Kisukari
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Kisukari (jina la kitaalamu: diabetes mellitus) ni ugonjwa unaoonyesha viwango vikubwa vya glukosi katika damu. Sababu yake ni uhaba wa homoni ya insulini mwilini au upungufu wa uwezo wa mwili wa kukubali insulini.
Dalili za kisukari ni
- kukojoa kupitia kiasi cha kawaida
- kiuu kikubwa
- kuona vibaya na matatizo ya macho hadi kuwa kipofu
- kuchoka haraka
- vidonda vinavyopoa polepole mno hasa kwenye miguu hadi kupotea viungo
Watu wachache huzaliwa na uhaba wa insulini. Watu walio wengi wana ushaifu fulani unaokuwa hatari kutokana na aina za vyakula na maisha ya kila siku. Kutumia sukari nyingi pamoja mafuta mengi katika chakula na vyinywaji, kukosa mazoezi ya mwili (kwa watu wenye kazi ofisini), kunywa pombe nyingi na kuvuta sigara huongeza hatari ya kushika kisukari kuanzia baada ya miaka ya ujana.
Viungo vya Nje [hariri]
- World Health Organization Diabetes Programme
- Juvenile Diabetes Research Foundation International
- American Diabetes Association
- Diabetes Forum
- Young Diabetic Community
- Canadian Diabetes Association
- Diabetes Australia
- Diabetes New Zealand
- Diabetes UK
- DiabetesFriends.net - Social Networking for Diabetics
- Diabetes Forum UK