Ulumbi
Ulumbi, kwa asili ya neno, ni sifa ya matumizi bora ya lugha (tafakari chanzo cha neno katika kitenzi cha Kiswahili: kulumba, yaani kutumia maneno vizuri). Wataalamu mbalimbali wameutumia ulumbi kumaanisha "uhodari wa kutumia lugha ili kufaulisha mawasiliano" (Buliba et al 2006:65) au "sifa ya kutumia maneno mengi" (Wamitila 2003: 291). Wengine lakini wameutumia sawa na uwingilugha, yaani uwezo wa kutumia lugha mbili au zaidi (k.m. TUKI 1990: 41; Massamba 2004: 101).
Chini ya kipengele cha kwanza cha ulumbi, yaani uhodari wa kutumia lugha, kuna umahiri na umilisi.
Chini ya kipengele cha pili cha ulumbi, yaani uwezo wa kutumia lugha nyingi, kuna ujozilugha, ubadilishaji msimbo na diglosia.
Marejeo [hariri]
- Buliba, Aswani, Kimani Njogu & Alice Mwihaki 2006, "Isimujamii kwa Wanafunzi wa Kiswahili", Nairobi: The Jomo Kenyatta Foundation
- Massamba, David 2004, "Kamusi ya Isimu na Falsafa ya Lugha", Chuo Kikuu cha Dar es Salaam
- TUKI 1990, "Kamusi Sanifu ya Isimu na Lugha", Chuo Kikuu cha Dar es Salaam
- Wamitila, Kyallo 2003, “Kamusi ya Fasihi – Istilahi na Nadharia”, Nairobi: Focus Books
Tazama pia [hariri]
Viambishi ni mofimu au viungo vyenye maana ambavyo hufungamanishwa na mzizi/shina la neno ili kulipa neno hilo maana mbalimbali za kisarufi kama vile nafsi, wakati, hali, urejeshi, n.k Viambishi awali ni vile vinavyotangulia mzizi wenyewe, yaani huwa kabla ya mzizi/shina. SHINA AU MZIZI: Hakuna tofauti kati ya shina na mzizi MZIZI/SHINA, Ni sehemu ya neno inayobeba maana yake kuu na huwa haibadiliki, Kwa mfano, tuangalie vitenzi vifuatavyo: a-na-LIM-a wa-li-LIM-i-a ni-ta-LIM-iw-a wa-na-vyo-LIM-a Ukiangalia kwa makini, utaona kuna sehemu ya kitenzi hiki ambayo haibadiliki katika mifano ya hapo juu. Sehemu hiyo ni (-LIM-). Na hii ndiyo shina au mzizi wa kitenzi LIMA. Mfano mwingine: a-li-ki-SOM-a hu-SOM-ew-a wa-li-SOM-e-an-a a-li-m-SOM-e-a i-li-SOM-w-a Tunaona hapa mzizi/shina la kitenzi SOMA, ni -som- Ili utambue shina/mzizi wa kitenzi unafaa kuwazia hali mbalimbali au kauli tofautitofauti za mnyambuliko wa kitenzi halafu ubainishe sehemu isiyobadilika.