Hukwe Zawose
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Hukwe Zawose ((* 1940 Bugiri - † 30 Desemba 2003 Bagamoyo) huyu alikuwa ni mwanamuziki wa kiasili wa kitanzania, na muziki wake hasa ulikuwa ni wa kabila la Wagogo. Ala aliyotumia zaidi ilikuwa ilimbal pamoja na zeze; alipiga pia filimbi.
Kipaji chake cha muziki kiligunduliwa na aliyekuwa rais wa kwanza wa Tanzania hayati J. K. Nyerere wakati alipofanya ziara mkoa wa Dodoma. Alivutiwa na muziki wa Hukwe, na aliporudi Daressalaam alimuita Hukwe kwenye kikundi cha utamaduni cha Taifa Bagamoyo Players.
Katika miaka ya 1990 Zawose alirekodi muziki pamoja na Peter Gabriel na kutoa CD kadhaa.
Albamu Kadhaa [hariri]
- Tanzania Yetu (1989)
- Mateso (1989)
- The Miracle of the Thumb Piano in Tanzania (1989)
- Chibite (1996)
- Mkuki Wa Roho (2000)
- Assembly (2002)
Viungo vya Nje [hariri]
Sikiliza [hariri]
| Makala hii kuhusu muziki wa Afrika bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Hukwe Zawose kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |