Rombo
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Mahali pa Rombo (kijani) katika mkoa wa Kilimanjaro.
Rombo ni miongoni mwa wilaya sita za mkoa wa Kilimanjaro upande wa mashariki ya mlima. Mkuu ni makao makuu ya wilaya hiyo. Warombo ni sehemu ya Wachagga.
Wilaya imepakana na Kenya upande wa kaskazini na mashariki, wilaya ya Hai upande wa magharibi na wilaya ya Moshi vijijini upande wa Kusini.
Idadi ya wakazi ni 246,479 (sensa ya 2002) [1].
Viungo vya Nje [hariri]
| Makala hii kuhusu maeneo ya Mkoa wa Kilimanjaro bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Rombo kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |