Kiido

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Rukia: urambazaji, tafuta
Bandera ya Kiido

Kiido ni lugha ya kupangwa. Inafanana sana na Kiesperanto, lakini haizungumzwi na watu wengi kama Kiesperanto.

Serufi [hariri]

Nomino (majina) zote zinahitimu kwa kiambishi tawali -o, kwa mfano "arbo" (mti). Wingi wa nomino unahitimu kwa -i (arbi = miti).

Vivumishi vinahitimu kwa kiambishi tawali -a, kwa mfano "alta" (-refu).

Vitenzi vina viambishi tamati mbalimbali:

  • -ar inatumika kwa vitenzi-jina (kwa mfano "facar" = "kufanya")
  • -as inatumika kwa njeo ya wakati uliopo (kwa mfano "me facas" = "ninafanya"
  • -is inatumika kwa njeo ya wakati uliopita (kwa mfano "me facas" = "nilifanya" au "nimefanya")
  • -os inatumika kwa njeo ya wakati ujao (kwa mfano "me facos" = "nitafanya")
  • -us inatumika kwa hali a masharti (kwa mfano "me facus" = "ningefanya")
  • -ez inatumika kwa hali ya kuamuru (kwa mfano "facez!" = "fanya!"; "il facez" = "afanye")

Viungo vya nje [hariri]


Viambishi ni mofimu au viungo vyenye maana ambavyo hufungamanishwa na mzizi/shina la neno ili kulipa neno hilo maana mbalimbali za kisarufi kama vile nafsi, wakati, hali, urejeshi, n.k Viambishi awali ni vile vinavyotangulia mzizi wenyewe, yaani huwa kabla ya mzizi/shina. SHINA AU MZIZI: Hakuna tofauti kati ya shina na mzizi MZIZI/SHINA, Ni sehemu ya neno inayobeba maana yake kuu na huwa haibadiliki, Kwa mfano, tuangalie vitenzi vifuatavyo: a-na-LIM-a wa-li-LIM-i-a ni-ta-LIM-iw-a wa-na-vyo-LIM-a Ukiangalia kwa makini, utaona kuna sehemu ya kitenzi hiki ambayo haibadiliki katika mifano ya hapo juu. Sehemu hiyo ni (-LIM-). Na hii ndiyo shina au mzizi wa kitenzi LIMA. Mfano mwingine: a-li-ki-SOM-a hu-SOM-ew-a wa-li-SOM-e-an-a a-li-m-SOM-e-a i-li-SOM-w-a Tunaona hapa mzizi/shina la kitenzi SOMA, ni -som- Ili utambue shina/mzizi wa kitenzi unafaa kuwazia hali mbalimbali au kauli tofautitofauti za mnyambuliko wa kitenzi halafu ubainishe sehemu isiyobadilika.