Cherehani
Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Cherehani (pia: charahani; kutoka Kiajemi چرخ charakh "gurudumu" na خان khan "nyumba") ni mashine ya kushonea vitu kama kitambaa, nguo, viatu au mifuko.
Inatumia uzi kwa kuunganisha vipande viwili vya kitambaa au ngozi. Tofauti na ushonaji kwa mkono cherehani hutumia nyuzi mbili moja ya juu na nyingine ya chini zinazounganishwa.
Mwendo wa cherehani unatokana siku hizi mara nyingi na injini ya umeme. Kuna pia vyerehani vinavyosukumwa kwa mguu au kwa mkono.
Siku hizi kuna aina nyingi kwenye viwanda zilizobuniwa kwa shughuli maalum.
