa wa akili mbali na matatizo ya lugha.[25] Utafiti uliofanyika Uswidi 2008 uligundua kwamba, kwa watu wenye umri wa miaka 15 au zaidi walioachiliwa huru kutoka hospitalini baada ya kutambuliwa kuwa na ASD, waliotekeleza uhalifu kwa nguvu pia walikuwa na uwezekano mkubwa wa kuwa na matatizo mengine ya kisaikolojia kama vile wendawazimu.[26]

Mawasiliano

Takribani thuluthi au nusu ya watu walio na tawahudi hukosa kuwa na umilisi wa mazungumzo wa kutosha kukidhi mahitaji yao ya mawasiliano ya kila siku.[27] Tofauti katika mawasiliano inaweza kuwepo katika mwaka wa kwanza wa uhai, na inaweza kujumuisha kuchelewa kuanza kubwabwaja, ishara zisizo za kawaida, mwitikio uliopunguka, na mifumo ya matamshi isiyooana na ya mlezi. Katika mwaka ya pili na wa tatu, watoto walio na ugonjwa wa akili hubwabwaja mara kidogo na maneno yao huwa machache iliyo uchache wa konsonanti, maneno, na mchanganyiko wa maneno, ishara zao mara nyingi haziambatani na maneno. Watoto walio na tawahudi ni nadra kuombi kitu au kujieleza, kuna uwezekano wa wao kurudia tu maneno ya watu wengine (ekolalia)[28][29] au kugeuza kinyume viwakilishi.[30] Mwongozo shirikishi wa makini unaonekana kuwa muhimu katika mazungumzo amilifu, na upungufu katika mwongozo shirikishi wa makini unaonekana kuwatofautisha watoto wachanga walio na ASD:[3] kwa mfano, wanaweza kuangalia mkono unaoashiria badala ya kifaa kinachoashiriwa,[20][29] na pia hushindwa mara nyingi kuashiria vitu ili kutoa maoni au kujieleza.[3] Watoto walio na ugonjwa wa akili wanaweza kuwa na ugumu katika micheza ya ubunifu na kufanya ishara kuwa lugha.[28][29]

Katika jozi ya chunguzi, watoto walio na umri wa miaka 8-15 na wenye ugonjwa wa akili wa kiwango cha juu walifanya bora kuliko waliokuwa wakilinganishwa nao katika mtihani wa msamiati na tahajia. Jozi la watu wazima lilifanya bora zaidi. Makundi yote ya walio na ugonjwa wa akili yalifanya vibaya zaidi kuliko waliokuwa wakilinganishwa nao katika mitihani changamano ya lugha kama vile, jazanda, ufahamu na uchanganuzi. Kwa kuwa mara nyingi watu hutathminiwa kutokana na uelewa wao wa kimsingi wa lugha, chunguzi hizi zinaonyesha kwamba watu wanaozungumza na watu wenye ugonjwa wa akili wanaweza kukadiria juu zaidi kuhusu uelewa wa wasikilizaji wao.[31]

Tabia radidi

Watu walio na ugonjwa wa akili hudhihirisha aina mbalimbali ya tabia tabia radidi au finyu, ambayo Mizani ya Tabia Radidi-Iliyorekebishwa (ufupisho wa Kiingereza RBS-R)[32] inainisha kama ifuatavyo.

Young boy asleep on a bed, facing the camera, with only the head visible and the body off-camera. On the bed behind the boy's head is a dozen or so toys carefully arranged in a line, ordered by size.
Mvulana mdogo aliye na tawahudi, na msururu sahihi wa vijidude livyotengeneza
  • Uradidi ni msogezo wa kujirudiarudia, kama vile kupigapiga mkono, kufanya kelele, kutikisa kichwa, au kutikisa mwili.
  • Tabia ya kulazimisha inanuiwa na huonekana kufuata kanuni, kama vile kupanga vitu katika vitita au mistari.
  • Uhafidhina ni kukataa kukubali mabadiliko, kwa mfano, kusisitiza kwamba samani isisongozwa au kukataa kukatizwa.
  • Uhalisia unahusisha tabia isiyobadili mpangilio wa shughuli za kila siku, kama vile kutobadili menyu au jinsi ya kuvalia. Hii huhusishwa kikaribu na uhafidhina na wathibitishaji wa kujitegemea wamependekeza kuchanganya vipengele hivi viwili.[32]
  • Tabia vikwazo ni finyu katika lengo, nia, au kitendo, kama vile mshughuliko na kipindi kimoja cha runinga, mwanasesere, au mchezo.
  • Kujiumiza hujumuisha vitendo vya kudhuru au vinavyoweza kumdhuru mtu, kama vile kuchokora macho, kujichokoa ngozi, kuuma mkono, na kugonga kichwa.[3] Utafiti mmoja wa 2007 uliarifu kwamba majeraha ya kujiumiza kwa wakati fulani yaliathiri 30% ya watoto walio na ASD.[25]

Hakuna tabia moja radidi au maumivu ya kujisabishia yanayoonekana kuwa mahsusi kwa walio na ugonjwa wa akili, lakini ni ugonjwa wa akili unaonekana kuwa na mfumo wa ongezeko na ushadidi wa matukio ya tabia hizi.[33]

Dalili nyinginezo

Walio na ugonjwa wa akili wanaweza kuwa na dalili zisizotonekana kwa uaguzi, lakini ambazo zinaweza kumwathiri mtu binafsi au familia.[17] Inakadiriwa kuwa kati ya 0.5% hadi 10% ya watu walio na ASD hudhihirisha vipaji visivyo vya kawaida, kwa mfano ujuzi wa kukumbuka maswali madogomadogo pamoja na vipaji nadra sana na kuwa watumishi wa ajabu .[34] Watu wengi walio na ASD hudhihirisha ujuzi mkuu katika mtazamo na makini, ikilinganishwa na watu wa kawaida.[35] Ulemavu katika hisia hupatikana miongoni mwa zaidi ya 90% ya watu walio na tawahudi, na hudhaniwa kuwa sifa msingi na baadhi ya watu,[36] ingawa hakuna ushahidi mzuri kwamba dalili za kihisia hutofautisha tawahudi na maradhi mengine ya ukuaji.[37] Utofauti ni makubwa katika mwitikio-chini (kwa mfano, kutembea kuelekea jambo) kuliko mwitikio-juu (kwa mfano, kuitikia sauti kubwa kutokana na taharuki) au kwa kutafuta mhemko (kwa mfano, misogezo yenye urari).[38] Takribani 60% -80% ya watu walio na ugonjwa akili huwa matatizo katika mwendo ikiwa ni pamoja na misuli iliyo dhoofika, mpangilio hafifu wa kusogeza viungo, na kutembea kwa viganja vya miguu, [36] upungufu katika katika taratibu za kusogeza viungo ni chache kwa walio na ASD na ni kubwa miongoni mwa walio na tawahudi uliokithiri.[39]

Tabia isiyo ya kawaida katika ulaji hutokea katika robo tatu ya watoto walio na ASD, kiasi kwamba awali ilikuwa moja ya viashiria vya uaguzi. Ubaguaji ndilo la tatizo la kawaida zaidi, ingawa desturi za ulaji na kukataa kula pia hutokea;[25] hii haionekani kusababisha utapiamlo. Ingawa baadhi ya watoto walio na tawahudi pia huwa na dalili za ugonjwa wa tumbo na utumbo (GI), kuna ukosefu wa data madhubuti zilizochapishwa kuunga mkono nadharia kwamba watoto walio na ugonjwa wa akili wana tofauti au dalili zaidi za GI kuliko kawaida,[40] chunguzi zimeripoti matokeo yanayokinzana, na uhusiano kati ya GI na matatizo ya ASD si wazi.[41]

Wazazi wa watoto wenye ASD huwa na viwango vya juu vya msongo.[42] Ndugu wa watoto walio na ASD wameripoti kupokea pongezi zaidi na migogoro michache kutoka kwa ndugu walioathirika kuliko ndugu za watoto ambao hawajaathirika au wa wale walio na akili taahira, ndugu za watu walio na ASD wana hatari kubwa zaidi ya kutoendelea vizuri na kuwa uhusiano mbaya baina ya ndugu kama watu wazima.[43]

Uainishaji

Tawahudi ni moja kati ya matano ya Magonjwa ya Ukuaji ya Kuenea Kote, hufupishwa kwa Kiingereza kama (PDD), ambayo huhusishwa na matatizo makubwa katika mwingiliano wa kijamii na mawasiliano, na kutojihusisha na mambo mengi mbali na tabia za kujirudiarudia sana.[14] Dalili hizi haziashirii maradhi, udhaifu, au masumbuko ya hisia.[16]

Kati ya aina tano za Magonjwa ya Ukuaji ya Kuenea Kote PDD, Aspaja ina karibiana na tawahudi kwa ishara na sababu zinazodhaniwa kusababisha magonjwa haya; Ugonjwa wa Rett na ugonjwa wa uchangukaji utotoni yana ishara kadhaa zinazofanana na ugonjwa wa tawahudi, lakini yana visababishi tofauti, PDD isiyotambukika vinginevyo (PDD-NOS, pia hujulikana kama tawahudi usio wa kawaida) huaguliwa wakati vigezo vya kutambua magonjwa mengine maalum havikutimizwa.[44] Tofauti na tawahudi, watu walio na Aspaja hawana uchelewaji mkubwa katika ukuaji wa lugha.[1] Istilahi ya Tawahudi inaweza kukanganya, huku tawahidi, ugonjwa wa Aspaja na PDD-NOS zikijulikana kama Wigo wa Magonjwa ya Akili kwa Watoto (ASD)[9] au wakati mwingine Magonjwa ya Tawahudi, [45] huku tawahidi wenyewe mara nyingi ukitwa Ugonjwa wa Akili kwa watoto, tawahudi utotoni, au tawahudi ya wakembe. Katika makala hii, Tawahudi inarejelea Ugonjwa ya Akili kwa watoto unavyotambulika kimapokeo, japo katika matibabu, tawahudi, ASD, na PDD mara nyingi hutumika kwa maana sawa.[46] ASD, kwa hiyo, ni sehemu tu ya tapo pana ya fenotaipu ya tawahidi, inayowarejelea watu ambao huenda hawana ASD lakini wana sifa bainishi ya tawahidi, kama vile kuepuka kuwatazama watu machoni.[47]

Kujidhihirisha kwa tawahidi huchukua wigo mpana, ikiwa ni pamoja na ulemavu shadidi- unaowafanya kuwa kimya, wenye akili taahira, na wenye kipigapiga makofi na kubembea-na watu wanaotekeleza majukumu makubwa lakini walio na njia zisiyo za kawaida ya kijamii, wenye malengo finyu, na wenye kutumia istilahi nyingi, na sheria za vitabuni katika mawasiliano.[48] Kwa sababu ya wigo wa tabia ni endelevu, mipaka baina ya vitengo vya uaguzi ni kama tu ya kubahatisha.[36] Wakati mwingine dalili za ugonjwa hugawanywa katika viwango vya chini, kati-juu- na vya tawahudi au (TC, TK, na TJ), kulingana na Kiwango cha Akili,IQ,[49] au kiwango cha usaidizi anachohitaji katika maisha ya kila siku, vitengo hivi havijasanifishwa na ni tata. Tawahudi pia unaweza kugawanywa kuwa tawahudi usio na dalili na ulio na dalili; tawahudi ulio na dalili unahusishwa na ulemavu shadidi wa akili au dalili za kuzaliwa ulio na ishara za kimwili, kama vile skelerosisi ya mishipa.[50] Ingawa watu waliona ugonjwa wa Aspaja aghalabu hufanya vizuri kuliko wenye tawahudi katika mitihani ya utambuzi, kiwango cha mwingiliano kati Aspaja, TJ, na tawahudi isiyo na dalili si wazi Hitilafu ya kutaja: Closing </ref> missing for <ref> tag[20][28][51]au kwamba kuna uhusiano endelevu wa tabia kati ya tawahudi iliyo na, na isiyo na kurudi nyuma.[52]

Tafiti kujua visababishi imekinzwa na kutokuwa na uwezo wa kutambua kundi maalum la wanajamii wenye umuhimu kibayolojia[53] na mipaka ya jadi kati ya taaluma za tiba ya maradhi ya akili, saikolojia, nyurolojia na taaluma ya matibau ya watoto.[54] Teknolojia mpya kama vile fMRI na upigaji picha tensa inaweza kusaidia kutambua aina za fenotaipu (sifa zinazoonekana) vinazoweza kutazamwa kupitia uchanganuzi elektroniki wa ubongo, ili kuzidisha utafiti wa kiniurojenetiki wa tawahudi[55] mfano mmoja ni kupungua kwa shughuli katika eneo la fusifomu wa ubongo, ambayo inahusishwa na mtazamo usio kamili wa watu na vitu.[2] Imependekezwa kuanisha tawahudi kutumia jenetiki pamoja na tabia.[56]

Visababishi

Makala kuu: Causes of autism

Kwa muda mrefu imedhaniwa kuwa kuna sababu moja katika viwango vya kijenetiki, kitambuzi, na neva kinachosababisha dalili tatu baifinu za tawahudi.[57] Hata hivyo, kuna ongezeko la shaka kwamba tawahudi ni ugonjwa changamano ambao vipengee vyake vya kimsingi vina visababishi tofauti ambavyo aghalabu hutokea pamoja.[57][58]

Three diagrams of chromosome pairs A, B that are nearly identical. 1: B is missing a segment of A. 2: B has two adjacent copies of a segment of A. 3: B's copy of A's segment is in reverse order.
Utanguaji (1), urudiaji (2) na upinduaji(3) yote ni ulemavu katika kromosomu iliyohusishwa katika tawahudi [59].

