Cherehani

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Cherehani cha zamani cha Singer
Jinsi ya kuunganisha uzi wa juu na uzi wa chini katika cherehani

Cherehani (pia: charahani; kutoka Kiajemi چرخ charakh "gurudumu" na خان khan "nyumba") ni mashine ya kushonea vitu kama kitambaa, nguo, viatu au mifuko.

Inatumia uzi kwa kuunganisha vipande viwili vya kitambaa au ngozi. Tofauti na ushonaji kwa mkono cherehani hutumia nyuzi mbili moja ya juu na nyingine ya chini zinazounganishwa.

Mwendo wa cherehani unatokana siku hizi mara nyingi na injini ya umeme. Kuna pia vyerehani vinavyosukumwa kwa mguu au kwa mkono.

Siku hizi kuna aina nyingi kwenye viwanda zilizobuniwa kwa shughuli maalum.

WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
WikiLettreMini.svg Makala hiyo kuhusu "Cherehani" bado ni mbegu. Unaweza kusaidia kuikuza kwa kubofya kitufe kilichoandikwa "hariri".

Ikiwepo makala kuhusu Cherehani kwa lugha nyingine, unaweza kuitafsiri kwa Kiswahili.