Clotilde Niragira : Tofauti kati ya masahihisho

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Content deleted Content added
Anzisha Makala Mpya
(Hakuna tofauti)

Pitio la 09:55, 10 Aprili 2022

Clotilde Niragira. (1968 – 19 Februari 2021) alikuwa mwanasiasa na mwanasheria wa Burundi. Alihudumu kama mkuu wa wizara tatu tofauti katika serikali ya Pierre Nkurunziza na alikuwa Katibu Mkuu wa Tume ya Ukweli na Maridhiano ya nchini Burundi.

HISTORIA YAKE KWA UFUPI

Clotilde Niragira alizaliwa katika Jumuiya ya Bugenyuzi katika Mkoa wa Karuzi, Burundi mnamo mwaka 1968. Aliolewa na alikuwa na watoto watatu na alikuwa wakili kabla ya kuingia kwenye siasa.[1] Mwaka 2005 aliteuliwa kuwa Waziri wa Sheria na Mlinzi wa Mihuri ya Serikali katika Baraza la Mawaziri la nchi hiyo na Rais Pierre Nkurunziza. Mnamo 2006, Niragira aliidhinisha kuachiliwa kwa wafungwa 3,300.[2] Aliteuliwa kuwa Waziri wa Utumishi wa Umma, Kazi na Usalama wa Jamii, na Nkurunziza katika mabadiliko ya baraza la mawaziri tarehe 14 Novemba 2007.[3][4]

Marejeo

  1. "Disparition de Clotilde Niragira ! – IWACU". www.iwacu-burundi.org. Iliwekwa mnamo 2022-04-10.
  2. Ambos, Kai; Large, Judith; Wierda, Marieke (2008-12-04). Building a Future on Peace and Justice: Studies on Transitional Justice, Peace and Development The Nuremberg Declaration on Peace and Justice (kwa Kiingereza). Springer Science & Business Media. ISBN 978-3-540-85754-9.
  3. http://allafrica.com/stories/200711150797.html
  4. Turner, B. (2017-01-12). The Statesman's Yearbook 2009: The Politics, Cultures and Economies of the World (kwa Kiingereza). Springer. ISBN 978-1-349-74027-7.