Tawahudi una msingi imara katika jenetiki, ingawa jenetiki ya tawahudi ni changamano na si wazi ikiwa ASD inaelezewa zaidi na mabadiliko makuu ya jeni au kwa kwa mwingiliano nadra wa aina mbalimbali za jenetiki aina moja.[4][60] Uchangamano hutokana na mwingiliano kati ya jeni mablimbali, mazingira, na vipengele vya ndani ya jeni visivyobadili viinitete DNA lakini vinaweza kurithika na huathiri wa mwonekano wa jeni.[16] Uchunguzi wa mapacha unaonyesha kwamba uwezo wa kurithika kwa tawahudi ni 0.7 na kwa ASD uwezekani ni wa hadi 0.9, ndugu za walio na tawahudi wanakabiliwa na uwezekano wa hadi mara 25 zaidi kupata tawahudi wakilinganishwa na watu wengine wa kawaida.[36] Hata hivyo, mabadiliko mengi ya viinitete vinavyoongeza uwezekano wa tawahudi hazijatambuliwa. Kwa kawaida, tawahudi hauwezi kuhusishwa na mabadiliko ya Mendeli (jeni moja) au kwa kasoro ya kromosomu moja kama vile kromosomu X dhaifu, na hakuna dalili zozote za kijenetiki zinazohusishwa na ASD zimedhibitishwa kimahususi kusababisha ASD.[4] Jeni mbalimbali zinazodhaniwa kuhusika zimetambuliwa, huku athari kidogo tu zikionekana kuhusishwa na jeni yoyote maalum.[4] Idadi kubwa ya watu wenye tawahudi walio na familia zisizoathirika inaoweza kutokana na mabadiliko ya idadi nakali - mabadiliko ya kujianzisha yenye ikiwemo kujifuta au kijizidisha kwa viungo vya kijenetiki wakati wa meyosisi.[61] Kwa hiyo, kiwango kikubwa cha sababu za tawahudi kinaweza kuhusishwa na visababishi vya kijenetiki vilivyo na uwezo wa kurithika lakini havirithiki: yaani, mabadiliko katika jeni inayosababisha tawahudi hayako katika mkusanyiko wa jeni ya mzazi.[59]

Viwango kadhaa vya ushahidi vinaashiria utendakazi mbaya wa sinepsisi kuwa kisababishi cha tawahudi.[2] Baadhi ya mabadiliko nadra katika viinitete vinaweza kusababisha tawahidi kwa kuvuruga baadhi ya njia za sinepsisi, kama vile zinazohusika na unatishaji wa chembechembe.[62] Tafiti za ubadilishaji wa jeni miongoni mwa panya zinaonyesha kwamba dalili za tawahudi zinahusiana kwa karibu na hatua za ukuaji wa baadaye unaotegemea shughuli katika sinepsina kwa mabadiliko yanayotegemea mifanyiko.[63] Teratojeni zote zinazojulikana (dutu zote zinazosababisha ulemavu wa kuzaliwa) zinazohusiana na uwezekano wa tawahudi huonekana kufanya kazi katika wiki ya nane ya kwanza ya kushika mimba, na japo hii hauzuii uwezekano kwamba tawahudi inaweza kuanza au kuathirika baadaye, ni ushahidi tosha kwamba tawahudi hujitokeza mapema sana katika ukuaji.[5] Japo sababu nyingine za kimazingira za kweli zimenakiliwa na hazijawahi kuthibitishwa kwa tafiti za kuaminika, [6] chunguzi za kina zinaendelea.[64] Sababu za kimazingira ambazo zimedaiwa kuchangia au kuzidisha tawahudi, au zinazoweza kuwa muhimu katika tafiti za siku zijazo, ni pamoja na aina fulani ya vyakula , magonjwa ya kuambukiza, metali nzito, viyeyusha, taka ya dizeli, PCB fithaleti, na fenoli zinazotumika katika bidhaa za plastiki, viuadudu, vizima moto vilivyo na bromini , pombe, uvutaji sigara, mihadarati, chanjo[8], na msongo wa akili kwa mzazi[65], ingawa hakuna uhusiano uliopatikana, na baadhi kutupiliwa mbali kabisa. Wazazi wanaweza kufahamu kwa mara ya kwanza dalili za tawahudi katika mtoto wao wakati wa chanjo ya kawaida, na hii amechangia kuibuka kwa nadharia kwamba chanjo au kemikali zinazotumika kuzihifadhi husababisha tawahudi, na kupelekea utafiti wa kisayansi ambao tayari umethibitisha kuwa huo si ukweli. Ingawa nadharia hizi zinakosa ushahidi thabiti wa kisayansi na hazina mashiko kisayansi, wasiwasi wa wazazi kuhusu tawahudi imesababisha viwango vya chini vya kuchanjwa kwa watoto na uwezekano wa juu wa kuzuka kwa surua katika baadhi ya maeneo. Hitilafu ya kutaja: Closing </ref> missing for <ref> tag Tabia hizo huonekana kuwa na pathofisiolojia nyingi.[18]

Pathofisiolojia

Two diagrams of major brain structures implicated in autism. The upper diagram shows the cerebral cortex near the top and the basal ganglia in the center, just above the amygdala and hippocampus. The lower diagram shows the corpus callosum near the center, the cerebellum in the lower rear, and the brain stem in the lower center.
Tawahudi huathiri amidala , ubongonyuma , na sehemu nyingine nyingi ya ubongo name=Amaral/> <ref.

Tofauti na nyigi ya maradhi mengine ya ubongo kama vile Ugonjwa wa Kikakamaa tawahudi hauna utaratibu wazi wa kuunganisha iwe katika kiwango cha molekuli, chembe, au mifumo, haijulikana kama tawahudi ni hali chache zinazotatiza urazini unaosababishwa na mabadiliko katika viinitete vinavyokutanika katika njia chache za molekyuli, au ni (kama ulemavu wa akili) kama mkusanyiko mkubwa wa matatizo yaliyo na taratibu mbalimbali.[13] Tawahudi yaonekana hutokana na vipengele vya ukuaji vinayoathiri ubongo au mifumo yote tekelezi ya ubongo,[66] na kuvuruga mipangilio wa muda ya ukuaji wa ubongo zaidi ya matokeo ya mwisho.[67] Tafiti za nyuroanatomia na mahusiano ya teratojeni zinaonyesha sana kwamba utaratibu wa tawahudi hujumuisha kugeuza ukuaji wa ubongo punde tu baada ya mimba kutungwa.[5] Ukiushi huu unaonekana kuanzisha msururu wa matukio ya kipatholojia katika ubongo ambayo kwa ukubwa yanaathiriwa na mambo ya kimazingira.[68] Mara tu baada ya kuzaliwa, ubongo wa mtoto mwenye tawahudi hukua kwa kasi zaidi kuliko kawaida, ikifuatiwa na ukuaji wa kawaida au polepole kiasi utotoni. Haijulikani ikiwa ukuaji wa kasi zaidi mapema hutokea kwa watoto wote walio na tawahudi. Inaonekana kudhihirika zaidi katika maeneo ya ubongo yanayosimamia ukuaji mkuu wa ujuzi za kiutambuzi.[36] Nadharia tete za ukuaji kasi usio wa kawaida wa chembe na misingi ya molekyuli ya patholojia ni pamoja na ifuatayo:

  • Uwingi kupita kiasi wa niuroni zinazosababisha miunganiko mingi kupindukia katika maeneo muhimu ya ubongo.[69]
  • Uhamimiaji uliovurugwa wa niuroni katika kipindi cha mapema cha ujaouzito.[70][71]
  • Ukosefu wa ulinganisho baina ya mitandao sisimuzi na mitandao ya kudhibiti msisimko.[71]
  • Miundo kasoro ya sinepsi na miba ya dendraiti,[71] kwa mfano, kwa ubadilikaji wa nureksini - mfumo wa chembe za unataji wa niurolijini, [72] au kwa udhibiti hafifu wa usanisi protini za sinepi.[73] Ukuaji wa sinepi uliovurugwa pia unawekuchangia kifafa, ambayo inaweza kueleza kwa nini hali hizi mbili zinahusiana.[74]

Mwingiliano kati ya mfumo wa kinga na mfumo wa neva kuanza mapema katika hatua ya kiinitete cha maisha, na ukuaji uliofanikiwa wa mfumo wa neva unategemea mwitikio unauwiano wa kinga. Inawezekana kwamba shughulu potovu ya kinga katika vipindi muhimu vya ukuaji wa mfumo wa neva ni sehemu ya taratibu za aina fulani za ASD.[75] Ingawa baadhi ya ulemavu katika mfumo wa kinga umepatikana katika vijikundi maalum vya watu wenye tawahudi, haijulikani kama ulemvu huo ni muhimu au huchangia mifanyiko ya ugonjwa wa tawahudi.[76] Kwa kuwa zindikomwilinafsi hupatikana katika hali zingine ambazo si za ASD, na si kila mara hupatikana katika ASD,[77] uhusiano kati ya kuvurugwa kwa kinga mwili na tawahudi bado haujabainika na una utata.[70]

Uhusiano wa kemikali za neva na tawahudi haueleweki vizuri; kadhaa zimechunguzwa huku kukiwa na ushahidi zaidi katika jukumu la serotonini na tofauti za kimaumbile katika usafirishaji wake.[2] Baadhi ya takwimu zinaonyesha ongezeko la ukuaji wa homoni kadhaa, takwimu zinaashiria kwa kupungua kwa vipengele vya ukuaji.[78] Aidha, baadhi makosa ya kimetaboli ya kuzaliwa yanahusishwa na tawahudi lakini pengine huchangia chini ya 5% ya matukio.[79]

Nadharia ya mfumo wa niuroni akisi (MNA) kuhusu tawahudi inakisia kwamba mabadiliko katika ukuaji wa MNA unahitilafiana na uigaji na husababisha sifa za msingi za tawahudi ambazo ni ulemavu katika mwingiliano wa kijamii na matatizo ya mawasiliano. MNA hufanya kazi wakati mnyama anapofanya kitendo au anapomtazama mnyama mwingine akifanya kitendo sawa na hicho. Mfumo wa Niuroni Akisi MAN unaweza kuchangia uelewa mtu fulani kuhusu watu wengine kuwezesha kubwia kimtazamo tabia zao kupitia kujumuishwa kwa mienendo yao, nia, na hisia Hitilafu ya kutaja: Closing </ref> missing for <ref> tag Hata hivyo, watu walio na tawahudi wana msisimko usio wa kawaida katika mizunguko nyingi ya ubongo nje ya MAN[80] na nadharia MAN haieleza utendaji wa kawaida wa watoto walio na tawahudi katika majukumu ya kuiga yanayohusu lengo au kifaa.[81]

[[File:Powell2004Fig1A.jpeg|thumb|upright|alt=A human brain viewed from above. About 10% is highlighted in yellow and 10% in blue. There is only a tiny (perhaps 0.5%) green region where they overlap.|Watu walio na tawahudi angalabu hutumia ya maeneo mbalimbali ya ubongo (njano) kwa kazi sogezi ikilinganishwa na kundi la kudhibiti (samawati) Hitilafu ya kutaja: Closing </ref> missing for <ref> tag Katika tawahudi kuna ushahidi wa kupunguka kwa miunganiko akisi, mtandao mkubwa wa miungano ya ubongo inayohusika katika uchakataji wa masuala ya kijamii na kihisia, huku mitandao chanya, ikitumika katika kudhititi umakini na kufikiri kuliko na lengo. Kwa watu walio na tawahudi mitandao hiyo mwili haihusiani vibaya kiwakati, na hivyo kudokezea kukosa usawa wa kujibana katika mitandao hiyo miwili, na huenda kuashiria kuvuruga mrejeleo wa kibinafsi wazo.[82] Utafiti mmoja wa 2008 ulipata mtindo maalum wa ishara katika gamba la singulamu inayotofautiana katika watu waliona ASD.[83]

Nadharia tete ya muungano wa chinichini wa tawahudi kwamba tawahudi inahusishwa na kutofanya kazi kikamilifu kwa viunganishi na uoanishaji wa hali ya juu wa niuro, pamoja na uziada wa michakato ya chini.[84] Ushahidi wa nadharia hii imepatikana katika tafiti za picha za niuro ya watu walio na tawahudi[31] na kwa utafiti wa mawimbi ya ubongo yaliyopendekeza kuwa watu wazima walio na ASD wana miungano zaidi katika gamba na muunganiko akisi dhaifu kati tundu la mbele na katika gamba lote.[85] Ushahidi mwingine unaonyesha miunganiko isiyo ya kawaida sana sana huwa katika kila kizio cha gamba na kwamba tawahudi ni ugonjwa unaohusishwa na gamba.[86]

Kutokana na tafiti zilizohusishwa na matukio, mabadiliko ya muda mfupi kwa utendakazi wa kielektroniki wa ubongo katika kuitikia michocheo, kuna ushahidi wa kutosha kuelezea tofauti katika watu walio na tawahudi katika masuala ya uangalifu, mkao, kusikiliza pamoja na michocheo ya kutazama, kugundua nupya, lugha na kutambua nyuso , na kuhifadhi habari, tafiti kadhaa zimepata upendeleo kwa michocheo isiyo ya kijamii.[87] Kwa mfano, chunguzi ya michorosumaku ya ubongo zimegundua ushahidi wa watoto walio na tawahudi kuchelewa kuitikia uchakatai wa ujumbe wa sauti kutoka katika ubongo.[88]

Niurosaikolojia

Nadharia mbili kuu za utambuzi imependekezwa kuhusu mahusiano kati ya akili tawahudi na tabia.

Aina ya kwanza inalenga upungufu katika utambuzi wa kijamii. Nadharia ya kumwelewa mwingine na huruma pinadai kwamba watu walio na tawahudi wanaweza kuhurumia-yaani, wanaweza kuanzisha msharti ya utendaji ya kushughulikia matukio katika ubongo-lakini ina ufanisi mdogo katika kuelewa hali ya mwingine kwa kusimamia matukio yaliyoanzishwa na kitu kingine. Upanuzi wa nadharia tete ya ubongo wa mwanaume, inapendekeza kwamba tawahudi ni tikio baya la ubongo wa mwanamume, hufafanuliwa kwa vipimo vya nafsia kama watu ambao kwao uratibu ni vyema kuliko kuelewa hali za wengine,[89] upanuzi huu ni tata, kwa kuwa tafiti nyingi inapinga wazo kwamba watoto wavulana na wasichana huitika tofauti kwa watu na vitu.[90]

Nadharia hizi kwa kiasi fulani zinafanana na nadharia a akili ya awali katika mtazamo, inayodhahania kwamba tabia ya kitawahudi inajitokeza kutokana na kukosa uwezo wa kujifafanulia hali kiakisliau watu wengine. Dhanio ya nadharia tete ya akili ina mhimili katika mwitikio usio wa kawaida wa watoto walio na tawahudi kwa uchunguzi wa Anne-Sally wa kutathmini motisha ya wengine,[89] na nadharia ya mfumo akisi wa niuro ya tawahudi ilivyoelezwa vizuri katika ramani za Pathofisiolojia dhana tete.[91] Hata hivyo, uchunguzi nyingi hazijagundua ushahidi wa kuharibika uwezo wa watu walio na tawahudi kuelewa nia au malengo ya msingi ya watu wengine , badala yake, data zinaonyesha kwamba kasoro hupatikana katika kuelewa hisia changamano za kijamii au katika kuzingatia mitazamo ya wengine.[92]

Kitengo cha pili kinaangazia michakato ya isiyo ya kijamii katika utendakazi wa kijumla. Nadharia tete ya kasoro ya utendaji inakisia kuwa tabia za tabia za kitawahudi kwa kiwango chache hutokana na upungufu katika kumbukumbu ya kazi, upangaji, uzuiaji, na aina nyingine ya kazi tendaji.[93] Chunguzi za michakato tendaji ya kimsingi kama vile tendo la jicho kuongasonga huonyesha kuboreka kutoka utoto hadi ujana, lakini havifikii viwango vya kawaida vya utendaji wa kawaida kwa mtu mzima.[94] Uziti wa nadharia hiyo ni kutabiri tabia zinazorudiwaridiwa na vivutio vichache;[95] mapungufu mawili ni kwamba nadharia ya jukumu tekelezi ni vigumu kupima[93] na kwamba upungufu wa utenda jukumu haujapatikana miononi mwa watoto walio na tawahudi.[23]

Nadharia ya udhaifu kati uwiano mkuu inakisia kwamba uwezo wa kutoona picha kubwa ndio msingi wa usumbufu wa tawahudi. Nguvu moja ya nadharia hii ni kutabiri vipaji na vilele katika utendaji wa watu walio na tawahudi.[96] Nadharia nyingine inayofanana na hiyo-nadharia ya utambuzi akisi-inalenga zaidi ubora wa michakato iliyoanza mahala moja na shughuli tambuzi kwa watu walio na tawahudi.[97] Nadharia hizi zinaelezeka vizuri kutoka katika nadharia ya ufiche ya tawahudi.

Hakuna aina moja ya nadharia inayoridhisha ikiwa yenyewe, nadharia ya utambuzi kijamii haifafanui vyema tabia zisizobadilika na za kujirudiarudia kwa walio na tawahudi, huku nadharia zisizo za kijamii zina ugumu kueleza hitilafu za kijamii na matatizo ya kimawasiliano.[58] Nadharia iliyochangnywa kwa kutegemea hitilafu mbalimbali inaweza kuwa muhimu zaidi.[98]

Uchunguzi

Takribani nusu ya wazazi wa watoto walio na ASD hutambua tabia isiyo ya kawaida kwa mtoto wao katika umri wa miezi 18, takriban khumusi nne hutambua abapofika umri wa miezi 24.[51] Kwa kuwa kuahirisha matibabu kunaweza kuathiri matokeo ya hapo baadaye, ishara yoyote kati ya zifuatazo ni sababu ya kuhakikisha mtoto anakaguliwa na mtaalamu bila kuchelewa:

  • Kukosa kubwabwaja kufikia mwezi wa 12.
  • Kukosa ishara (kuashiria kwa vidole, kupunga ishara ya kuaga, nk) kufikia mwezi wa 12.
  • Kutoweza kutaja maneno ya neno moja kufikia mwezi wa 16.
  • Kukosa virai vya maneno mawili ya kujianzia (mbali na matukio ya ukasuku) kufikia mwezi wa 24.
  • Kupoteza ujuzi wowote wa lugha yoyote au ujuzi wa jamii, katika umri wowote.[17]

Nchini Marekani na Ujapan mazoezi ni kuwachunguza watoto wote kubaini ASD wakitimia miezi 18 na 24, kwa kutumia vipimo maalum vya kuchunguza tawahudi kirasmi. Kinyume ni kwamba, nchini Uingereza, watoto ambao familia au madaktari wametambua ishara zinazoweza kuwa za tawahudi ndio hukaguliwa. Haijulikani njia gani bora zaidi.[2] Vifaa vya uchunguzi ni pamoja na Orodha ya Kuchunguza Tawahudi katika Watoto (M-CHAT), Hojaji ya Kuchunguza Ishara za Mapema ya Tawahudi, na Orodha ya Mwaka wa Kwanza, data ya awali ya M-CHAT na CHAT iliyoitangulia kwa watoto wenye umri wa miezi 18-30 inaonyesha kwamba inatumika vizuri katika mazingira ya kimatibabu na kwamba ina uwezo wa kuonyesha athari ndogondogo (hasi nyingi zisizo za kweli) lakini ubayana mzuri (chanya chache zisizo za kweli).[51] Inaweza kuwa sahihi zaidi kutatangulia vipimo hivi na uchunguzi mpana usiotofautisha ASD na matatizo mengine ya ukuaji.[99] Vifaa vya uchunguzi viliyoundwa kwa ajili ya utamaduni wa jamii moja kuchunguza tabia kama vile kuangalia mwingine machoni vinaweza vikawa si muafaka katika utamaduni tofauti.[100] Ingawa uchunguzi wa kijenetiki wa tawahudi kwa ujumla bado haiwezekani, inaweza kuzingatiwa katika baadhi ya matukio, kama vile kwa watoto walio na dalili za kinyurolojia na maumbile ya. ulemavu wa kuzaliwa[101]

Uaguzi

Uaguzi unategemea tabia, si sababu au utaratibu.[18][102] Tawahudi inafafanuliwa katika DSM-IV-TR kuwa na angalau jumla ya dalili sita, ikiwa ni pamoja na angaa dalili mbili za kulemaa kwa ubora wa mahusiano ya kijamii, angalau dalili moja ya kuharibika kwa ubora katika mawasiliano, na angalau dalili moja ya tabia finyu na kujirudiarudia. Mfano wa dalili ni pamoja na kukosa kuonyesha hisia sawa na wengine au za kijamii, utumizi wa lugha ya kurudiarudiaha au lugha ya kipekepeke, na uvutiwaji wa kuendelea na sehemu ya vitu. Mwanzo lazima uwe kabla ya umri wa miaka mitatu, huku kukiwa na ucheleweshaji au utendaji usio wa kawaida katika mahusiano ya kijamii, lugha kama inavyotumika katika mawasiliano ya kijamii, au ishara au micheza bunifu. Mvurugiko haufai kuelezeka kwa ubora kuwa uliosababishwa na ugonjwa wa Rett au Ugonjwa wa uchangukaji utotoni.[1] ICD-10 pia kimsingi hutumia ufafanuzi huo.[14]

Zana kadhaa za uagizi zinapatikana. Mbili hutumika sanasana katika kutafiti tawahudi: Mahojiano Aguzi ya Tawahudi-Yaliyorekebishwa (ADI-R), ni mahojiano yenye mwongozo kidogo yanayotumiwa na mzazi, na Jedwali la Uaguzi wa Tawahudi kwa Kutazama (ADOS) hutumia uchunguzi na mwingiliano na mtoto. Mizani ya Kukadiria Tawahudi Utotoni (CARS) hutumika sana katika mazingira ya kimatibabu kutathmini ushadidi wa tawahudi kwa kumchunguza watoto.[20]

Kwa kawaida daktari wa watoto hufanya uchunguzi wa awali kwa kutumia historia ya ukuaji na uchunguzi wa kimwili wa mtoto. Panapohitajika uaguzi na uchunguzi hufanyika kwa msaada wa wataalamu wa ASD, kuangalia na kukadiria vipengele vya kitambuzi, mawasiliano, familia, na sababu nyingine kwa kutumia zana sanifu, na kuzingatia hali yoyote ya kimatibabu inayohusiana na ugonjwa huo.[103] Mwana nyurosaikolojia wa watoto mara nyingi huombwa kutathmini tabia na ujuzi tambuzi, ili kusaidia uaguzi na kusaidia kupendekeza husaidizi wa kielimu.[104] Uaguzi tofautishi wa ASD katika kiwangi hiki pia unaweza kuzingatia ulemavu wa kiakili, matatizo ya kusikia, na ulemavu maalum wa lugha [103] kama vile ugonjwa wa Landau-Kleffner.[105] Uwepo wa tawahudi unewanaweza kuifanya vigumu kuagua matatizo ya kiakili yanayotokea pamoja kama vile unyogovu.[106]

Tathmini jenetiki ya kimatibabu mara nyingi hufanywa baada ya ASD imeaguliwa, hasa wakati dalili nyingine tayari zinaashiria sababu za kijenetiki.[46] Ingawa teknolojia ya kijenetiki inaruhusu wataalamu wa jenetiki kuhusisha takribani 40% ya visi na visababishi vya kijenetiki,[107] mwongozo wa makubaliano katika mataifa ya Marekani na Uingereza unahusu picha zenye umadhubuti wa hali ya juu wa kromosomu na tathmini X unaohitaji uangalifu zaidi.[46] Uaguzi wa kwanza wa mfano wa aina jeni umapendekezwa, ambao utakuwa ukichunguza mara kwa mara nakala kadhaa za jinomu moja.[108] Jinsi vipimo vipya vya kijenetiki vinavyoundwa masuala kadhaa ya kimaadili, kisheria, na kijamii yatajitokeza. Upatikanaji wa kibiashara wa upimaji unaweza kutangulia uelewa wa kutosha wa jinsi ya kutumia matokeo ya upimaji, ikizingatiwa uchangamani wa jeni za tawahudi.[109] Vipimo vya kimetaboli na picha za neva wakati mwingine husaidia , lakini si mara kwa mara.[46]

Wakati mwingine ASD inaweza kuaguliwa katika umri wa miezi 14, ingawa uaguzi huendelea kuwa imara katika kipindi cha miaka mitatu ya kwanza ya maisha: kwa mfano, mtoto wa mwaka moja anayetimiza viwango vya kuaguliwa kuwa na ASD anauwezekano mdogo kuliko wa mtoto wa miaka mitatu kuendelea kuonyesha dalili hizo kwa muda wa miaka michache baadaye.[51] Nchini Uingereza Mpango wa Taifa wa Watoto wenye Tawahudi inapendekeza wiki zisizozidi 30 kutoka shaka ya kwanza hadi kukamilika kwa uaguzi na tathmini, hata hivyo ni visa vichache hushughulikiwa haraka hivyo kihalisia.[103] Uchunguzi mmoja wa 2009 nchini Marekani uligundua kwamba umri wastani wa uaguzi wa ASD ulikuwa miaka 5.7, juu kabisa ya mapendekezo, na kwamba 27% ya watoto walisalia bila kuaguliwa katika umri wa miaka 8.[110] Ingawa dalili za tawahudi na ASD huanza mapema utotoni, wakati mwingine huwa hazipatikani; miaka baadaye, watu wazima wanaweza kutafuta uaguzi ili kuwasaidia au rafiki zao na familia kujielewa, kuwa saidia waajiri wao kufanya marekebisho au, katika baadhi ya maeneo kudai ulemavu posho ya walemavu au faida nyingine.[111]

Uaguzi unaoweka ushadidi wa ugonjwa chini au juu zaidi ni tatizo katika matukio ambayo hayajidhihirishi kikamilifu, na ongezeko la hivi karibuni katika idadi zilizoripotiwa za matukio ya ASD huenda imetokana na mabadiliko katika mbinu za uaguzi. Ongezeko la umaarufu wa matibabu kwa dawa na upanuzi wa faida umewapa motisha watoa huduma kuagua ASD na kusababisha baadhi ya uaguzi shadidi wa juu zaidi katika watoto walio na dalili zisizo za uhakika. Kinyume ni kwamba, gharama ya uchunguzi na uaguzi na changamoto ya kupata malipo inaweza kuzuia au kuchelewesha uaguzi.[112] Ni vigumu hasa kuagua tawahudi miongoni mwa wasio na uwezo wa kuona, kwa kiwango fulani ni kwa sababu baadhi ya vigezo vya uaguzi hutegemea kuona, na kwa kiwango kwa sababu dalili za tawahudi huingiliana na yale ya maradhi ya upofu wa kawaida au mienendo pofu.[113]

Udhibiti

Makala kuu: Autism therapies
A young child points, in front of a woman who smiles and points in the same direction.
Mtoto mwenye umri wa miaka mitatu mwenye tawahudi aashiria samaki katika hodhisamaki, kama sehemu ya majaribio ya athari ya mafunzo ya pamoja katika ukuaji wa lugha. [114]

Malengo kuu wakati wa kuwatibu watoto walio na tawahudi ni kupunguza mapungufu yanayohusishwa na ugonjwa huo na dhiki ya familia, na kuongeza ubora wa maisha na uhuru akisi. Hakuna tiba moja iliyo bora na matibabu kwa kawaida hutolewa kutegemea mahitaji ya mtoto.[9] Familia na mfumo wa elimu ndio vyanzo muhimu vya matibabu.[2] Chunguzi za hatua za udhibiti zina matatizo ya kimtindo yanayozuia uthibitisho wa kamilifu kuhusu umadhubuti.[115] Ingawa hatua nyingi za udhibiti wa kisaikojamii zimeonysha kiwango fulani cha matokeo mema , na kuashiria kwamba matibabu ya aina yoyote yanafaa kuliko kutotubu, ubora wa utaratibu wa mapitio ya chunguzi hizi kwa jumla hayajakuwa mazuri, matokeo yao ya kimatibabu huwa ya kimajaribio zaidi, na kuna ushahidi mdogo wa umadhubuti linganifu katika mbinu za matibabu.[116] Mipango shadidi na endelevu ya elimu maalum na tabia tiba mapema katika maisha yanaweza kuwasaidia watoto kupata ujuzi wa, kujimudu, kijamii, na ujuzi wa kazi,[9] na aghalabu kuboresha utendaji na kupunguza ukali wa dalili na tabia zisizo za kawaida,[117] madai kwamba udhibiti kuanzia umri wa miaka mitatu ni muhimu hayajathibitishwa.[118] Mbinu zilizopo ni pamoja na Uchambuzi Tabia Kimatumizi (ABA), vilinganishi vya ukuaji, mafundisho yaliyopangiliwa, matibabu ya uzungumzaji na lugha, matibabu ya ujuzi wa kijamii, na tiba kwa ulemavu.[9] Baadhi ya miingilio ya kielimu yana ufanisi fulani kwa watoto: matibabu ya ABA yamethibitisha umadhubuti katika kuongezeka kijumla kwa utendaji kwa watoto ambao hawajaenda shuleni[119] na yameimarishwa ili kuboresha utendaji wa kiakili wa watoto wadogo.[117] Taarifa za wataalamu wa nyurosaikolojia mara nyingi hayafikii vizuri waelimishaji, hali inayosababisha pengo kati ya kile ripoti inapendekeza na elimu inayotolewa.[104] Haijulikana kama harakati za matibabu kwa watoto husababisha uboreshwaji mkubwa baada ya watoto kukua,[117] na utafiti mdogo kuhusu ufanisi wa mipango ya mafunzo ya kinyumbani kwa watu wazima unaonyesha matokeo mchanganyiko.[120]

Dawa nyingi zinazotumika kutibu dalili za ASD huathiri kuingiliana kwa mtoto na nyumba au shule wakati tabia matibabu yameshindwa.[16][121] Zaidi ya nusu ya watoto wa Marekani walioaguliwa kuwa na ASD hupewa dawa za kuathiri akili au kinza-msukosuko, huku aina za dawa zinazotumika mara kwa mara zikiwa tibamfadhaiko, vichangamshi, na vizuia magonjwa ya akili.[122] Mbali na dawa za kuzuia magonjwa ya akili,[123] kuna utafiti mchache wa kuaminika kuhusu umadhubuti au usalama wa matibabu ya dawa kwa vijana na watu wazima walio na ASD Hitilafu ya kutaja: Closing </ref> missing for <ref> tag na hakuna dawa inayojulikana hupunguza dalili za kimsingi za tawahudi ambazo ni ulemavu wa kijamii na mawasiliano.[124] Majaribio katika panya yamerudisha nyuma au kupunguza baadhi ya dalili zinazohusishwa na tawahudi kwa kuondoa au kurekebisha kazi za jeni baada ya kuzaliwa,[63] hii inapendekeza uwezekano wa kulenga matibabu katika mabadiliko mahsusi ya jeni nadra inayojulikana kusababisha tawahudi.[62]

Ingawa matibabu mengi na udhibiti mbadala unapatiakna, ni chache zinaushahidi wa uchunguzi wa kisayansi.[23][125] Mbinu za matibabu zina ushahidi mdogo wa kijarabati katika ubora wa hali za maisha , na mipango nyingi huzingatia hatua za mafanikio ambazo hukosa ukweli wa kubashirika na umuhimu katika dunia halisi.[24] Ushahidi wa kisayansi unaonekana jambo lisilo la muhimu kwa watoa huduma ikilinganishwa na mpango wa uuzaji, upatikanaji wa mafunzo, na maombi ya wazazi.[126] Ingawa matibabu mengi mbadala, kama vile melatonin, yana madhara kidogo tu [127] yanaweza kumhatarisha mtoto. Utafiti mmoja wa 2008 iligundua kuwa ikilinganishwa na rika zao, wavulana walio na tawahudi huwa na mifupa konde sana ikiwa hawali chakula kilicho na kasini,[128] mnamo 2005, matibabu ya kelesheni yalimuua mvulana wa umri wa miaka mitano aliyekuwa na tawahudi.[129]

Matibabu ni ghali, gharama yasiyo ya moja kwa moja pia ni ghali. Kwa mtu aliyezaliwa mwaka 2000, utafiti mmoja wa Marekani ulikadirio matumizi ya wastani maishani ya dola 3.77 million (thamani halisi ya sasa ni 2024 dola, marekebiso ya liyofanyiwa mfumuko wa bei kutoka makisio ya 2003[130]), kukiwa na takriban 10% ya huduma ya matibabu, 30% elimu ya ziada na huduma nyingine, na 60% kwa tija ya kiuchumi iliyopotea.[131] Mipango inayosimamiwa na serikali mara nyingi haitoshi au hazifai kwa watoto fulani, na gharama ya dawa au tiba inayotumiwa na wazazi bila kurejeshewa fedha na serikali imehusishwa na matatizo ya kifedha katika familia,[132] uchunguzi mmoja wa Marekani 2008 ulipata hasara ya wastani 14% ya mapato ya kila mwaka katika familia ya watoto walio na ASD,[133] na uchunguzi mwingine unaohusiana na huo ulipata kwamba ASD inahusishwa na uwezekano mkubwa kwamba matatizo ya ulezi wa watoto yanaathiri uwezekano wa wazazi kuajiriwa.[134] Majimbo ya Marekani yanazidi kuhitaji kuwa bima ya afya ya kibinafsi ishughulikie huduma za kitawahudi, kuhamisha gharama kutoka mipango ya unafadhili wa elimu ya umma hadi katika mipango ya kibinafsi ya kufadhili bima ya afya.[135] Baada ya utotoni, masuala makuu ya kimatibabu ni pampja na ulinzi wa mahala pa makazi, mafunzo ya kazi na kuajiriwa, kujamiiana, ujuzi wa kijamii, na mipango ya mali pa kuishi.[136]

Ubashiri

Hakuna tiba inajulikana.[2][9] Mara moja moja watoto hupona, hivi kwamba hupoteza uaguzi wa ASD, [137] hii hutokea wakati mwingine baada ya matibabu makali na wakati mwingine bila matibabu. Haijulikani uponyaji hufanyika vipi;[117] viwango vilivyoripotiwa katika sampuli zisizochaguliwa za watoto walio na ASD zimekuwa kati ya 3% hadi 25%.[137] Watoto wachache waliokuwa na tawahudi wamepata uwezo wa kuongea katika umri miaka 5 au zaidi.[138] Watoto wengi wengi walio na tawahudi hukosa misaada ya kijamii, mahusiano thabiti, fursa za ajira baadaye au uwezo wa kujifanyia maamuzi ya kibinafsi.[24] Ingawa matatizo ya kimsingi ni kana kwamba huendelea, ushadidi wa dalili aghalabu hupungua kulingana na umri.[16] Chunguzi chache za hali ya juu hushughulikia ubashiri wa muda mrefu. Baadhi ya watu wazima kuonyesha maendeleo ya wastani katika ujuzi wa mawasiliano, lakini wachache hudorora, hakuna utafiti umelenga tawahudi baada ya umakamo.[139] Kumudu lugha kabla ya umri miaka sita, kuwa na Kiwango cha Akili cha zaidi ya 50, na kuwa na ujuzi unaoweza kumpatia mtu ajira ni utabiri wa matokeo bora, maisha ya kujitegemea huenda yasiwezekane kwa walio na tawahudi shadidi.[140] Uchunguzi mmoja mnamo 2004 nchini Uingereza kwa watu wazima 68 waliokuwa wameaguliwa kabla ya 1980 kuwa watoto wenye tawahudi walio na Kiwango cha Akili, IQ cha zaidi ya 50 uligundua kwamba 12% walifanikiwa kupata kiwango cha juu cha uhuru katika utu uzima, 10% walikuwa na idadi fulani ya marafiki na kijumla walikuwa na kazi japo walihitaji kiwango fulani cha msaada, 19% walikuwa na kiasi fulani cha uhuru lakini kijumla walikuwa wakiishi nyumbani na walihitaji msaada na usimamizi mkubwa katika maisha ya kila siku, 46% walihitaji makazi maalum katika vituo vya ASD wakihitaji kiwango cha juu cha msaada na uhuru mdogo sana, na 12% walihitajika kiwango cha juu cha utunzi hospitalini.[11] Uchunguzi mmoja wa 2005 nchini Uswidi wa watu wazima 78 ambao haukuwatenga watu waliokuwa na Kiwango cha Akili, IQ cha chini ulipata ubashiri mbaya zaidi, kwa mfano, 4% tu walipata uhuru.[141] Uchunguzi mmoja nchini Kanada mwaka wa 2008 wa watu wazima 48 walioaguliwa kuwa na ASD wakiwa watoto kabla ya kuenda shule ulipata matokeo kama yafuatavyo, vibaya (46%), kadiri (32%), vizuri (17%), na vizuri sana (4%), 56% ya watu hao walikuwa wameajiriwa wakati fulani katika maisha yao, wengi wao katika kujitolea, na katika sehemu zilizolindwa au kazi za muda.[142] Mabadiliko katika mikakati ya uaguzi na kuongeza katika upatikanaji wa tiba za mapema madhubuti inaifanya vigumu kubaini kama matokeo haya yanaweza kuchukuliwa kuwakislisha watoto walioaguliwa hivi karibuni.[8]

Epidemolojia

Bar chart versus time. The graph rises steadily from 1996 to 2007, from about 0.7 to about 5.3. The trend curves slightly upward.
Ripoti za matukio ya tawahudi kwa watoto 1,000 ziliongezeka kwa kasi Marekani kuanzia 1996 hadi 2007. Haijulikani ni kiasi gani, kama ipo, cha ongezeko kilitokana na mabadiliko katika uenezi wa tawahidi.

