Mtumiaji:Johteo/Umri wa kupiga kura

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Umri wa kupiga kura ni umri wa chini uliowekwa na sheria ambao mtu lazima afikie kabla ya kustahiki kupiga kura katika uchaguzi wa umma. Umri wa kawaida wa kupiga kura ni miaka 18; hata hivyo, umri wa kupiga kura ni chini ya miaka 16 na hadi 25 kwa sasa (tazama orodha hapa chini).[1] Nchi nyingi zimeweka umri wa chini zaidi wa kupiga kura, ambao mara nyingi huwekwa katika katiba yao. Katika nchi kadhaa kupiga kura ni lazima kwa wale wanaostahiki kupiga ilihali katika nyingi ni hiari.

Wakati haki ya kupiga kura ilipokuwa ikianzishwa katika demokrasia, umri wa kupiga kura uliwekwa kwa ujumla kuwa miaka 21 au zaidi katika miaka ya 1970 nchi nyingi zilipunguza umri wa kupiga kura hadi 18. Mjadala unaendelea katika nchi kadhaa kuhusu mapendekezo ya kupunguza umri wa kupiga kura au chini ya miaka 18. Nchini Brazil kwa kwa mfano umri wa chini ulipungua kutoka miaka 18 hadi 16 katika katiba ya 1988.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]

  1. Zeglovits, Eva; Aichholzer, Julian (2014-07-03). "Are People More Inclined to Vote at 16 than at 18? Evidence for the First-Time Voting Boost Among 16- to 25-Year-Olds in Austria". Journal of Elections, Public Opinion and Parties 24 (3): 351–361. ISSN 1745-7289. PMC 4864896. PMID 27226806. doi:10.1080/17457289.2013.872652.