Nenda kwa yaliyomo

Chuo Kikuu cha Ilorin

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Chuo Kikuu Cha Ilorin)

Chuo Kikuu cha Ilorin, kinachojulikana pia kama Unilorin, ni chuo kikuu kinachomilikiwa na serikali ya shirikisho kilichopo Ilorin, Jimbo la Kwara, Nigeria.[1]Chuo kikuu kipo kwenye eneo kubwa la ardhi, takriban hekta 15,000 katika mji wa kale wa Ilorin; na hivyo kuwa chuo kikuu kikubwa zaidi nchini Nigeria na mojawapo ya vikubwa zaidi barani Afrika kwa ukubwa wa ardhi. Chuo kikuu kina jumla ya vitivo 17 na zaidi ya idara 100 za masomo. Kilianzishwa kwa amri ya serikali ya kijeshi ya shirikisho mnamo Agosti, 1975.[2]

  1. Pulse Contributor (2018-05-09). "List of Federal Universities in Nigeria". Pulse Nigeria (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2024-07-13. {{cite web}}: |author= has generic name (help)
  2. "National Universities Commission". web.archive.org. 2015-04-26. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2015-04-26. Iliwekwa mnamo 2024-07-13.{{cite web}}: CS1 maint: bot: original URL status unknown (link)