Mapitio ya hivi karibuni zaidi yanakisia uenezi kuwa kati ya mtu 1-2 kwa kila 1,000 kwa tawahudi na takribani 6 kwa kila 1,000 kwa ASD,[8] kwa sababu ya ukosefu wa data, takwimu hizi zinaweza kutoa makisio ya chini ya uenezi wa ASD.[46] Uenezi wa PDD-NOS munakisiwa kuwa 3.7 kwa kila 1,000, Aspaja kuwa 0.6 kwa kila 1,000, na ugonjwa wa uchangukaji utotoni kuwa 0.02 kwa kila 1,000.[143] Idadi ya matukio ya tawahudi yaliyoripotiwa yaliongezeka katika miaka ya 1990 na mapema miaka ya 2000. Ongezeko hili kwa kiasi kikubwa kinasemekana kutokana na mabadiliko katika mikakati ya uaguzi, mielekeo wa rufaa, upatikanaji wa huduma, umri wakati wa uaguzi, na uhamasishaji umma,[143][144] ingawa athari za kimazingira ambazo hazijatambulika haziwezi kupuuziliwa mbali.[6] Ushahidi uliopo haufutilii uwezekano kwamba uenezi wa kweli wa tawahudi umeongezeka; [143] ongezeko halisi linaweza kupendekeza kuelekeza makini na ufadhili zaidi katika vipengele vya mabadiliko ya kimazingira badala ya kuendelea kuzingatia vipengele vya kijenetiki.[64]

Wavulana wana hatari kubwa kuwa na ASD kuliko wasichana. Wastani wa uwiano wa kijinsia ni 4.3:1 na inaweza kuathirika sana na ulemavu wa kitambuzi: inaweza kuwa na ukaribu wa 2:1 na walio na akili taahira na zaidi ya 5.5:1 psipo na akili taahira.[8] Ingawa ushahidi hauhusishi hatari zozote zinazofungamanishwa na ujauzito na kusababisha ya tawahudi, hatari ya tawahudi inahusishwa na umri mkubwa wa mmoja wa wazazi, ugonjwa wa kisukari, kutokwa na damu, na matumizi ya dawa za magonjwa ya akili kwa mama wakati wa ujauzito.[145] Hatari ni kubwa zaidi kwa baba mwenye umri mkubwa kuliko mama mwenye umri mkubwa, maelezo mawili ya uwezekano yanajulikana, kuongeza kwa uwezekano wa mabadiliko ya kijenetiki katika manii kongwe, na nadharia tete kwamba wanaume huchelewa kuoa ikiwa wana upungufu wa kijenetiki na kuonyesha baadhi ya ishara za tawahudi.[36] Wataalam wengi wanaamini kuwa rangi, kabila, na usuli wa kiuchumi haziathiri uwepo wa tawahudi.[146]

Hali nyingine kadhaa ni ya kawaida kwa watoto walio na tawahudi.[2] Hizi ni pamoja na:

  • Matatizo ya Kijenetiki. Takribani 10-15% ya matukio ya tawahudi yana hali ya Mendeli (jeni moja) inayoweza kutambulika, ulemavu wa kromosomu, au dalili nyingine za kijenetiki,[147] na ASD inahusishwa na matatizo kadhaa ya kijenetiki.[148]
  • Akili taahira. Kiwango cha watu watu walio na tawahudi ambao pia wanatimiza vigezo vya akili taahira kimeripotiwa kuwa popote kati ya 25%-70%, utofauti mkubwa unaashiria ugumu wa kutathmini akili ya walio na tawahudi.[149] Kwa maradhi mengie ya ASD mbali na tawahudi, uhusiano na akili taahira ni dhaifu sana.[150]
  • Matatizo ya wasiwasi s ni ya kawaida miongoni mwa watoto walio na ASD, hakuna takwimu imara, lakini uchunguzi umeripoti ueneze wa kuanzia 11% hadi 84%. Matatizo mengi ya wasiwasi yana dalili yanayoelezeka vyema kwa ASD yenyewe, au ni vigumu kutofautisha na za dalili ASD.[151]
  • Kifafa, kukiwa na tofauti katika uwezekano wa kupata kifafa kutegemea umri, kiwango cha utambuzi, na aina ya tatizo la lugha.[152]
  • Ulemavu kadhaa wa kimetaboli, Kama vile feniliketonuria, unahusishwa na dalili za kitawahudi.[79]
  • Ulemavu mdogo wa kimwili huongezeka kwa kiasi kikubwa miongoni mwa walio na tawahudi.[153]
  • Uaguzi wa mbelembele. Ingawa sheria ya DSM-IV inafutilia mbali uaguzi wa pamoja wa hali nyingine nyingi pamoja na tawahudi, kigezo kamili cha ADHD, ugonjwa wa Tourette, na hali nyingine kama hizi mara nyingi huwa zipo na uaguzi wa pamoja unazidi kukubalika.[154]
  • Matatizo ya usingizi huathiri takribani thuluthi mbili ya watu walio na ASD wakati fulani katika utoto. Kwa kawaida haya huwa ni pamoja na dalili za Kukosa usingizi kama vile matatizo ya kupata usingizi, kuamka usiku, na kupoteza usingizi mapema asubuhi. Matatizo ya usingizi yanayohusishwa na tabia zisizo za kawaida na msongo wa kifamilia, na mara nyingi huangaziwa katika matibabu mbali na uaguzi wa kimsingi wa ASD.[155]

Historia

Mifano michache ya dalili za tawahudi na matibabu yalifafanuliwa kitambo kabla ya tawahudi kutajwa. Kitabu cha Table Talk cha Martin Luther kina hadithi ya mvulana wa umri wa miaka 12 ambaye yawezekana alikuwa tawahudi shadidi.[156] Kwa mujibu wa katibu wa Luther, Mathesius, Luther alidhani mvulana huyo alikuwa pande la mtu aliye na roho ngumu aliyepagawa shetani, na akashauri kwamba asongwe pumzi.[157] Kumbukumbu nzuri ya awali ya tukio la tawahudi ni ile ya Hugh Blair wa Borgue, kama inavyoelezwa katika kesi ya mahakama ya 1747 ambapo ndugu yake kwa ufanisi alibatilisha ndoa ya Blair ili kupata urithi wa Blair.[158] The Wild Boy of Aveyron, mtoto mwitu aliyekamatwa mwaka wa 1798, alionyesha ishara kadhaa za tawahudi; mwanafunzi wa fani ya kimatibabu Jean Itard alimtibu kwa kutumia mipangilio ya kitabia iliyoundwa kumsaidia kuwa na utangamano wa kijamii na kuchochea uzungumzaji kwa njia ya kuiga.[159]

Neno la Kilatini Kipya autismus (Tafsiri ya Kiingereza Autism) liliasisiwa na mtaalamu wa magonjwa ya akili wa Kiswizi Eugen Bleuler mwaka wa 1910 alipokuwa akifafanua dalili za skizofrenia. Aliunyumbua kutoka neno la Kigiriki autós (αὐτός, maana yake -mwenyewe), na kulitumia kumaanisha uvutiwaji wa kibinafsi usio mwema, akimaanisha "kujitenga kwa mgonjwa wa tawahudi na kuwa katika kaputi zake mwenyewe, ambapo ushawishi mwingine kutoka nje unakuwa ni usumbufu usiovumilika".[160]

Head and shoulders of a man in his early 60s in coat and tie, facing slightly to his right. He is balding and has a serious but slightly smiling expression.
Leo Kanner ilianzisha kauli early infantile Autism katika 1943.

Neno Autism kwa mara ya kwanza lilichukua maana yake ya kisasa mwaka wa 1938 wakati Hans Asperger wa Chuo Kikuu cha Vienna Hospital alipochukua istilahi ya Bleuler autistic psychopaths katika mhadhara nchini Ujerumani kuhusu saikolojia ya watoto.[161] Asperger alikuwa akichunguzi aina ya ASD ambayo sasa inajulikana kama dalili za Aspaja, japo kwa sababu mbalimbali haikutambuliwa kuwa uaguzi tofauti hadi 1981.[159] Leo Kanner wa John Hopkins Hospital kwa mara ya kwanza alitumia Autism katika maana yeke ya kisasa katika Kiingereza wakati alipoanzisha kauli infantile Autism katika ripoti ya 1943 ya watoto 11 waliokuwa na tabia zinazofanana sana.[30] Takribani sifa zote zilivyoelezewa katika maandiko ya kwanza ya Kanner kuhusu, hasa "upweke wa kitawahudi" na "matukio ya kutobadilika" bado yanachukuliwa kuwa matatizo ya wigo wa tawahudi.[58] Haijulikani ikiwa Kanner alibuni neno hilo bila kutegemea mtazamo wa Asperger.[162]

Utumizi upya wa Kanner wa Autism ulisababisha miongo kadhaa ya kuchanganyikiwa kiistilahi kama vile skizofrenia ya utotoni, na mkazo wa wataalamu wa akili za watoto kuhusu mapungufu ya ulezi wa mama yalipelekea uelewa mbaya wa tawahudi jisni mtoto alivyoitikia akina "mama majokofu ". Kuanzia mwishoni mwa miaka ya 1960 tawahudi ilitengwa kuwa ugonjwa tofauti kwa kudhihirisha kuwa ni tatizo la maisha yote, na kuutofautisha na taahira ya akili na skizofrenia na tofauti na matatizo mengine ya ukuaji, na kuonyesha faida ya kuwashirikisha wazazi katika mipango kakamavu ya matibabu.[163] Hata katikati ya miaka ya 1970 kulikuwa na ushahidi mdogo wa wa athari ya kijenetiki katika tawahudi, sasa inadhaniwa kuwa mmoja ya matatizo ya akili inayoweza kurithika.[164] Ingawa kuchipuka kwa mashirika ya wazazi na kutonyanyapaliwa kwa ASD ya utotoni yameathiri pakubwa jinsi tunavyoichukulia ASD,[159] wazazi wanaendelea kuhisi unyanyapaa wa kijamii katika hali ambapo tabia za watoto wao wenye tawahudi yanachukuliwa vibaya na wengine,[165] na wengi wa madaktari wa huduma za msingi na madaktari bingwa bado huonyesha baadhi huzingati amani inayooana na utafiti wa zamani kuhusu tawahudi.[166] Mtandao imewasaidia watu wenye tawahudi kusambaziana jumbe zisizo za mazungumzo na kubadilishana hisia ambazo wao hupata ugumu kukabiliana nazo, na imewapa njia ya kuunda jamii za tovuti na kazi kutoka mbali.[167] Mielekeo ya kijamii na kidesturi ya tawahudi imesitawi: wengine katika jamii hutafuta tiba, huku wengine wakiaamini kwamba tawahudi ni njia nyingine tu ya maisha.[12][168]

