Kindi-jua

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Kindi-jua
Kindi-jua kijivu (Heliosciurus gambianus)
Kindi-jua kijivu (Heliosciurus gambianus)
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Ngeli: Mammalia (Wanyama wenye viwele wanaonyonyesha wadogo wao)
Oda: Rodentia (Wagugunaji)
Nusuoda: Sciuromorpha (Wanyama kama kindi)
Familia: Sciuridae (Wanyama walio na mnasaba na kindi)
Muirhead, 1819
Nusufamilia: Xerinae (Wanyama wanaofanana na kindi)
Osborn, 1910
Kabila: Protoxerini (Wanyama wanaofanana sana na kindi)
Jenasi: Heliosciurus
Trouessart, 1880
Ngazi za chini

Spishi 6:

Kindi-jua ni wanyama wadogo wa jenasi Heliosciurus katika kabila Protoxerini la familia Sciuridae. Mkia yao una miviringo myeusi na kahawia au kijivu. Kama kindi wote spishi hizi hupitisha takribani saa zote mitini na huteremka kwa nadra ardhini. Hupatikana mara nyingi wakipumzika juani, sababu ya jina lao. Wanatokea misitu ya Afrika ya Magharibi, ya Kati na ya Mashariki kutoka Senegali mpaka Eritrea na Zimbabwe. Hula mbegu, makokwa, matunda, matumba, machipukizi, wadudu, mayai na mijusi, ndege na wanyama wadogo.

Spishi[hariri | hariri chanzo]

Picha[hariri | hariri chanzo]