Orodha ya wapiga gitaa wa Afrika

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Hii ni orodha ya wapiga gitaa maarufu barani Afrika.

Kialfabeti[hariri | hariri chanzo]

  • Barthelemy Attisso - mpigaji gitaa kiongozi wa bendi ya Orchestre Baobab, huko nchini Senegal.
  • Omara "Bombino" Moctar - mpigaji maarufu, mwimbaji na mtunzi kutoka mjini Agadez, Niger.
  • Alick Macheso - mpigaji gitaa mkuu wa bendi ya Orchestra Mberikwazvo, nchini  Zimbabwe.
  • Oliver De Coque - wa Ogene Sound Super of Africa
  • Mamadou Diop (pia anajulikana kama Modou Diop) - mpiga rizim gitaa wa kutoka Senegal, lakini kwa sasa yupo nchini Marekani
  • Afel Bocoum - Mpiga gitaa marufu kutoka nchini Mali, Ali Farka Touré ndiye mwalimu wake
  • Henri Bowane - Ni mtu mkubwa katika masuala mazima ya uanzishwaji wa rumba la Kikongo, wanafunzi wa awali wa Franco.
  • Diblo Dibala -  Mwanamuziki wa Kikongo ambaye maarufu kwa mtindo wa soukous, anafahamika kama "Machine Gun" kwa kasi na maarifa yke ya juu katika upigaji mzima wa gitaa.
  • Nico Kasanda (aka "Dr. Nico") - mmoja kati ya waanzilishi wa muziki wa soukous.
  • François Luambo Makiadi (aka "Franco") - Mwanamuziki wa Kikongo, mwanzilishi wa kundi zima la muziki wa Jazz maarufu OK Jazz.
  • Nico Mbarga - mpigaji gitaa mkuu na mtunzi maarufu wa wimbo maarufu wa "Sweet Mother."
  • Oliver Mtukudzi - Mpigaji gitaa kutoka nchini Zimbabwe na kiongozi wa 'Black Spirits'
  • Jean-Bosco Mwenda - Mwanzilishi wa mtindo wa Kiafrika maarufu "mtindo wa kidole" katika miaka ya 1950, Kongo
  • Ray Phiri- Mpigaji gitaa marufu kutoka mjini Mpumalanga, Afrika Kusini
  • Jonah Sithole Mpigaji gitaa kutoka nchini Zimbabwe, anapiga na Thomas Mapfumo
  • Djelimady Tounkara, mpiga gitaa maarufu wa bendi ya Super Rail Band kutoka mjini Bamako, Mali.
  • Ali Farka Touré - mwimbaji na mpiga gitaa kutoka nchini Mali.
  • Vieux Farka Touré - mtoto wa Ali Farka Touré, anachipukia kutoka nchini Mali.
  • Sir Victor Uwaifo- Mpigaji gitaa kutoka kwa watu wanaongea Kibini/Kiedo, yupo mjini Benin, Jimbo la  Edo, Nigeria.
  • Dr Sir Warrior - Mwimbaji na Mpigaji gitaa wa bendi ya Oriental Brothers International Band
  • Jonah Sithole - Mpiga mbira na gitaa marehemu ambaye awali alikuwa anapiga na Thomas Mapfumo
  • Joshua Dube - Mpigaji gitaa hayati ambaye awali alikuwa akipiga na Thomas Mapfumo
  • Habib Koité - mwimbaji na mpigaji gitaa kutoka nchini Senegal