Marejeo

  1. 1.0 1.1 1.2 American Psychiatric Association. Diagnostic and Statistical Manual of Mental Disorders. 4th, text revision (DSM-IV-TR) ed. 2000. ISBN 0890420254. Diagnostic criteria for 299.00 Autistic Disorder.
  2. 2.0 2.1 2.2 2.3 2.4 2.5 2.6 2.7 Levy SE, Mandell DS, Schultz RT. Autism. Lancet. 2009;374(9701):1627–38. doi:10.1016/S0140-6736(09)61376-3. PMID 19819542.
  3. 3.0 3.1 3.2 3.3 3.4 Johnson CP, Myers SM, Council on Children with Disabilities. Identification and evaluation of children with autism spectrum disorders. Pediatrics. 2007;120(5):1183–215. doi:10.1542/peds.2007-2361. PMID 17967920. Lay summary: AAP, 2007-10-29.
  4. 4.0 4.1 4.2 4.3 Abrahams BS, Geschwind DH. Advances in autism genetics: on the threshold of a new neurobiology. Nat Rev Genet. 2008;9(5):341–55. doi:10.1038/nrg2346. PMID 18414403.
  5. 5.0 5.1 5.2 Arndt TL, Stodgell CJ, Rodier PM. The teratology of autism. Int J Dev Neurosci. 2005;23(2–3):189–99. doi:10.1016/j.ijdevneu.2004.11.001. PMID 15749245.
  6. 6.0 6.1 6.2 Rutter M. Incidence of autism spectrum disorders: changes over time and their meaning. Acta Paediatr. 2005;94(1):2–15. doi:10.1080/08035250410023124. PMID 15858952.
  7. Hitilafu ya kutaja: Invalid <ref> tag; no text was provided for refs named vaccines
  8. 8.0 8.1 8.2 8.3 8.4 Newschaffer CJ, Croen LA, Daniels J et al. The epidemiology of autism spectrum disorders [PDF]. Annu Rev Public Health. 2007;28:235–58. doi:10.1146/annurev.publhealth.28.021406.144007. PMID 17367287.
  9. 9.0 9.1 9.2 9.3 9.4 9.5 9.6 Myers SM, Johnson CP, Council on Children with Disabilities. Management of children with autism spectrum disorders. Pediatrics. 2007;120(5):1162–82. doi:10.1542/peds.2007-2362. PMID 17967921. Lay summary: AAP, 2007-10-29.
  10. Hitilafu ya kutaja: Invalid <ref> tag; no text was provided for refs named Stefanatos
  11. 11.0 11.1 Howlin P, Goode S, Hutton J, Rutter M. Adult outcome for children with autism. J Child Psychol Psychiatry. 2004;45(2):212–29. doi:10.1111/j.1469-7610.2004.00215.x. PMID 14982237.
  12. 12.0 12.1 Silverman C. Fieldwork on another planet: social science perspectives on the autism spectrum. Biosocieties. 2008;3(3):325–41. doi:10.1017/S1745855208006236.
  13. 13.0 13.1 Geschwind DH. Autism: many genes, common pathways? Cell. 2008;135(3):391–5. doi:10.1016/j.cell.2008.10.016. PMID 18984147.
  14. 14.0 14.1 14.2 World Health Organization. F84. Pervasive developmental disorders; 2007 [cited 2009-10-10].
  15. Rogers SJ. What are infant siblings teaching us about autism in infancy? Autism Res. 2009;2(3):125–37. doi:10.1002/aur.81. PMID 19582867.
  16. 16.0 16.1 16.2 16.3 16.4 16.5 Rapin I, Tuchman RF. Autism: definition, neurobiology, screening, diagnosis. Pediatr Clin North Am. 2008;55(5):1129–46. doi:10.1016/j.pcl.2008.07.005. PMID 18929056.
  17. 17.0 17.1 17.2 [59] ^ Filipek PA, Accardo PJ, Baranek GT et al. The screening and diagnosis of autistic spectrum disorders. J Autism Dev Disord. 1999;29(6):439–84. doi:10.1023/A:1021943802493. PMID 10638459. Chapisho hili linawakilisha makubaliano ya wawakilishi kutoka mashirika tisa ya wataalamu na nne za wazazi yaliyo Marekani
  18. 18.0 18.1 18.2 London E. The role of the neurobiologist in redefining the diagnosis of autism. Brain Pathol. 2007;17(4):408–11. doi:10.1111/j.1750-3639.2007.00103.x. PMID 17919126.
  19. Sacks O. An Anthropologist on Mars: Seven Paradoxical Tales. Knopf; 1995. ISBN 0679437851.
  20. 20.0 20.1 20.2 20.3 [107] ^ Volkmar F, Chawarska K, Klin A. Autism in infancy and early childhood. Annu Rev Psychol. 2005;56:315–36. doi:10.1146/annurev.psych.56.091103.070159. PMID 15709938. Usasaishaji mdogo unapatikana kwa: Volkmar FR, Chawarska K. Autism in infants: an update. World Psychiatry. 2008;7(1):19–21. PMID 18458791.
  21. Sigman M, Dijamco A, Gratier M, Rozga A. Early detection of core deficits in autism. Ment Retard Dev Disabil Res Rev. 2004;10(4):221–33. doi:10.1002/mrdd.20046. PMID 15666338.
  22. Rutgers AH, Bakermans-Kranenburg MJ, van IJzendoorn MH, van Berckelaer-Onnes IA. Autism and attachment: a meta-analytic review. J Child Psychol Psychiatry. 2004;45(6):1123–34. doi:10.1111/j.1469-7610.2004.t01-1-00305.x. PMID 15257669.
  23. 23.0 23.1 23.2 Sigman M, Spence SJ, Wang AT. Autism from developmental and neuropsychological perspectives. Annu Rev Clin Psychol. 2006;2:327–55. doi:10.1146/annurev.clinpsy.2.022305.095210. PMID 17716073.
  24. 24.0 24.1 24.2 Burgess AF, Gutstein SE. Quality of life for people with autism: raising the standard for evaluating successful outcomes. Child Adolesc Ment Health. 2007;12(2):80–6. doi:10.1111/j.1475-3588.2006.00432.x.
  25. 25.0 25.1 25.2 Dominick KC, Davis NO, Lainhart J, Tager-Flusberg H, Folstein S. Atypical behaviors in children with autism and children with a history of language impairment. Res Dev Disabil. 2007;28(2):145–62. doi:10.1016/j.ridd.2006.02.003. PMID 16581226.
  26. Långström N, Grann M, Ruchkin V, Sjöstedt G, Fazel S. Risk factors for violent offending in autism spectrum disorder: a national study of hospitalized individuals. J Interpers Violence. 2008;24(8):1358–70. doi:10.1177/0886260508322195. PMID 18701743.
  27. Noens I, van Berckelaer-Onnes I, Verpoorten R, van Duijn G. The ComFor: an instrument for the indication of augmentative communication in people with autism and intellectual disability. J Intellect Disabil Res. 2006;50(9):621–32. doi:10.1111/j.1365-2788.2006.00807.x. PMID 16901289.
  28. 28.0 28.1 28.2 Landa R. Early communication development and intervention for children with autism. Ment Retard Dev Disabil Res Rev. 2007;13(1):16–25. doi:10.1002/mrdd.20134. PMID 17326115.
  29. 29.0 29.1 29.2 Tager-Flusberg H, Caronna E. Language disorders: autism and other pervasive developmental disorders. Pediatr Clin North Am. 2007;54(3):469–81. doi:10.1016/j.pcl.2007.02.011. PMID 17543905.
  30. 30.0 30.1 [437] ^ Kanner L. Autistic disturbances of affective contact. Nerv Child. 1943;2:217–50. Imechapishwa tena katika Acta Paedopsychiatr. 1968;35(4):100–36. PMID 4880460.
  31. 31.0 31.1 Williams DL, Goldstein G, Minshew NJ. Neuropsychologic functioning in children with autism: further evidence for disordered complex information-processing. Child Neuropsychol. 2006;12(4–5):279–98. doi:10.1080/09297040600681190. PMID 16911973.
  32. 32.0 32.1 Lam KSL, Aman MG. The Repetitive Behavior Scale-Revised: independent validation in individuals with autism spectrum disorders. J Autism Dev Disord. 2007;37(5):855–66. doi:10.1007/s10803-006-0213-z. PMID 17048092.
  33. Bodfish JW, Symons FJ, Parker DE, Lewis MH. Varieties of repetitive behavior in autism: comparisons to mental retardation. J Autism Dev Disord. 2000;30(3):237–43. doi:10.1023/A:1005596502855. PMID 11055459.
  34. Treffert DA. The savant syndrome: an extraordinary condition. A synopsis: past, present, future. Philos Trans R Soc Lond B Biol Sci. 2009;364(1522):1351–7. doi:10.1098/rstb.2008.0326. PMID 19528017. Lay summary: Wisconsin Medical Society.
  35. Plaisted Grant K, Davis G. Perception and apperception in autism: rejecting the inverse assumption. Philos Trans R Soc Lond B Biol Sci. 2009;364(1522):1393–8. doi:10.1098/rstb.2009.0001. PMID 19528022.
  36. 36.0 36.1 36.2 36.3 36.4 36.5 Geschwind DH. Advances in autism. Annu Rev Med. 2009;60:367–80. doi:10.1146/annurev.med.60.053107.121225. PMID 19630577.
  37. Rogers SJ, Ozonoff S. Annotation: what do we know about sensory dysfunction in autism? A critical review of the empirical evidence. J Child Psychol Psychiatry. 2005;46(12):1255–68. doi:10.1111/j.1469-7610.2005.01431.x. PMID 16313426.
  38. Ben-Sasson A, Hen L, Fluss R, Cermak SA, Engel-Yeger B, Gal E. A meta-analysis of sensory modulation symptoms in individuals with autism spectrum disorders. J Autism Dev Disord. 2009;39(1):1–11. doi:10.1007/s10803-008-0593-3. PMID 18512135.
  39. Fournier KA, Hass CJ, Naik SK, Lodha N, Cauraugh JH. Motor coordination in autism spectrum disorders: a synthesis and meta-analysis. J Autism Dev Disord. 2010. doi:10.1007/s10803-010-0981-3. PMID 20195737.
  40. Erickson CA, Stigler KA, Corkins MR, Posey DJ, Fitzgerald JF, McDougle CJ. Gastrointestinal factors in autistic disorder: a critical review. J Autism Dev Disord. 2005;35(6):713–27. doi:10.1007/s10803-005-0019-4. PMID 16267642.
  41. Buie T, Campbell DB, Fuchs GJ 3rd et al. Evaluation, diagnosis, and treatment of gastrointestinal disorders in individuals with ASDs: a consensus report. Pediatrics. 2010;125(Suppl 1):S1–18. doi:10.1542/peds.2009-1878C. PMID 20048083.
  42. Montes G, Halterman JS. Psychological functioning and coping among mothers of children with autism: a population-based study. Pediatrics. 2007;119(5):e1040–6. doi:10.1542/peds.2006-2819. PMID 17473077.
  43. Orsmond GI, Seltzer MM. Siblings of individuals with autism spectrum disorders across the life course [PDF]. Ment Retard Dev Disabil Res Rev. 2007;13(4):313–20. doi:10.1002/mrdd.20171. PMID 17979200.
  44. Volkmar FR, State M, Klin A. Autism and autism spectrum disorders: diagnostic issues for the coming decade. J Child Psychol Psychiatry. 2009;50(1–2):108–15. doi:10.1111/j.1469-7610.2008.02010.x. PMID 19220594.
  45. Freitag CM. The genetics of autistic disorders and its clinical relevance: a review of the literature. Mol Psychiatry. 2007;12(1):2–22. doi:10.1038/sj.mp.4001896. PMID 17033636.
  46. 46.0 46.1 46.2 46.3 46.4 Caronna EB, Milunsky JM, Tager-Flusberg H. Autism spectrum disorders: clinical and research frontiers. Arch Dis Child. 2008;93(6):518–23. doi:10.1136/adc.2006.115337. PMID 18305076.
  47. Piven J, Palmer P, Jacobi D, Childress D, Arndt S. Broader autism phenotype: evidence from a family history study of multiple-incidence autism families [PDF]. Am J Psychiatry. 1997;154(2):185–90. PMID 9016266.
  48. Happé F. Understanding assets and deficits in autism: why success is more interesting than failure [PDF]. Psychologist. 1999;12(11):540–7.
  49. Baron-Cohen S. The hyper-systemizing, assortative mating theory of autism [PDF]. Prog Neuropsychopharmacol Biol Psychiatry. 2006;30(5):865–72. doi:10.1016/j.pnpbp.2006.01.010. PMID 16519981.
  50. Cohen D, Pichard N, Tordjman S et al. Specific genetic disorders and autism: clinical contribution towards their identification. J Autism Dev Disord. 2005;35(1):103–16. doi:10.1007/s10803-004-1038-2. PMID 15796126.
  51. 51.0 51.1 51.2 51.3 Landa RJ. Diagnosis of autism spectrum disorders in the first 3 years of life. Nat Clin Pract Neurol. 2008;4(3):138–47. doi:10.1038/ncpneuro0731. PMID 18253102.
  52. Ozonoff S, Heung K, Byrd R, Hansen R, Hertz-Picciotto I. The onset of autism: patterns of symptom emergence in the first years of life. Autism Res. 2008;1(6):320–328. doi:10.1002/aur.53. PMID 19360687.
