Visiwa vya Mariana ya Kaskazini

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Commonwealth of the Northern Mariana Islands
Sankattan Siha Na Islas Mariånas
Bendera ya Visiwa vya Mariana ya Kaskazini Nembo ya Visiwa vya Mariana ya Kaskazini
Bendera Nembo
Kaulimbiu ya taifa:
Wimbo wa taifa: Gi Talo Gi Halom Tase (Kichamoru)
Satil Matawal Pacifico (Kikarolini)
Lokeshen ya Visiwa vya Mariana ya Kaskazini
Mji mkuu Saipan
15°15′ N 145°45′ E
Mji mkubwa nchini
Lugha rasmi Kiingereza , Kichamoru, Kikarolini
Serikali Serikali ya kiraisi Demokrasia
Donald Trump
Eloy Inos
Eneo la ng'ambo la Marekani
Mkataba

1975
Eneo
 - Jumla
 - Maji (%)
 
463.63 km² (ya 196)
‘‘(kidogo sana)’’
Idadi ya watu
 - 2010 kadirio
 - Msongamano wa watu
 
53,833 ()
116.1/km² (93)
Fedha US Dollar (USD)
Saa za eneo
 - Kiangazi (DST)
(UTC+10)
(UTC)
Intaneti TLD .mp
Kodi ya simu +1 670

-


Visiwa vya Mariana ya Kaskazini ni eneo la ng'ambo la Marekani linalojitawala katika Pasifiki ya magharibi, kusini kwa Japani.

Jiografia[hariri | hariri chanzo]

Visiwa 16 vyenye eneo la kilometa mraba 463 jumla ni sehemu ya funguvisiwa ya Mariana na vikubwa ni Saipan, Tinian na Rota. Sehemu ya kusini ya funguvisiwa ni Guam ambayo pia ni eneo la ng'ambo la Marekani.

Historia[hariri | hariri chanzo]

Wakazi wa kwanza wanaojulikana ni Wachamoru.

Tangu mwaka 1667 visiwa vilikuwa koloni la Hispania.

Baada ya vita ya Marekani dhidi Hispania sehemu ya kusini ya Mariana ikatwaliwa na Marekani. Kaskazini ikauzwa kwa Ujerumani.

Baada ya vita kuu ya kwanza ya dunia makoloni ya Ujerumani ziligawiwa kwa nchi mbalimbali na Mariana ya Kaskazini ziliwekwa chini ya utawala wa Japani.

Baada ya Vita Kuu ya Pili ya Dunia visiwa vikawa sehemu ya eneo lindwa la Pasifiki lililotawaliwa na Marekani.

Mwaka 1978 visiwa vikapata madaraka ya kujitawala kwa ushirikiano na Marekani. Guam, ambapo kuna kituo muhimu cha kijeshi, inaendelea kuwa kama koloni la Marekani.

Watu[hariri | hariri chanzo]

Wachamorro ndio wakazi asili.

Idadi ya wakazi imefikia 53,883 (2010): kati yao 50% wana asili ya Asia (Wafilipino, Wachina, Wakorea, Wajapani, Wabangladesh n.k.). Wakazi asili ni 37.9% tu.

Upande wa dini, wengi wao ni Wakatoliki (64.1%).

Uchumi[hariri | hariri chanzo]

Uchumi unategemea hasa utalii.

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]



Majimbo na maeneo ya Marekani
Majimbo ya Marekani
AlabamaAlaskaArizonaArkansasCaliforniaColoradoConnecticutDelawareFloridaGeorgiaHawaiiIdahoIllinoisIndianaIowaKansasKentuckyLouisianaMaineMarylandMassachusettsMichiganMinnesotaMississippiMissouriMontanaNebraskaNevadaNew HampshireNew JerseyNew MexicoNew YorkNorth CarolinaNorth DakotaOhioOklahomaOregonPennsylvaniaRhode IslandSouth CarolinaSouth DakotaTennesseeTexasUtahVermontVirginiaWashingtonWest VirginiaWisconsinWyoming
Mkoa wa Mji Mkuu
Mkoa wa Columbia (Washington D.C.)
Visiwa vya ng'ambo
Katika Pasifiki: Samoa ya MarekaniVisiwa vya Mariana ya KaskaziniGuamKatika Karibi: Puerto RicoVisiwa vya Virgin vya MarekaniVisiwa vidogo sana vya Pasifiki:Kisiwa cha HowlandKisiwa cha Jarvis Atolli ya JohnstonKingman ReefAtolli ya MidwayKisiwa cha BakerAtolli ya PalmyraKisiwa cha WakeKisiwa kidogo cha Karibi: Kisiwa cha Navassa
Makala hii kuhusu eneo fulani bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu eneo hilo kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Je, unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.


Usitaje majina ya madiwani na viongozi au maafisa wengine wa sasa maana wanabadilika haraka mno.