Visiwa vya Solomon

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
(Elekezwa kutoka Solomon Islands)
Solomon Islands
Bendera ya Visiwa vya Solomon Nembo ya Visiwa vya Solomon
Bendera Nembo
Kaulimbiu ya taifa: To Lead is to Serve (Kuongoza ni kuhudumia)
Wimbo wa taifa: God Save Our Solomon Islands
Mungu abariki Visiwa vyetu vya Solomon
Lokeshen ya Visiwa vya Solomon
Mji mkuu Honiara
9°28′ S 159°49′ E
Mji mkubwa nchini Honiara
Lugha rasmi Kiingereza
Serikali Ufalme wa kikatiba
Charles III wa Uingereza
David Vunagi
Manasseh Sogavare
uhuru
tarehe

7 Julai 1978
Eneo
 - Jumla
 - Maji (%)
 
28,400 km² (ya 142)
3.2%
Idadi ya watu
 - Julai 2018 kadirio
 - Msongamano wa watu
 
652,857 (ya 167)
18.1/km² (ya 200)
Fedha Dollar ya Solomoni (SBD)
Saa za eneo
 - Kiangazi (DST)
(UTC+11)
(UTC)
Intaneti TLD .sb
Kodi ya simu +677

-


Ramani ya Solomoni

Visiwa vya Solomon ni nchi ya visiwani ya Melanesia katika Bahari ya Pasifiki iliyoko mashariki kwa Papua Guinea Mpya.

Eneo lake ni visiwa karibu 1000, vyenye jumla ya km² 28,400 na wakazi 652,857, wengi wakiwa Wamelanesia (95.3%), wakiongea lugha 90. Lugha rasmi ni Kiingereza.

Kati yao 97.4% ni Wakristo wa madhehebu mbalimbali, kuanzia Anglikana na Katoliki (19%).

Mji mkuu ni Honiara kwenye kisiwa cha Guadalcanal.

Historia[hariri | hariri chanzo]

Visiwa vimekaliwa tangu miaka elfu kadhaa na Wamelanesia.

Kuanzia karne ya 19 vilikuwa koloni la Ujerumani na la Uingereza.

Wakati wa Vita Kuu ya Pili ya Dunia mapigano makali kati ya Japani na Marekani yalitokea hapo.

Visiwa vilipata uhuru mwaka 1978.

Mashujaa wa visiwa vya Solomon wakiwa na silaha

Tazama pia[hariri | hariri chanzo]


Makala hii kuhusu eneo fulani bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu eneo hilo kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Je, unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.


Usitaje majina ya madiwani na viongozi au maafisa wengine wa sasa maana wanabadilika haraka mno.