  53. Altevogt BM, Hanson SL, Leshner AI. Autism and the environment: challenges and opportunities for research. Pediatrics. 2008;121(6):1225–9. doi:10.1542/peds.2007-3000. PMID 18519493.
  54. Reiss AL. Childhood developmental disorders: an academic and clinical convergence point for psychiatry, neurology, psychology and pediatrics. J Child Psychol Psychiatry. 2009;50(1-2):87–98. doi:10.1111/j.1469-7610.2008.02046.x. PMID 19220592.
  55. Piggot J, Shirinyan D, Shemmassian S, Vazirian S, Alarcón M. Neural systems approaches to the neurogenetics of autism spectrum disorders. Neuroscience. 2009;164(1):247–56. doi:10.1016/j.neuroscience.2009.05.054. PMID 19482063.
  56. Stephan DA. Unraveling autism. Am J Hum Genet. 2008;82(1):7–9. doi:10.1016/j.ajhg.2007.12.003. PMID 18179879.
  57. 57.0 57.1 Happé F, Ronald A. The 'fractionable autism triad': a review of evidence from behavioural, genetic, cognitive and neural research. Neuropsychol Rev. 2008;18(4):287–304. doi:10.1007/s11065-008-9076-8. PMID 18956240.
  58. 58.0 58.1 58.2 Happé F, Ronald A, Plomin R. Time to give up on a single explanation for autism. Nat Neurosci. 2006;9(10):1218–20. doi:10.1038/nn1770. PMID 17001340.
  59. 59.0 59.1 Beaudet AL. Autism: highly heritable but not inherited. Nat Med. 2007;13(5):534–6. doi:10.1038/nm0507-534. PMID 17479094.
  60. Buxbaum JD. Multiple rare variants in the etiology of autism spectrum disorders. Dialogues Clin Neurosci. 2009;11(1):35–43. PMID 19432386.
  61. Cook EH, Scherer SW. Copy-number variations associated with neuropsychiatric conditions. Nature. 2008;455(7215):919–23. doi:10.1038/nature07458. PMID 18923514.
  62. 62.0 62.1 Betancur C, Sakurai T, Buxbaum JD. The emerging role of synaptic cell-adhesion pathways in the pathogenesis of autism spectrum disorders. Trends Neurosci. 2009;32(7):402–12. doi:10.1016/j.tins.2009.04.003. PMID 19541375.
  63. 63.0 63.1 Walsh CA, Morrow EM, Rubenstein JL. Autism and brain development. Cell. 2008;135(3):396–400. doi:10.1016/j.cell.2008.10.015. PMID 18984148.
  64. 64.0 64.1 Szpir M. Tracing the origins of autism: a spectrum of new studies. Environ Health Perspect. 2006;114(7):A412–8. PMID 16835042. PMC 1513312.
  65. Kinney DK, Munir KM, Crowley DJ, Miller AM. Prenatal stress and risk for autism. Neurosci Biobehav Rev. 2008;32(8):1519–32. doi:10.1016/j.neubiorev.2008.06.004. PMID 18598714.
  66. Müller RA. The study of autism as a distributed disorder. Ment Retard Dev Disabil Res Rev. 2007;13(1):85–95. doi:10.1002/mrdd.20141. PMID 17326118.
  67. Amaral DG, Schumann CM, Nordahl CW. Neuroanatomy of autism. Trends Neurosci. 2008;31(3):137–45. doi:10.1016/j.tins.2007.12.005. PMID 18258309.
  68. Casanova MF. The neuropathology of autism. Brain Pathol. 2007;17(4):422–33. doi:10.1111/j.1750-3639.2007.00100.x. PMID 17919128.
  69. Courchesne E, Pierce K, Schumann CM et al. Mapping early brain development in autism. Neuron. 2007;56(2):399–413. doi:10.1016/j.neuron.2007.10.016. PMID 17964254.
  70. 70.0 70.1 Schmitz C, Rezaie P. The neuropathology of autism: where do we stand? Neuropathol Appl Neurobiol. 2008;34(1):4–11. doi:10.1111/j.1365-2990.2007.00872.x. PMID 17971078.
  71. 71.0 71.1 71.2 Persico AM, Bourgeron T. Searching for ways out of the autism maze: genetic, epigenetic and environmental clues. Trends Neurosci. 2006;29(7):349–58. doi:10.1016/j.tins.2006.05.010. PMID 16808981.
  72. Südhof TC. Neuroligins and neurexins link synaptic function to cognitive disease. Nature. 2008;455(7215):903–11. doi:10.1038/nature07456. PMID 18923512.
  73. Kelleher RJ 3rd, Bear MF. The autistic neuron: troubled translation? Cell. 2008;135(3):401–6. doi:10.1016/j.cell.2008.10.017. PMID 18984149.
  74. Tuchman R, Moshé SL, Rapin I. Convulsing toward the pathophysiology of autism. Brain Dev. 2009;31(2):95–103. doi:10.1016/j.braindev.2008.09.009. PMID 19006654.
  75. Ashwood P, Wills S, Van de Water J. The immune response in autism: a new frontier for autism research. J Leukoc Biol. 2006;80(1):1–15. doi:10.1189/jlb.1205707. PMID 16698940.
  76. Stigler KA, Sweeten TL, Posey DJ, McDougle CJ. Autism and immune factors: a comprehensive review. Res Autism Spectr Disord. 2009;3(4):840–60. doi:10.1016/j.rasd.2009.01.007.
  77. Wills S, Cabanlit M, Bennett J, Ashwood P, Amaral D, Van de Water J. Autoantibodies in autism spectrum disorders (ASD). Ann N Y Acad Sci. 2007;1107:79–91. doi:10.1196/annals.1381.009. PMID 17804535.
  78. Hughes JR. A review of recent reports on autism: 1000 studies published in 2007. Epilepsy Behav. 2008;13(3):425–37. doi:10.1016/j.yebeh.2008.06.015. PMID 18627794.
  79. 79.0 79.1 Manzi B, Loizzo AL, Giana G, Curatolo P. Autism and metabolic diseases. J Child Neurol. 2008;23(3):307–14. doi:10.1177/0883073807308698. PMID 18079313.
  80. Frith U, Frith CD. Development and neurophysiology of mentalizing [PDF]. Philos Trans R Soc Lond B Biol Sci. 2003;358(1431):459–73. doi:10.1098/rstb.2002.1218. PMID 12689373. PMC 1693139.
  81. Hamilton AFdC. Emulation and mimicry for social interaction: a theoretical approach to imitation in autism. Q J Exp Psychol. 2008;61(1):101–15. doi:10.1080/17470210701508798. PMID 18038342.
  82. Broyd SJ, Demanuele C, Debener S, Helps SK, James CJ, Sonuga-Barke EJS. Default-mode brain dysfunction in mental disorders: a systematic review. Neurosci Biobehav Rev. 2009;33(3):279–96. doi:10.1016/j.neubiorev.2008.09.002. PMID 18824195.
  83. Chiu PH, Kayali MA, Kishida KT et al. Self responses along cingulate cortex reveal quantitative neural phenotype for high-functioning autism. Neuron. 2008;57(3):463–73. doi:10.1016/j.neuron.2007.12.020. PMID 18255038. Lay summary: Technol Rev, 2007-02-07.
  84. Just MA, Cherkassky VL, Keller TA, Kana RK, Minshew NJ. Functional and anatomical cortical underconnectivity in autism: evidence from an FMRI study of an executive function task and corpus callosum morphometry. Cereb Cortex. 2007;17(4):951–61. doi:10.1093/cercor/bhl006. PMID 16772313.
  85. Murias M, Webb SJ, Greenson J, Dawson G. Resting state cortical connectivity reflected in EEG coherence in individuals with autism. Biol Psychiatry. 2007;62(3):270–3. doi:10.1016/j.biopsych.2006.11.012. PMID 17336944.
  86. Minshew NJ, Williams DL. The new neurobiology of autism: cortex, connectivity, and neuronal organization. Arch Neurol. 2007;64(7):945–50. doi:10.1001/archneur.64.7.945. PMID 17620483.
  87. Jeste SS, Nelson CA 3rd. Event related potentials in the understanding of autism spectrum disorders: an analytical review. J Autism Dev Disord. 2009;39(3):495–510. doi:10.1007/s10803-008-0652-9. PMID 18850262.
  88. Roberts TP, Schmidt GL, Egeth M et al. Electrophysiological signatures: magnetoencephalographic studies of the neural correlates of language impairment in autism spectrum disorders. Int J Psychophysiol. 2008;68(2):149–60. doi:10.1016/j.ijpsycho.2008.01.012. PMID 18336941.
  89. 89.0 89.1 Baron-Cohen S. Autism: the empathizing–systemizing (E-S) theory [PDF]. Ann N Y Acad Sci. 2009;1156:68–80. doi:10.1111/j.1749-6632.2009.04467.x. PMID 19338503.
  90. Spelke ES. Sex differences in intrinsic aptitude for mathematics and science?: a critical review [PDF]. Am Psychol. 2005;60(9):950–8. doi:10.1037/0003-066X.60.9.950. PMID 16366817.
  91. Hitilafu ya kutaja: Invalid <ref> tag; no text was provided for refs named Iacoboni
  92. Hamilton AFdC. Goals, intentions and mental states: challenges for theories of autism. J Child Psychol Psychiatry. 2009;50(8):881–92. doi:10.1111/j.1469-7610.2009.02098.x. PMID 19508497.
  93. 93.0 93.1 Kenworthy L, Yerys BE, Anthony LG, Wallace GL. Understanding executive control in autism spectrum disorders in the lab and in the real world. Neuropsychol Rev. 2008;18(4):320–38. doi:10.1007/s11065-008-9077-7. PMID 18956239.
  94. O'Hearn K, Asato M, Ordaz S, Luna B. Neurodevelopment and executive function in autism. Dev Psychopathol. 2008;20(4):1103–32. doi:10.1017/S0954579408000527. PMID 18838033.
  95. Hill EL. Executive dysfunction in autism. Trends Cogn Sci. 2004;8(1):26–32. doi:10.1016/j.dr.2004.01.001. PMID 14697400.
  96. Happé F, Frith U. The weak coherence account: detail-focused cognitive style in autism spectrum disorders. J Autism Dev Disord. 2006;36(1):5–25. doi:10.1007/s10803-005-0039-0. PMID 16450045.
  97. Mottron L, Dawson M, Soulières I, Hubert B, Burack J. Enhanced perceptual functioning in autism: an update, and eight principles of autistic perception. J Autism Dev Disord. 2006;36(1):27–43. doi:10.1007/s10803-005-0040-7. PMID 16453071.
  98. Rajendran G, Mitchell P. Cognitive theories of autism. Dev Rev. 2007;27(2):224–60. doi:10.1016/j.dr.2007.02.001.
  99. Wetherby AM, Brosnan-Maddox S, Peace V, Newton L. Validation of the Infant–Toddler Checklist as a broadband screener for autism spectrum disorders from 9 to 24 months of age. Autism. 2008;12(5):487–511. doi:10.1177/1362361308094501. PMID 18805944.
  100. Wallis KE, Pinto-Martin J. The challenge of screening for autism spectrum disorder in a culturally diverse society. Acta Paediatr. 2008;97(5):539–40. doi:10.1111/j.1651-2227.2008.00720.x. PMID 18373717.
  101. Lintas C, Persico AM. Autistic phenotypes and genetic testing: state-of-the-art for the clinical geneticist. J Med Genet. 2009;46(1):1–8. doi:10.1136/jmg.2008.060871. PMID 18728070. PMC 2603481.
  102. Baird G, Cass H, Slonims V. Diagnosis of autism. BMJ. 2003;327(7413):488–93. doi:10.1136/bmj.327.7413.488. PMID 12946972. PMC 188387.
  103. 103.0 103.1 103.2 Dover CJ, Le Couteur A. How to diagnose autism. Arch Dis Child. 2007;92(6):540–5. doi:10.1136/adc.2005.086280. PMID 17515625.
  104. 104.0 104.1 Kanne SM, Randolph JK, Farmer JE. Diagnostic and assessment findings: a bridge to academic planning for children with autism spectrum disorders. Neuropsychol Rev. 2008;18(4):367–84. doi:10.1007/s11065-008-9072-z. PMID 18855144.
  105. Mantovani JF. Autistic regression and Landau–Kleffner syndrome: progress or confusion? Dev Med Child Neurol. 2000;42(5):349–53. doi:10.1017/S0012162200210621. PMID 10855658.
  106. Matson JL, Neal D. Cormorbidity: diagnosing comorbid psychiatric conditions. Psychiatr Times. 2009;26(4).
  107. Schaefer GB, Mendelsohn NJ. Genetics evaluation for the etiologic diagnosis of autism spectrum disorders. Genet Med. 2008;10(1):4–12. doi:10.1097/GIM.0b013e31815efdd7. PMID 18197051. Lay summary: Medical News Today, 2008-02-07.
  108. Ledbetter DH. Cytogenetic technology—genotype and phenotype. N Engl J Med. 2008;359(16):1728–30. doi:10.1056/NEJMe0806570. PMID 18784093.
  109. McMahon WM, Baty BJ, Botkin J. Genetic counseling and ethical issues for autism. Am J Med Genet C Semin Med Genet. 2006;142C(1):52–7. doi:10.1002/ajmg.c.30082. PMID 16419100.
