Kialur
Kialur ni lugha ya Kinilo-Sahara nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Uganda inayozungumzwa na Waalur. Mwaka wa 2001 idadi ya wasemaji wa Kialur nchini Kongo imehesabiwa kuwa watu 750,000, na 2002 kulikuwa na wasemaji 617,000 nchini Uganda. Kufuatana na uainishaji wa lugha kwa ndani zaidi, Kialur kiko katika kundi la Kinilotiki.
Viungo vya nje[hariri]
- lugha ya Kialur kwenye Multitree
- ramani ya Kialur
- http://www.ethnologue.org/show_language.asp?code=alz
Viambishi ni mofimu au viungo vyenye maana ambavyo hufungamanishwa na mzizi/shina la neno ili kulipa neno hilo maana mbalimbali za kisarufi kama vile nafsi, wakati, hali, urejeshi, n.k Viambishi awali ni vile vinavyotangulia mzizi wenyewe, yaani huwa kabla ya mzizi/shina. SHINA AU MZIZI: Hakuna tofauti kati ya shina na mzizi MZIZI/SHINA, Ni sehemu ya neno inayobeba maana yake kuu na huwa haibadiliki, Kwa mfano, tuangalie vitenzi vifuatavyo: a-na-LIM-a wa-li-LIM-i-a ni-ta-LIM-iw-a wa-na-vyo-LIM-a Ukiangalia kwa makini, utaona kuna sehemu ya kitenzi hiki ambayo haibadiliki katika mifano ya hapo juu. Sehemu hiyo ni (-LIM-). Na hii ndiyo shina au mzizi wa kitenzi LIMA. Mfano mwingine: a-li-ki-SOM-a hu-SOM-ew-a wa-li-SOM-e-an-a a-li-m-SOM-e-a i-li-SOM-w-a Tunaona hapa mzizi/shina la kitenzi SOMA, ni -som- Ili utambue shina/mzizi wa kitenzi unafaa kuwazia hali mbalimbali au kauli tofautitofauti za mnyambuliko wa kitenzi halafu ubainishe sehemu isiyobadilika.