Sumcot

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Sumcot ni kituo cha mafunzo ya kompyuta katika mji wa Sumve, uliopo mkoa wa Mwanza, Tanzania. Ilianzishwa kwa msaada wa Wilde Ganzen, NGO ya Uholanzi na Sumve Foundation kwa lengo la kusaidia Hospitali Teule ya Wilaya ya Sumve (DDH).

Sumcot hutumika kufundisha makundi ya watu wafuatao katika ujuzi wa msingi wa kompyuta:

  • Wafanyakazi wa Sumve DDH
  • Wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana
  • Wanafunzi wa Shule ya sekondari ya Sumve (wavulana na wasichana)
  • Wanafunzi wa NMTC (Kituo cha Mafunzo ya Uuguzi na Ukunga)
  • Wananchi wengine wa Sumve, wanaotaka kupata/kuboresha ujuzi wa kompyuta

Kituo hicho katika mwezi Oktoba mwaka 2019 kilikuwa na kompyuta 16 za wanafunzi, pamoja na kompyuta moja ya mezani na kompyuta ndogo za mwalimu. Ina projekta inayotumika kuonyesha maonyesho kama sehemu ya masomo. Pia kuna mtandao wa eneo la ndani na seva ya faili ya kituo. Mwaka 2019 TTCL ilijenga mnara katika kituo cha Sumcot ambao utatoa huduma za mtandao wa haraka.

Marejeo[hariri | hariri chanzo]