  110. Shattuck PT, Durkin M, Maenner M et al. Timing of identification among children with an autism spectrum disorder: findings from a population-based surveillance study. J Am Acad Child Adolesc Psychiatry. 2009;48(5):474–83. doi:10.1097/CHI.0b013e31819b3848. PMID 19318992.
  111. National Autistic Society. Diagnosis: how can it benefit me as an adult?; 2005 [cited 2008-03-24].
  112. Shattuck PT, Grosse SD. Issues related to the diagnosis and treatment of autism spectrum disorders. Ment Retard Dev Disabil Res Rev. 2007;13(2):129–35. doi:10.1002/mrdd.20143. PMID 17563895.
  113. Cass H. Visual impairment and autism: current questions and future research. Autism. 1998;2(2):117–38. doi:10.1177/1362361398022002.
  114. Hitilafu ya kutaja: Invalid <ref> tag; no text was provided for refs named Powell
  115. Ospina MB, Krebs Seida J, Clark B et al. Behavioural and developmental interventions for autism spectrum disorder: a clinical systematic review. PLoS ONE. 2008;3(11):e3755. doi:10.1371/journal.pone.0003755. PMID 19015734. PMC 2582449.
  116. Krebs Seida J, Ospina MB, Karkhaneh M, Hartling L, Smith V, Clark B. Systematic reviews of psychosocial interventions for autism: an umbrella review. Dev Med Child Neurol. 2009;51(2):95–104. doi:10.1111/j.1469-8749.2008.03211.x. PMID 19191842.
  117. 117.0 117.1 117.2 117.3 Rogers SJ, Vismara LA. Evidence-based comprehensive treatments for early autism. J Clin Child Adolesc Psychol. 2008;37(1):8–38. doi:10.1080/15374410701817808. PMID 18444052.
  118. Howlin P, Magiati I, Charman T. Systematic review of early intensive behavioral interventions for children with autism. Am J Intellect Dev Disabil. 2009;114(1):23–41. doi:10.1352/2009.114:23;nd41. PMID 19143460.
  119. Eikeseth S. Outcome of comprehensive psycho-educational interventions for young children with autism. Res Dev Disabil. 2009;30(1):158–78. doi:10.1016/j.ridd.2008.02.003. PMID 18385012.
  120. Van Bourgondien ME, Reichle NC, Schopler E. Effects of a model treatment approach on adults with autism. J Autism Dev Disord. 2003;33(2):131–40. doi:10.1023/A:1022931224934. PMID 12757352.
  121. Leskovec TJ, Rowles BM, Findling RL. Pharmacological treatment options for autism spectrum disorders in children and adolescents. Harv Rev Psychiatry. 2008;16(2):97–112. doi:10.1080/10673220802075852. PMID 18415882.
  122. Oswald DP, Sonenklar NA. Medication use among children with autism spectrum disorders. J Child Adolesc Psychopharmacol. 2007;17(3):348–55. doi:10.1089/cap.2006.17303. PMID 17630868.
  123. Posey DJ, Stigler KA, Erickson CA, McDougle CJ. Antipsychotics in the treatment of autism. J Clin Invest. 2008;118(1):6–14. doi:10.1172/JCI32483. PMID 18172517. PMC 2171144.
  124. Buitelaar JK. Why have drug treatments been so disappointing? Novartis Found Symp. 2003;251:235–44; discussion 245–9, 281–97. doi:10.1002/0470869380.ch14. PMID 14521196.
  125. [333] ^ Ukosefu wa msaada kwa uingiliaji kati:
  126. Stahmer AC, Collings NM, Palinkas LA. Early intervention practices for children with autism: descriptions from community providers. Focus Autism Other Dev Disabl. 2005;20(2):66–79. doi:10.1177/10883576050200020301. PMID 16467905.
  127. Angley M, Semple S, Hewton C, Paterson F, McKinnon R. Children and autism—part 2—management with complementary medicines and dietary interventions [PDF]. Aust Fam Physician. 2007;36(10):827–30. PMID 17925903.
  128. Hediger ML, England LJ, Molloy CA, Yu KF, Manning-Courtney P, Mills JL. Reduced bone cortical thickness in boys with autism or autism spectrum disorder. J Autism Dev Disord. 2008;38(5):848–56. doi:10.1007/s10803-007-0453-6. PMID 17879151. Lay summary: NIH News, 2008-01-29.
  129. Brown MJ, Willis T, Omalu B, Leiker R. Deaths resulting from hypocalcemia after administration of edetate disodium: 2003–2005. Pediatrics. 2006;118(2):e534–6. doi:10.1542/peds.2006-0858. PMID 16882789.
  130. Consumer Price Index (estimate) 1800–2008. Federal Reserve Bank of Minneapolis. Retrieved December 7, 2010.
  131. Ganz ML. The lifetime distribution of the incremental societal costs of autism. Arch Pediatr Adolesc Med. 2007;161(4):343–9. doi:10.1001/archpedi.161.4.343. PMID 17404130. Lay summary: Harvard School of Public Health, 2006-04-25.
  132. Sharpe DL, Baker DL. Financial issues associated with having a child with autism. J Fam Econ Iss. 2007;28(2):247–64. doi:10.1007/s10834-007-9059-6.
  133. Montes G, Halterman JS. Association of childhood autism spectrum disorders and loss of family income. Pediatrics. 2008;121(4):e821–6. doi:10.1542/peds.2007-1594. PMID 18381511.
  134. Montes G, Halterman JS. Child care problems and employment among families with preschool-aged children with autism in the United States. Pediatrics. 2008;122(1):e202–8. doi:10.1542/peds.2007-3037. PMID 18595965.
  135. Reinke T. States increasingly mandate special autism services. Manag Care. 2008;17(8):35–6, 39. PMID 18777788.
  136. Aman MG. Treatment planning for patients with autism spectrum disorders. J Clin Psychiatry. 2005;66(Suppl 10):38–45. PMID 16401149.
  137. 137.0 137.1 Helt M, Kelley E, Kinsbourne M et al. Can children with autism recover? if so, how? Neuropsychol Rev. 2008;18(4):339–66. doi:10.1007/s11065-008-9075-9. PMID 19009353.
  138. Pickett E, Pullara O, O'Grady J, Gordon B. Speech acquisition in older nonverbal individuals with autism: a review of features, methods, and prognosis. Cogn Behav Neurol. 2009;22(1):1–21. doi:10.1097/WNN.0b013e318190d185. PMID 19372766.
  139. Seltzer MM, Shattuck P, Abbeduto L, Greenberg JS. Trajectory of development in adolescents and adults with autism. Ment Retard Dev Disabil Res Rev. 2004;10(4):234–47. doi:10.1002/mrdd.20038. PMID 15666341.
  140. Tidmarsh L, Volkmar FR. Diagnosis and epidemiology of autism spectrum disorders. Can J Psychiatry. 2003;48(8):517–25. PMID 14574827.
  141. Billstedt E, Gillberg C, Gillberg C. Autism after adolescence: population-based 13- to 22-year follow-up study of 120 individuals with autism diagnosed in childhood. J Autism Dev Disord. 2005;35(3):351–60. doi:10.1007/s10803-005-3302-5. PMID 16119476.
  142. Eaves LC, Ho HH. Young adult outcome of autism spectrum disorders. J Autism Dev Disord. 2008;38(4):739–47. doi:10.1007/s10803-007-0441-x. PMID 17764027.
  143. 143.0 143.1 143.2 Fombonne E. Epidemiology of pervasive developmental disorders. Pediatr Res. 2009;65(6):591–8. doi:10.1203/PDR.0b013e31819e7203. PMID 19218885.
  144. Wing L, Potter D. The epidemiology of autistic spectrum disorders: is the prevalence rising? Ment Retard Dev Disabil Res Rev. 2002;8(3):151–61. doi:10.1002/mrdd.10029. PMID 12216059.
  145. Gardener H, Spiegelman D, Buka SL. Prenatal risk factors for autism: comprehensive meta-analysis. Br J Psychiatry. 2009;195(1):7–14. doi:10.1192/bjp.bp.108.051672. PMID 19567888.
  146. Bertoglio K, Hendren RL. New developments in autism. Psychiatr Clin North Am. 2009;32(1):1–14. doi:10.1016/j.psc.2008.10.004. PMID 19248913.
  147. Folstein SE, Rosen-Sheidley B. Genetics of autism: complex aetiology for a heterogeneous disorder. Nat Rev Genet. 2001;2(12):943–55. doi:10.1038/35103559. PMID 11733747.
  148. Zafeiriou DI, Ververi A, Vargiami E. Childhood autism and associated comorbidities. Brain Dev. 2007;29(5):257–72. doi:10.1016/j.braindev.2006.09.003. PMID 17084999.
  149. Dawson M, Mottron L, Gernsbacher MA. Learning in autism [PDF]. In: Byrne JH, editor-in-chief, Roediger HL 3rd, volume editor. Learning and Memory: A Comprehensive Reference. Vol. 2. Academic Press; 2008. doi:10.1016/B978-012370509-9.00152-2. ISBN 0-12-370504-5. p. 759–72.
  150. Chakrabarti S, Fombonne E. Pervasive developmental disorders in preschool children. JAMA. 2001;285(24):3093–9. doi:10.1001/jama.285.24.3093. PMID 11427137.
  151. White SW, Oswald D, Ollendick T, Scahill L. Anxiety in children and adolescents with autism spectrum disorders. Clin Psychol Rev. 2009;29(3):216–29. doi:10.1016/j.cpr.2009.01.003. PMID 19223098.
  152. Spence SJ, Schneider MT. The role of epilepsy and epileptiform EEGs in autism spectrum disorders. Pediatr Res. 2009;65(6):599–606. doi:10.1203/PDR.0b013e31819e7168. PMID 19454962.
  153. Ozgen HM, Hop JW, Hox JJ, Beemer FA, van Engeland H. Minor physical anomalies in autism: a meta-analysis. Mol Psychiatry. 2010;15(3):300–7. doi:10.1038/mp.2008.75. PMID 18626481.
  154. Steyaert JG, De La Marche W. What's new in autism? Eur J Pediatr. 2008;167(10):1091–101. doi:10.1007/s00431-008-0764-4. PMID 18597114.
  155. Richdale AL, Schreck KA. Sleep problems in autism spectrum disorders: prevalence, nature, & possible biopsychosocial aetiologies. Sleep Med Rev. 2009;13(6):403–11. doi:10.1016/j.smrv.2009.02.003. PMID 19398354.
  156. Wing L. The history of ideas on autism: legends, myths and reality. Autism. 1997;1(1):13–23. doi:10.1177/1362361397011004.
  157. Miles M. Independent Living Institute. Martin Luther and childhood disability in 16th century Germany: what did he write? what did he say?; 2005 [cited 2008-12-23].
  158. Houston R, Frith U. Autism in History: The Case of Hugh Blair of Borgue. Blackwell; 2000. ISBN 0-631-22089-5.
  159. 159.0 159.1 159.2 Wolff S. The history of autism. Eur Child Adolesc Psychiatry. 2004;13(4):201–8. doi:10.1007/s00787-004-0363-5. PMID 15365889.
  160. [431] ^ Kuhn R; tr. Cahn CH. Eugen Bleuler's concepts of psychopathology. Hist Psychiatry. 2004;15(3):361–6. doi:10.1177/0957154X04044603. PMID 15386868. nukuu ni tafsiri ya halisi ya kitabu cha Bleuler cha 1910.
  161. Asperger H. [The psychically abnormal child]. Wien Klin Wochenschr. 1938;51:1314–7. German.
  162. Lyons V, Fitzgerald M. Asperger (1906–1980) and Kanner (1894–1981), the two pioneers of autism. J Autism Dev Disord. 2007;37(10):2022–3. doi:10.1007/s10803-007-0383-3. PMID 17922179.
  163. Fombonne E. Modern views of autism. Can J Psychiatry. 2003;48(8):503–5. PMID 14574825.
  164. Szatmari P, Jones MB. Genetic epidemiology of autism spectrum disorders. In: Volkmar FR. Autism and Pervasive Developmental Disorders. 2nd ed. Cambridge University Press; 2007. ISBN 0521549574. p. 157–78.
  165. Chambres P, Auxiette C, Vansingle C, Gil S. Adult attitudes toward behaviors of a six-year-old boy with autism. J Autism Dev Disord. 2008;38(7):1320–7. doi:10.1007/s10803-007-0519-5. PMID 18297387.
  166. Heidgerken AD, Geffken G, Modi A, Frakey L. A survey of autism knowledge in a health care setting. J Autism Dev Disord. 2005;35(3):323–30. doi:10.1007/s10803-005-3298-x. PMID 16119473.
  167. Biever C. Web removes social barriers for those with autism. New Sci. 2007;(2610):26–7.
  168. Harmon A. How about not 'curing' us, some autistics are pleading. New York Times. 2004-12-20.

Viungo vya nje

Wikimedia Commons ina media kuhusu:

Kigezo:Link GA Kigezo:Link FA Kigezo:Link FA Kigezo:Link FA